Fall Army Worm
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 19,331
- 14,259
Wakuu heshima zenu!
Mimi ninayeandika Haya naomba kudeclare interest kwamba pia ni Mtumishi wa Serikali yetu. Kinachonisikitisha, ni namna Watu mbalimbali wanavyotoa Kauli za Kuwadharau, Kuwabeza na Kuwapuuza Watumishi. Fikiri Matharani Mtu anasema kwamba Watumishi kwanini wadai nyongeza ya Mishahara wakati hakuna wanachozalisha. Kauli hii peke yake inaweza kushusha Morali ya kufanya Kazi, Binafsi Sina Shida na Serikali maana najua Yapo Majukumu mazito yanayolikabiri Taifa, mbali ya Nyongeza za Mishahara, najua Serikali inatupenda sema tu Mambo ni mengi.
Lakini swali kwanini Watu mnatudharau? Kosa letu ni lipi? Sasa Mlitaka tufanyeje ili mridhike kuwa sisi ni wa maana kwenu? Ndugu Zangu Si kila Kazi inayofanywa na Mtumishi wa Serikali lazima ionyeshe Matunda hapo hapo, Zipo kazi huonyesha Matunda baada ya muda mrefu mfano, Kazi ya Walimu, Maafisa Ugani, Ustawi wa Jamii, Utafiti, n. K. Huleta Matunda baada ya Muda Fulani kuwa umepita,ni Tofauti na Sekta km vile Viwanda, Afya, Kodi, n. K. Ambazo huleta Matunda on the spot.
Jamani hivi kuna watu humu wanawadharau hata Walimu, Mimi Naona mnatenda Dhambi, kwasababu hata Hiyo Jeuri na Kiburi cha Kuandika hapa ukimdharau ni kutokana na Kazi ya Mwalimu huyo unayemdharau na kumbeza kwa si lolote. Wewe unayemdharau Daktari, unafanya hivyo kwasababu uko vizuri Kiafya, subiri Ukamatwe na homa Kali tuone km utaweza kushika hata simu au Kompyuta, thubutu yako badala yake utabaki ukimlilia daktari akusaidie, Lkn sasa wajitia kiburi kuwa Hawa si chochote, haya bhana ipo Siku, MUNGU anakuona tu na huo mdomo wako.Wengine wamewadharau kada ya Kilimo kwamba hata layman wa kijijini aweza kuwa mtaalamu wa Kilimo, OK!
Sawa, lakini mbona yakizuka Magonjwa yale hatarishi kwa Mazao mnawakimbilia na kuwaomba Ushauri namna ya kuyatokomeza? .Mbona Ukame ulipo ikumba nchi msimu uliopita mlikuwa mkisisitiza kuwa Watafiti wa Kilimo wajitahidi kuzalisha mbegu za muda mfupi na zinazovumilia Ukame na Magonjwa?, Kwanini basi msingewaambia Hao layman wa Vijijini wawazalishie mbegu hizo?
Jamani acheni Dharau kwa Watumishi. Kutokana na Kauli za Wengi zinafanya nikumbuke ule msemo wa "NJAA MWANA MALEGEZA, SHIBE MWANA MALEVYA".Watu wakiwa ktk Hali ya Raha isiyo na mikiki mikiki yoyote ile wanaweza KULEWA na kumdharau kila mtu, ndio maana Baadhi ya watu waliojikinai na kulewa Maisha mazuri hudiriki Kusema "HAKUNA MUNGU ".Hiyo yote ni kwasababu hawana shida na wakitaka chochote wanakipata. Hawa hawatofautiani Sana na Wanawadharau Watumishi kwasababu Wao Wamejitosheleza na km sio kujitosheleza basi tuseme hawajawahi kutana na Shida kubwa iliyohitaji Msaada wa Mtaalamu Fulani wa Sekta fulani Serikalini.
Wacha nisiwachoshe. Ombi langu kwenu ni Moja, naomba TUHESHIMIANE, Kila Mmoja anao umuhimu, Km ambavyo MUNGU alituumba na kutuweka Dunia kila Mmoja kwasababu fulani na MUNGU alijua kuwa kila mmoja ana umuhimu wake Vivyo hivyo hata ktk Maisha, Kila mtu anao umuhimu wake, Mtumishi wa Kada yoyote ile ana umuhimu wake ndio maana Kada hiyo iliwekwa ili watu waisomee na waitumikie, halikadhalika Mwananchi wa kawaida naye anao umuhimu wake, Mmoja akikosekana, lazima Mkwamo wa mambo Fulani utokee tu.
Asanteni.
Mimi ninayeandika Haya naomba kudeclare interest kwamba pia ni Mtumishi wa Serikali yetu. Kinachonisikitisha, ni namna Watu mbalimbali wanavyotoa Kauli za Kuwadharau, Kuwabeza na Kuwapuuza Watumishi. Fikiri Matharani Mtu anasema kwamba Watumishi kwanini wadai nyongeza ya Mishahara wakati hakuna wanachozalisha. Kauli hii peke yake inaweza kushusha Morali ya kufanya Kazi, Binafsi Sina Shida na Serikali maana najua Yapo Majukumu mazito yanayolikabiri Taifa, mbali ya Nyongeza za Mishahara, najua Serikali inatupenda sema tu Mambo ni mengi.
Lakini swali kwanini Watu mnatudharau? Kosa letu ni lipi? Sasa Mlitaka tufanyeje ili mridhike kuwa sisi ni wa maana kwenu? Ndugu Zangu Si kila Kazi inayofanywa na Mtumishi wa Serikali lazima ionyeshe Matunda hapo hapo, Zipo kazi huonyesha Matunda baada ya muda mrefu mfano, Kazi ya Walimu, Maafisa Ugani, Ustawi wa Jamii, Utafiti, n. K. Huleta Matunda baada ya Muda Fulani kuwa umepita,ni Tofauti na Sekta km vile Viwanda, Afya, Kodi, n. K. Ambazo huleta Matunda on the spot.
Jamani hivi kuna watu humu wanawadharau hata Walimu, Mimi Naona mnatenda Dhambi, kwasababu hata Hiyo Jeuri na Kiburi cha Kuandika hapa ukimdharau ni kutokana na Kazi ya Mwalimu huyo unayemdharau na kumbeza kwa si lolote. Wewe unayemdharau Daktari, unafanya hivyo kwasababu uko vizuri Kiafya, subiri Ukamatwe na homa Kali tuone km utaweza kushika hata simu au Kompyuta, thubutu yako badala yake utabaki ukimlilia daktari akusaidie, Lkn sasa wajitia kiburi kuwa Hawa si chochote, haya bhana ipo Siku, MUNGU anakuona tu na huo mdomo wako.Wengine wamewadharau kada ya Kilimo kwamba hata layman wa kijijini aweza kuwa mtaalamu wa Kilimo, OK!
Sawa, lakini mbona yakizuka Magonjwa yale hatarishi kwa Mazao mnawakimbilia na kuwaomba Ushauri namna ya kuyatokomeza? .Mbona Ukame ulipo ikumba nchi msimu uliopita mlikuwa mkisisitiza kuwa Watafiti wa Kilimo wajitahidi kuzalisha mbegu za muda mfupi na zinazovumilia Ukame na Magonjwa?, Kwanini basi msingewaambia Hao layman wa Vijijini wawazalishie mbegu hizo?
Jamani acheni Dharau kwa Watumishi. Kutokana na Kauli za Wengi zinafanya nikumbuke ule msemo wa "NJAA MWANA MALEGEZA, SHIBE MWANA MALEVYA".Watu wakiwa ktk Hali ya Raha isiyo na mikiki mikiki yoyote ile wanaweza KULEWA na kumdharau kila mtu, ndio maana Baadhi ya watu waliojikinai na kulewa Maisha mazuri hudiriki Kusema "HAKUNA MUNGU ".Hiyo yote ni kwasababu hawana shida na wakitaka chochote wanakipata. Hawa hawatofautiani Sana na Wanawadharau Watumishi kwasababu Wao Wamejitosheleza na km sio kujitosheleza basi tuseme hawajawahi kutana na Shida kubwa iliyohitaji Msaada wa Mtaalamu Fulani wa Sekta fulani Serikalini.
Wacha nisiwachoshe. Ombi langu kwenu ni Moja, naomba TUHESHIMIANE, Kila Mmoja anao umuhimu, Km ambavyo MUNGU alituumba na kutuweka Dunia kila Mmoja kwasababu fulani na MUNGU alijua kuwa kila mmoja ana umuhimu wake Vivyo hivyo hata ktk Maisha, Kila mtu anao umuhimu wake, Mtumishi wa Kada yoyote ile ana umuhimu wake ndio maana Kada hiyo iliwekwa ili watu waisomee na waitumikie, halikadhalika Mwananchi wa kawaida naye anao umuhimu wake, Mmoja akikosekana, lazima Mkwamo wa mambo Fulani utokee tu.
Asanteni.