GE2025 Mnyika: Muunganiko wa INEC, NIDA na CCM ni tishio kwa demokrasia

GE2025 Mnyika: Muunganiko wa INEC, NIDA na CCM ni tishio kwa demokrasia

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, amesema kuwa madai ya kuunganisha mfumo wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ni tishio kwa uhuru wa uchaguzi nchini Tanzania.

Akizungumza Jumatano Agosti 27, 2025 katika mkutano wa mtandaoni ujulikanao kama Baraza la Kidigitali, Mnyika amesema muunganiko huo unaweza kuhatarisha usalama wa daftari la kudumu la wapigakura na kuacha mianya ya kuingiliwa na mamlaka za serikali.

Soma pia: Kwanini NIDA, INEC na CCM ghafla wamepanic na kuropoka ovyo ovyo kimfanano baada ya Pole pole kumwaga siri zao?

Screenshot 2025-08-27 065201.png


“Mjadala huu ulianza tangu mwaka 2005 hadi mwaka 2020, na sisi kama CHADEMA tulionesha mashaka yetu kwamba kuunganisha mifumo hii miwili- NIDA na INEC kutafanya daftari la wapigakura kuwa chini ya mamlaka ya serikali badala ya tume huru,” amesema Mnyika.

Mnyika amerejea pia kauli ya kada wa CCM na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, ambaye hivi karibuni alidai kuwa mifumo ya NIDA, INEC na CCM imekuwa ikihusishwa ili kuhakikisha chama tawala kinashinda uchaguzi. Kauli hiyo ya Polepole ililazimu wakuu wa taasisi husika kujitokeza hadharani na kukanusha.

Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, James Kaji, alisema madai hayo “hayana ukweli wowote,” huku akisisitiza hakuna mfumo wa NIDA uliowahi kufungamanishwa na chama cha siasa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa INEC, Ramadhan Kailima, kupitia taarifa ya Agosti 23, 2025, alikanusha kuwa mifumo ya uchaguzi imeunganishwa na NIDA au chama chochote cha siasa.

Kailima aliongeza kuwa Tanzania haitumii mfumo wa kielektroniki katika kupiga kura wala kuhesabu matokeo, bali utaratibu wa kawaida (manual). Aidha, alisisitiza kuwa kitambulisho cha taifa hakitumiki kupigia kura, badala yake ni kadi ya mpiga kura pekee iliyotolewa na INEC.

Pamoja na utetezi huo, Mnyika amesisitiza kuwa hali hiyo inaonesha udhaifu wa mfumo wa uchaguzi wa Tanzania na akatoa wito kwa serikali kuandikisha upya daftari la wapigakura. “Wakati umefika sasa wa kusema imetosha. Tutake reforms na tuendelee na msimamo wa No Reforms, No Election,” amesisitiza.

Kwa mujibu wa CHADEMA, mageuzi ya katiba na uhuru wa tume ya uchaguzi ni miongoni mwa masharti ya msingi ya kupata uchaguzi wa haki na huru nchini.
 
Mnyima ni full katibu mkuu.
Huo ukaimu ni wako na msajiri.

Hiyo lugha ya ukaimu ilikuwa kufunika kombe ili mwanaharamu apite....sasa mwanaharamu hajapita......kwahiyo cheo chake kimerejeshwa.
 
Kamamtakumbuka Mbowe alishitakiwa kwa ugaidi kidogo almanasura anyongwe akaokolewa na Kamanda Kingai kuwakamata wale mak9mandoo watatu wakinywa mbege nfiani kwenda kumuua Lengai ole Sabaya. Utakumbuka kuwa Mr Mbowe aliwalipa makomandoo Mia alarm ya laki sita sita kianzio kwa kumuua oke Sabaya na kulipua vitus vya sheli Temeke. Mtu wa tigopesa alithibitisha kuwa mifumo ya mbowe ya tihopesa ilikuwa inasomana na mfumo wa NIDA kuwalipa makomandoo. Mr Polepole ni mbabaishaji anajikita zaidi kwa "ujingawako" yaani self deception. Indeed, hata tone tone anazoibia hela Mr Heche nayo ni mfumo wa CHADEMA na VODACOM (baada ya kuhama tigopesa, mfumo ni huohuo).
 
Kamamtakumbuka Mbowe alishitakiwa kwa ugaidi kidogo almanasura anyongwe akaokolewa na Kamanda Kingai kuwakamata wale mak9mandoo watatu wakinywa mbege nfiani kwenda kumuua Lengai ole Sabaya. Utakumbuka kuwa Mr Mbowe aliwalipa makomandoo Mia alarm ya laki sita sita kianzio kwa kumuua oke Sabaya na kulipua vitus vya sheli Temeke. Mtu wa tigopesa alithibitisha kuwa mifumo ya mbowe ya tihopesa ilikuwa inasomana na mfumo wa NIDA kuwalipa makomandoo. Mr Polepole ni mbabaishaji anajikita zaidi kwa "ujingawako" yaani self deception. Indeed, hata tone tone anazoibia hela Mr Heche nayo ni mfumo wa CHADEMA na VODACOM (baada ya kuhama tigopesa, mfumo ni huohuo).
ROST. TAM
 
Back
Top Bottom