nyendo kintu
Member
- May 31, 2011
- 20
- 2
Ndugu wanajamvi jana nimesoma post hapa kuwa nchi yetu inakalibia kufikia kiasi cha kutokopesheka kutokana na inavyokomba pesa kwenye taasisi za fedha! Maskini Mkwele! Napenda kuuliza hapa kwetu kuna sheria inayomlinda raia mwema pindi atoapo taarifa za watu wanaokwepa kodi? na sheria ikoje? maana nimechoka kuona watu hawalipi kodi na wanaikosesha serikali mapato mengi japo na magamba wataziiba! bila kusahau ni motisha kiasi gani inatolewa kwa kodi itakayokuwa recovered. Tusikate tamaa 2015 tutalinda kodi zetu wenyewe maana magamba hoi.