Moral and legal obligation

Zing

JF-Expert Member
Jun 24, 2009
1,767
470
Je kipi kina uzito kati ya maadili na sheria katika kufanya maamuzi.

Mfano
Fundi bomba kaenda kutengeza kitu kwenye nyumba ya bibi kizee. kufika anamwambia bibi kize kifaa kidogo tu kilichoharibika ukarabati wake utagahrimu Milioni 1. Bibi kizeee anamwabia haya tengeneza. Fundi anatengeneza.

Baada ya kutengenza bibi anakwenda benki na fundi kuchukua hela. kufika benki anandika kuwa anataka kutoa milioni moja. mafanyakazi wa benki anamuuliza za nini sababu si kawaida yake? Bibi anamjibu fundi bomba amekuja kurekebisha tatizo.

Mfanyakazi wa benki anapiga simu polisi. kuripoti kuwa kuna tapeli anamuibia bibi kizee .


  • Kisheria/ leggaly fundi bomba ana haki ya kulipwa sababu alipatana na bibi na bibi anakiri kabisa

  • Kimaadili/ ethcally alichofanya fundi bomba ni kama wizi.

assume wewe ni mwanasheria una maoni gani
 
Inawezekana huyo bibi kizee wakati anafanya makubaliano hayo na hata kipindi anachukua fedha benki hakuwa anaelewa anachokifanya kutokanan a uzee wake labda, inategemea alikuwa na umri gani, kwani inasemekana uzee ukizidi sana tabia zinabadilika mtu anarudi kwenye utoto na kufanya mambo kama mtoto! Ndio maana hata wasomi kwenye ngazi za maamuzi kama waheshimiwa Majaji kabla hata hawajafikisha umri wa kustaafu kikatiba; waki misbehave hawana budi kustaafishwa kwa mujibu wa katiba. Inawezekana kabisa huyo bibi kizee wakati anaingia huo mkataba hakuwa competent to contract, yaani not of sound mind na kupelekea mkataba huo kuwa batili. Hayo ni maoni yangu tu na sio sheria!
 
Kama kisheria kuna kosa la kulaghai au kurubuni fundi ana hatia,pia kimaadili amevunja maadili.moral and legal are equal in obligation but differ in penalties
 
Hambaza na kapo wanamaon mazur na yanamshko ksheria...hata hvo Ukkaa ukfkr the legal oblgation is the child ov moral oblgation.. Kuna mazngra meng yanathbtsha hlo kwanza na kubwa zaid ya yote n kwamba sheria inakuwa yaan inabadlka muda hadi muda kama uwezavyo kubadl ktambaa. Nafas ya jaj au hakmu pia inasaidia hvo kama hakmu ataesklza kes hyo atakuwa na wigo mpana zaid wa kuamua.
HAYA NI MAWAZO YANGU TU.
 
Back
Top Bottom