minda
JF-Expert Member
- Oct 2, 2009
- 1,068
- 65
kwenye uchambuzi wa magazeti wa radio mbalimbali leo tumepata kusikia ya kwamba mkurugenzi wa uchaguzi rajabu kiravu amekanusha uwepo wa jimbo jipya la ushetu.
siku za karibuni imepata kusemwa ya kwamba lembeli alilikimbia jimbo la kahama na kuchukua fomu kwenye jimbo jipya la ushetu.
Lembeli amekuwa katika mvutano mkali wa kisiasa, kati yake na viongozi wengine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Kahama.
Uamuzi wa mbunge huyo kuhamia katika jimbo jipya, uliutangaza juzi baada ya Katibu wa CCM wa Wilaya ya Kahama, Sospeter Nyigoti, kutangaza kuwa wamepokea taarifa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kuwa imekubali kutangaza Jimbo ya Ushetu.
Baada ya taarifa hiyo, Lembeli alichukua na kujaza fomu ya kumwezesha kuomba kuteuliwa ili awanie ubunge katika jimbo hilo jipya badala ya jimbo lake la awali.
gonga hapa
sasa kwa mtindo huu sio kwamba lembeli sasa amekufa kisiasa? na huenda sio adhabu kwa kukosa staha? au tuseme chama chake kimeamua kumuingiza chaka ili apotee kwenye tasnia ya siasa hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa katika mvutano na uongozi wa chama chake wilayani?
yeyote mwenye thread atujuze ili tuwe na uhakika na ishu hii.
siku za karibuni imepata kusemwa ya kwamba lembeli alilikimbia jimbo la kahama na kuchukua fomu kwenye jimbo jipya la ushetu.
Lembeli amekuwa katika mvutano mkali wa kisiasa, kati yake na viongozi wengine wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Kahama.
Uamuzi wa mbunge huyo kuhamia katika jimbo jipya, uliutangaza juzi baada ya Katibu wa CCM wa Wilaya ya Kahama, Sospeter Nyigoti, kutangaza kuwa wamepokea taarifa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kuwa imekubali kutangaza Jimbo ya Ushetu.
Baada ya taarifa hiyo, Lembeli alichukua na kujaza fomu ya kumwezesha kuomba kuteuliwa ili awanie ubunge katika jimbo hilo jipya badala ya jimbo lake la awali.
gonga hapa
sasa kwa mtindo huu sio kwamba lembeli sasa amekufa kisiasa? na huenda sio adhabu kwa kukosa staha? au tuseme chama chake kimeamua kumuingiza chaka ili apotee kwenye tasnia ya siasa hasa ikizingatiwa kuwa alikuwa katika mvutano na uongozi wa chama chake wilayani?
yeyote mwenye thread atujuze ili tuwe na uhakika na ishu hii.