Moshi mweupe katika ndege zinazopita angani juu zaidi

Mzawa_G

JF-Expert Member
Feb 27, 2014
667
1,467
Nadhani katika kipindi chetu cha utoto tulikiwa tunapenda kuziita ndege za Urusi, yaani ni zile ndege ambazo zinapita anga la juu zaidi huku zikichora kitu mfano wa mstari wa moshi mzito sana.

Sasa leo nakufahamisha ambapo mstari huo kwa kitaalamu unafahamika kama Condensation Trails (Contrails).

Nataka nikuelekeze ni vipi moshi huo hutokea nyuma pindi ndege hizo zinapopita katika anga la juu zaidi.

Injini za ndege huzalisha mvuke mkubwa sana wenye joto kali huku kwa nyuma ambapo hukutana na hali ya hewa ya ubaridi kwenye anga la juu huko angani, mvuke huo wa joto unapokutana na ubaridi huunda kitu kama chenga chenga za barafu ambazo huganda na kubaki angani. Huku duniani huweza kuona kitu kama mfano wa wingu au moshi linalotawala sehemu yoyote ile ndege inapopita.

Nadhani kwa namna moja ama nyengine suala hili hufanana na ule mchakato wa wingu kujitengeneza, ambapo mvuke hutoka ardhini na kwenda juu unapokutana na hewa ya ubaridi basi huganda.

Moudyswema
Tanzaniascienceyetu
AstronomyKiswahili

FB_IMG_1679863072155.jpg
 
Mvuke huo wa joto unapokutana na ubaridi huunda kitu kama chenga chenga za barafu ambazo huganda na kubaki angani ,


Dah umetisha. Mwamba
 
Nadhani katika kipindi chetu cha utoto tulikiwa tunapenda kuziita ndege za Urusi , yaani ni zile ndege ambazo zinapita anga la juu zaidi huku zikichora kitu mfano wa mstari wa moshi mzito sana

Sasa leo nakufahamisha ambapo mstari huo kwa kitaalamu unafahamika kama Condensation Trails (Contrails)

Nataka nikuelekeze ni vipi moshi huo hutokea nyuma pindi ndege hizo zinapopita katika anga la juu zaidi

Injini za ndege huzalisha mvuke mkubwa sana wenye joto kali huku kwa nyuma ambapo hukutana na hali ya hewa ya ubaridi kwenye anga la juu huko angani , Mvuke huo wa joto unapokutana na ubaridi huunda kitu kama chenga chenga za barafu ambazo huganda na kubaki angani , Huku duniani huweza kuona kitu kama mfano wa wingu au moshi linalotawala sehemu yoyote ile ndege inapopita

Nadhani kwa namna moja ama nyengine suala hili hufanana na ule mchakato wa wingu kujitengeneza , Ambapo mvuke hutoka ardhini na kwenda juu unapokutana na hewa ya ubaridi basi huganda .

Moudyswema
Tanzaniascienceyetu
AstronomyKiswahili

View attachment 2567030
Tulikuwa tunaita roketi, tuliambiwa imeundwa mahsusi kusafirisha almasi/dhahabu toka Afrika Kusini kwenda Ulaya na haiwezi kutua kiwanja chochote ila ina viwanja vyake maalum
 
Nadhani katika kipindi chetu cha utoto tulikiwa tunapenda kuziita ndege za Urusi, yaani ni zile ndege ambazo zinapita anga la juu zaidi huku zikichora kitu mfano wa mstari wa moshi mzito sana.

Sasa leo nakufahamisha ambapo mstari huo kwa kitaalamu unafahamika kama Condensation Trails (Contrails).

Nataka nikuelekeze ni vipi moshi huo hutokea nyuma pindi ndege hizo zinapopita katika anga la juu zaidi.

Injini za ndege huzalisha mvuke mkubwa sana wenye joto kali huku kwa nyuma ambapo hukutana na hali ya hewa ya ubaridi kwenye anga la juu huko angani, mvuke huo wa joto unapokutana na ubaridi huunda kitu kama chenga chenga za barafu ambazo huganda na kubaki angani. Huku duniani huweza kuona kitu kama mfano wa wingu au moshi linalotawala sehemu yoyote ile ndege inapopita.

Nadhani kwa namna moja ama nyengine suala hili hufanana na ule mchakato wa wingu kujitengeneza, ambapo mvuke hutoka ardhini na kwenda juu unapokutana na hewa ya ubaridi basi huganda.

Moudyswema
Tanzaniascienceyetu
AstronomyKiswahili

View attachment 2567030
Unyevu nyevu ulioko angani ukikutana na gesi zenye joto kali kutoka kwenye exhaust (ekzost) ya ndege hugeuka kuwa mvuke, na ndicho unachokiona kama moshi mweupe !!
 
Back
Top Bottom