Mnyika kutikisa Handeni Leo

Mnyika kutikisa Handeni Leo

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Chama cha Demokrasia na Maendeleo leo kitafanya mkutano mkubwa wa hadhara katika jimbo la Handeni.

Taarifa ya Mkuu wa Habari wa chama hicho Tumaini Makene inasema mkutano huo wa hadhara wa kampeni za uchaguzi Jimbo la Handeni, utakaofanyika leo jioni mjini Handeni, mkoani Tanga, utahutubiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Chama, JJ Mnyika kuanzia saa 8 mchana.

Mojawapo ya masuala ya atakayoyazungumzia ni uchambuzi wa uteuzi wa Baraza la Mawaziri la JPM uliotangazwa jana. Unakaribishwa sana.

Mkutano huo pia utahudhuriwa na wabunge wa UKAWA.
 
Last edited by a moderator:
CDM imeibuka tena!! Watu wa Handeni hawataki kuzungusha; wao ni HAPA KAZI TU!!!
 
sawa ila waende na panadol kabisa maana mhutubiaji anasema mpaka povu litamtoka
 
mbona lowasa na sumaye hawaendi kuwasaidia wagombea wengine Wa ubunge. ie Handen wao kila cku kumpigia debe lema 2 arusha. Au hawana uhakika Wa kushinda sehem nyengine?
 
Waliofikiri JJM amesusa ati kisa CDM kubadilishia gia angani na DR. kuamua kusepa zake - na wajinyonge sasa ama wakae kimya milele!!

Watanzania bado tunayasubiri Mabadiliko ya kweli under UKAWA.
 
Chadema kinaendeleza siasa zake za matukio.eti uchambuzi wa baraza la JPM.watu wanataka majibu mbadala ya matatizo yao
 
Chadema kinaendeleza siasa zake za matukio.eti uchambuzi wa baraza la JPM.watu wanataka majibu mbadala ya matatizo yao


Pasipo kuwa na Baraza zuri lenye watendaji usitegemee kuapata hayo majibu mbadala ya matatizo yako. Utayasubiri hadi YESU atarudi wenzio wanakula kiulaniiiii wewe unapiga debe.

Lazima tukemee tupate baraza zuri lenye kuleta MABADILIKO YA KWELI TANZANIA.

Utamrudishaje Mwakyembe Wizarani!!!!!!!!!!!! Ana tuhuma ya Mabehewa Shirika la Reli na hajaongelea hata wakati wa kampeni kukanusha. Hivyo anaenda kuweka mikakati yakuiba tena.

Amepewa Wizara nyeti ili akaibe kwa kutumia mikataba feki na wawekezaji, pamoja na kutoa pesa BOT.
 
Mleta mada ndiye anajitekenya mwemyewe Na kucheka mwenyewe Na kuleta agenda ya Makofuli ba baraza lake
 
Ndio mnyika kawape vidonge vyao maana tumeletewa baraza magumashi
 
Back
Top Bottom