mwandandila999
Member
- Jul 29, 2015
- 22
- 16
Mwl J.K.Nyerere mara baada ya Tanganyika kupata Uhuru aliwatangazia Watanganyika wa wakati huo wapatao million nane,Maadui zao wakuu kuwa ni watatu 1~Umaskini 2~Maradhi 3~Ujinga.Mnanikera sana mnao mponda mh; Edward Ngoyai Lowasa kuwa hafai kuwa Rais wa nchi hii kwa hoja dhaifu sana eti Lowasa ni tajiri!!!? Eboooo mnataka maskini ili akatajirikie ikulu? Mnataka maskini ndiye awaongoze wakati yeye mwenyewe ameshindwa kumshinda adui umaskini?Mnataka yeye awaondolee umakini wakati yeye kashindwa kuundoa wakwake!!!?kwanini Adui yetu kama taifa Ndiyo iwe sifa ya mtu kuwa kiongozi wetu? Yaani sifa ya kuwa kiongozi iwe ni umaskini ulio nao?? Shame of you,you think like that. Naamini Taifa tunamhitaji mtu ambaye yeye mwenyewe amefanikiwa kuwafukuza adui wote hao yaani (A)Umaskini (B)maradhi na Ujinga.... Naamini sifa hizo Lowasa anazo maana hawazi atakula ama lava,hawazi leo akiumwa hawazi atapata matibabu,hawazi juu ya ugumu wa kupata Elimu bora, huyu ndiye tuna mhitaji atuletee mbinu zilizo mfanya yeye kuondokana na maadui wote watatu ili nasi kama watanzania tuwafukuze kama sio kuwapunguza.Niite mchungaji Mwandandila mtu niliye kosa mbinu au njia ya kuwafukuza Adui wote watatu.