Mpaka sasa BAVICHA ndio taasisi bora ya vijana nchini.

Mpaka sasa BAVICHA ndio taasisi bora ya vijana nchini.

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Nimejaribu kufuatilia kwa makini sana kuhusu umakini na activeness ya vijana nchini nimegundua kua kila kinachosikika mitandaoni kuhusu maendeleo ya nchi, kila sintofamu, kila attention nchini ni kazi ya BAVICHA.

Ni taasisi ambayo kwakweli imekua ikitoa amsha amsha na uhamasishaji mkubwa sana kwa vijana na kuwafanya wajitambue. Ukisikia kuna kitu serikali inakanusha au inalalamika, ukifuatilia kwa makini unakuta source ya kuhoji ni BAVICHA.


Hii ni hazina kubwa sana kwa CHADEMA, chama kinatakiwa kuwalea vijana hawa kwa gharama yeyote ile kama mboni ya jicho maana matunda yake yanaweza yasionekane kwa sasa lakini baadaye ndio chachu kubwa ya mabadiliko nchini.

Hawa ndio vijana ambao Mwalimu Nyerere alisema taifa linawahitaji, "yaani vijana wakorofi,wajeuri,kwenye kujiamini na wasioogopa kuhoji, sio vijana wa ndio bwanamkubwa"
Hayo maneno nayaona kwa vijana hawa na ni kweli kua alichokisema mwalimu ndio kinachooneka kwao.
 
Ukweli ndio huo kama huamini angali hoja za Lumumba b7 kwenye uzi huu.
 
Ukweli ndio huo kama huamini angali hoja za Lumumba b7 kwenye uzi huu.
Ilifika mahali wakasema eti JF imenunuliwa na BAVICHA, sasa mbona hata kule fb na twitter hawasemi zimenunuliwa na BAVICHA?
 
Ila ukisema bila kumung'unya maneno,hawa wanaoitwa BAVICHA hua wanakuwa na hoja fikirishi kuliko wa upande wa pili ambao utaona wanakimbilia udini,ukabila na matusi.
 
Nisawa vijana wa chadema nimakini lakini chama hakina mipango vitega uchumi ningumu kushinda na chama chenye pesa
 
UVCCM KAZI YAO NI PROPAGANDA ZA UONGO ILI TU WAPATE KKULA NA SASA BWANA YULE KAWASHIKIA KOONI HAWAONEKANI.


SWISSME
 
Haihitaji akili ya ziada kujua kuwa huu uzi utakuwa wa kejeli na matusi toka pande mbili zenye uhasama.
 
Uvccm wazee wa ngonjera na midundiko
 
Bavicha iliyoimbishwa Edward mwizi mkuu nayo ikaimba,wimbo ukabadilishwa kuwa Edward ndiye mmbeba maono ya mabadiliko nayo ikacheza na kuimba kwa sauti pambio hilo,hii ndiyo bavicha bora kweli?bavicha ambaye viongozi wake hutoka mfukoni kwa mbowe huo ndio ubora siyo?bavicha ambayo leo wanaambiwa twende na ukuta,kesho wanaambiwa ukuta haupo kuna mazungumzo na viongozi wa dini,baadae wanaambiwa kuna kata funua hata wasihoji mrejesho wa mazungumzo na viongozi wa dini!hii ndiyo taasisi bora kweli?bavicha na uvccm tofauti zao ni majina tu mengine wanafanana kwa kila kitu!
 
Back
Top Bottom