Mnaoshangaa majina ya Wakinga, mnayajua ya Wasambaa wa Tanga?

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,971
10,465
Kuna thread humu jukwani nimeona inaongelea majina ya ajabu ajabu ya Wakinga wa Makete mkoani Njombe, akina Bonet Sanga, Diff Nyaluke nk. Lakini naona majina ya Wasambaa wa Lushoto na Korogwe ni kiboko zaidi, achimia yale ya akina "SHE". Wao wana majina ya bidhaa/vifaa mbalimbali. Kama haya


Haruna Bendera
Hemed Sabuni
Juma Mswaki
Abdallah Siafu
Ally Msikiti (wanatamka Msigiti)
Mariamu Mshahara
Isihaka Mfuko
Imran Kibao
Maulid Msumari (wanatamka msumai)
Mashabani Msumeno
Jamal Karata
Jamila Makamba
Awadhi Barua
Jumaa Matagi (mayai)


...na kadhalika. Anaebisha awe na sababu za msingi. Wagosi hoyeeeeeee!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom