Mnyika kinara bungeni


Ndiyo maana nasema acheni uvivu wa kusoma. Muulize Magufuli majibu ya Mnyika kuhusu kituo cha Ubungo na wakati mwingine anapavamia pale Ubungo bila watu kuwa na taarifa.

Ni nani aliyebuni kuwepo na barabara za pembezoni ili kupunguza foleni za Dar ambako jiji zima ni foleni kila kona.

Unaposema kuwa wewe ni mkazi wa Ubungo ukumbuke hii ni JF hujui anaye-press keyboard yuko wapi na si ajabu anaishi nyumba mnayotizamana. Na hilo si la msingi.

Na hivi vigezo ndiyo maana halisi ya mbunge. Mabunge hafukuzwi kwa sababu akirudi jimboni analala. Ubunge ni uwakilishi mle bungeni. Hiyo definition yenu ni wenye njaa wametuzoesha na ndiyo tunayopigania kuondokana nayo maana hakuna sehemu ya katiba ya nchi yoyote duniani inasema mbunge kazi yake ni tofauti na ile ya uwakilishi eti kwamba imegeuka kuwa mhimizaji au mchangia maendeleo.

Mbunge akikutana na wananchi ni kwa mujibu wa kujua kero ili akamkamate waziri husik kule bungeni. Tafiti zaidi usipende tukumegee.
 

Mkuu M4C haitaacha mtu salama.CCM imeshikilia ubunge wa Ubungo miaka 50 huwalaumu bali unamlaumu Mnyika aliyeshika ubunge miaka 2
 
Mkuu wewe siku zote hakuna jema analofanya Mnyika...Mimi ni mkazi wa Ubungo na huyu ndiye mbunge bora ukilinganisha na wabunge wengine kwa kipindi cha miaka 20
Molemo nilijua utakuja tu tena nilitaka nikukaribishe. Mimi sina shida hata kidogo na JJ Mnyika. Namfahamu vizuri na sijawahi kumponda kwenye uchangiaji wake bungeni (kasoro ile ya dhaifu). Najua ni kijana makini na ana hoja makini za Kitaifa; sina shida na hilo. Tatizo langu ni kwamba Mnyika sasa arudi chini kwa watu waliomchagua aunganishe na hoja zake za kitaifa; asisahau waliompeleka huko kupata nafasi ya kuwa Kinara.

Nipe Ubora wake jimboni. Afadhali hata Keenja kwenye awamu yake ya kwanza.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu M4C haitaacha mtu salama.CCM imeshikilia ubunge wa Ubungo miaka 50 huwalaumu bali unamlaumu Mnyika aliyeshika ubunge miaka 2

Mkuu mimi siyo kwamba namlaumu kihivyo. Mkuu nami najivunia kuwa na Mbunge Kinara yaani Mnyika lakini ukinara wake urudi basi Jimboni ili na jimbo pia liwe Kinara. Sasa yeye Kinara jimbo siyo Kinara maana yake nini sasa?
 

Jaribu kurudisha akili nyuma ukumbuke maneno aliyomwambia Magufuli wakati anazindua kituo cha basi
Pia Mnyika kila anapomaliza mkutano wa bunge anafanya mikutano kila Kata kuchukua kero za wananchi kama wewe huhudhurii ni shauri yako hawezi kukufuata chumbani
Tatu naomba nikuambia watu wameichoka CCM na hilo ndilo la msingi zaidi.
 
Last edited by a moderator:

siyo eneo zuri kwa kuishi hata kidogo, maji mpaka mvua zinyeshe na zikinyesha hilo tope ni balaa tupu
 

Mkuu ni nani aliyebuni hizo barabara? Unamfahamu? Najua si Mnyika hata chembe. Yeye namshauri asimamie serikali kutekeleza ahadi ya chama tawala kuhusu hizo ring na bypass roads achilia mbali fly overs. Hapo najua utakuwa umetoka nje ya uwanja.

Kuhusu mbunge kusimamia serikali nalijua sana hilo ila katika hali ya sasa hilo peke yake halitamsaidia sana Mbunge. Mbunge anatakiwa ahamasishe maendeleo jimboni kwake ili wananchi chini ya uongozi wake wajiletee maendeleo. Mbunge ambaye ataitegemea serikali peke yake ilete maendeleo jimboni kwake hakika huyo si mbunge. Serikali ina vipaumbele ambavyo vingine ni tofauti na vya Mbunge na Jimbo. Wakati wabunge wanaomba kura na kutoa ahadi wakati wa kampeni walikuwa wamekubaliana na serikali kwamba nitatoa ahadi hizi kwa wanapiga kura wangu na serikali mtatekeleza kwa kuwa nitakuwa nawasimamia? Hapo ndipo hiyo gap inatakiwa izibwe na uhamasishaji ili wananchi wajiletee maendeleo.
 

Mkuu Molemo mimi diwani wangu ni Mwalimu Manota sasa muulize Mnyika amewahi kufika katani kwake mara ngapi? Nakumbuka aliwahi kuja Heche tukiuliza Mbunge tunaambiwa ana majukumu ya kitaifa. Nahudhuria sana mikutano tena hujui tu najitolea sana.

Watu wameichoka CCM sawa lakini sasa tufanye kazi ili jimbo liwe Kinara.

Jimbo la Ubungo zamani lilikuwa juu kuliko Temeke lakini hivi sasa Temeke inakuwa Kinara.

Mnyika turudishie ukinara Ubungo ili Ubungo iwe Kinara kama ulivyo Kinara Bungeni.
 
Mkuu laiti Mnyika angekuwa CCM ungemsifia vibaya sana....
Molemo mimi mbona namsifia sana Mnyika. Sina tatizo naye juu ya hoja zake. Najivunia kuwa na mbunge Kinara Bungeni tena siyo kwa kuangalia idadi ya michango tu bali contents za hiyo michango. Manake unaweza ukawa na michango mingi lakini pumba tupu; kwa Mnyika siyo hivyo.

Sasa Mbunge wangu ni Kinara kwa hoja maridhawa na mujarabu pale Mjengoni basi aje tushirikiane tulifanye jimbo letu pia Kinara hapa Dar. Mambo yatakuwa murua kabisa kwamba MBUNGE KINARA ANAONGOZA JIMBO KINARA.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu ningekushauri badala ya kuhangaika na Mnyika kwa kupiga propaganda ungefanya jitihada za kuleta mrejesho wa mbunge wa Ukonga ambaye tangu achaguliwe hajawahi kukutana na watu wake na ndiye mbunge ambaye nauli ya daladala kwenye jimbo lake ni Sh 1000 kutokana na ubovu wa barabara.Lakini huyu humsemei kwa vile ni kada mwenzio siyo?
 
big up kwa kuongea saaaanaaa bungeni lakini jimboni kunadoda hahahahaha...
 
naona anafuata nyayo zakatibu wake DR.slaa kwani nakumbuka kunaripoti zitoka kwaslaakupewa tuzo ya kuwa na mchango mkubwa bungeni kama sikosei.big up Mh.J.J.Mnyika
 
safi sana na ongeza juhudi zaidi Mh Nyika na wana wabunge wa CDM wote na wale wengine waliotoa michango yao mizuri kwa taifa.Kuna kitu kimoja ambacho wengi bado hatujakielewa wengi tunafikiri mbunge ndiyo mwenye kuleta maendeleo hapana hapa ndiyo tunapo kosea nisawa na wale wanaosema CDM imefanya nini mpaka tuichague? ndivyo ilivyo kwa Nyika na wabunge wengineo mnawalaumu hawajafanya kitu,ila ikumbukwe hawa hawakusanyi kodi au aina yoyote ile ya mapato.kutokuwa na maendeleo jimboni ni kutokana na bajeti finyu na mbunge akipinga bajeji akisema ni ndogo anazomewa na kuambiwa anatafuta umaarufu halafu bado anaambiwa hajafanya kitu jimboni kwake.Ila michango wanayoto bungeni na kushauri na hoja binafsi si tuu inasaidia bubge bali ni serekali ya chama chochote na taifa kwa ujumla labda iwe inatolewa kuchukuliwa na kuwekwa kapuni.Big up wabunge wote walio ingie 10 bora bado tunahitaji nguvu kazi yenu.
 
Barabara Kilungule vipi?
Moja ya michango yake inayompa juckpot ni swali kuhusu ujenzi wa barabara ya Kilungile kwa hiyo usihofu. Pia fahamu serikali ya CCM ingependa kumrudisha nyuma katika maendeleo ya jimbo ili kumchonganisha na wananchi.
 
Ikitolewa list ya wabunge wenye matusi,Lusinde no.1
 
ili kufanikiwa lazima uwe umeanzia mahali fulani. kama kafanya vizuri bungeni ni jambo zuri kwani tulimpeleka awatuwakilishe huko mjengoni. huko kafanikiwa bila shaka hata mambo ya kilungule yatafanikiwa, ila tusitake yote yafanikiwe kwa wakati mmoja , haiwezekani kijani. MBONA CCM WENYE MIAKA 50 BADO WANASEMA TUWE NA SUBIRA? miaka 50 mi sijafikisha, so..tangu nizaliwe bado wanakukuruka tu hawajatufikisha tunakotaka...huyu mnyika ana miaka 2 tu, mmeanza kumbebesha milawama ambayo ulitakiwa umuulize keenja kHaa jamani, watu bwana....
 
Mbunge wangu Aziz Abood amekuwa wangapi? maana sijawahi kumsikia Bungeni huyu. Ikiwezekana tutajiwe walioshika nafasi za chini wote ili tuwafukuze kazi 2015. Maana wengine wameenda kusinzia tu.
 
Swali zuri sana! Hii inatokana nakuto ogopa na kuweka maslai ya taifa mbele!

Pia nguvu ya kuchangia utokana na kuwa safi mbele ya jamii na kujiamini:

big up Mnyika umejitahd sana. lakin je wafikiri ni kwanini hawa wabunge wa CDM wameweza kufikia hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…