Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 17,572
- 27,314
Kumekuwa na hizi kauli za Mtetezi wa Wanyonge hivi karibuni..., Ila nadhani ni vema tukajiuliza myonge huyo ni nani na vipi anatetewa.
Binafsi nadhani myonge ni yule mwenye haki lakini hapewi haki yake na sio yule anayesaidiwa kuvunja haki / sheria sababu ya mapungufu / uhaba wa hiki au kile. Kwa hiyo kwangu mimi wanyonge ni wale ambao wamefanya kazi hawapewi au pension zao zinacheleweshwa, wana kesi hazisikilizwi kwa wakati, watoto wao wana akili/uwezo lakini hawapewi mikopo, ingawa wananchi wenzao wanalipa Kodi ila wakiugua wanakosa matibabu, ingawa serikali inakusanya kodi, hawapati huduma muhimu, wanatoa pesa/ wanakopeshwa ili wasome na wakimaliza wanaanza kudaiwa wakati walichosomeshwa hakiwafai/ hakiwezi kuwaingizia kipato (hao kwangu ndio wanyonge).
Wanyonge sio machinga wachuuzi (na kama ni wanyonge unyonge wao sio kuwa machinga) bali ni kwa nchi yao kukosa policies za kuwaondoa katika uchuuzi na kubangaiza / kubahatisha bila kuijua kesho yao, Pili kwa kuwaacha machinga waendelee kuchomwa jua kila kukicha bila kuwaandalia mazingira ya kuwatoa barabarani sio kuwatetea bali ni kwalaghai kwamba wao maisha yao pale ndio kikomo..., na kusema tu ninawapenda kwahio ninawaruhusu muingie popote (hata kama mnahatarisha maisha yenu) sio kuwapenda bali ni kutumia siasa/ propaganda na kuwahadaa.
Kama hio haitoshi watetezi hawa wa wanyonge wanaenda mbali zaidi ya kutengeneza chuki baina ya so called wanyonge na so called mafisadi/ wakwepa kodi (wafanyabiashara). Yaani badala ya hao watetezi wa wanyonge kuwashukuru wafanyabiashara wakubwa (so called wakwepa kodi) sababu wanatoa ajira kwa hawa wanyonge (kazi ambayo serikali imeshindwa) wanawaambia hawa wanyonge kwamba hawa ndio wakwepa kodi na wapiga deals, kwamba shida zenu sio sisi kukosa ubunifu bali ni wale walafi wanakula keki yote ya taifa.
Bila kujua ni vita gani tunapigana na nani tunapigana nae tunaweza kujikuta tunamalizana wenyewe kwa wenyewe wakati hao watetezi wetu ndio haswaaa hawafanyi kazi zao na hawatutetei bali wanatugombanisha.
Binafsi nadhani myonge ni yule mwenye haki lakini hapewi haki yake na sio yule anayesaidiwa kuvunja haki / sheria sababu ya mapungufu / uhaba wa hiki au kile. Kwa hiyo kwangu mimi wanyonge ni wale ambao wamefanya kazi hawapewi au pension zao zinacheleweshwa, wana kesi hazisikilizwi kwa wakati, watoto wao wana akili/uwezo lakini hawapewi mikopo, ingawa wananchi wenzao wanalipa Kodi ila wakiugua wanakosa matibabu, ingawa serikali inakusanya kodi, hawapati huduma muhimu, wanatoa pesa/ wanakopeshwa ili wasome na wakimaliza wanaanza kudaiwa wakati walichosomeshwa hakiwafai/ hakiwezi kuwaingizia kipato (hao kwangu ndio wanyonge).
Wanyonge sio machinga wachuuzi (na kama ni wanyonge unyonge wao sio kuwa machinga) bali ni kwa nchi yao kukosa policies za kuwaondoa katika uchuuzi na kubangaiza / kubahatisha bila kuijua kesho yao, Pili kwa kuwaacha machinga waendelee kuchomwa jua kila kukicha bila kuwaandalia mazingira ya kuwatoa barabarani sio kuwatetea bali ni kwalaghai kwamba wao maisha yao pale ndio kikomo..., na kusema tu ninawapenda kwahio ninawaruhusu muingie popote (hata kama mnahatarisha maisha yenu) sio kuwapenda bali ni kutumia siasa/ propaganda na kuwahadaa.
Kama hio haitoshi watetezi hawa wa wanyonge wanaenda mbali zaidi ya kutengeneza chuki baina ya so called wanyonge na so called mafisadi/ wakwepa kodi (wafanyabiashara). Yaani badala ya hao watetezi wa wanyonge kuwashukuru wafanyabiashara wakubwa (so called wakwepa kodi) sababu wanatoa ajira kwa hawa wanyonge (kazi ambayo serikali imeshindwa) wanawaambia hawa wanyonge kwamba hawa ndio wakwepa kodi na wapiga deals, kwamba shida zenu sio sisi kukosa ubunifu bali ni wale walafi wanakula keki yote ya taifa.
Bila kujua ni vita gani tunapigana na nani tunapigana nae tunaweza kujikuta tunamalizana wenyewe kwa wenyewe wakati hao watetezi wetu ndio haswaaa hawafanyi kazi zao na hawatutetei bali wanatugombanisha.