kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Wapo wapo hawana hatia wapo magerezani kwa sababu mtu fulani ameelekeza iwe hivyo. Wakati tunawaweka magerezani tuliamini tutakuwa huru na hatutakufa kabla yao. Sisi tunaojiona tupo huru tumewekwa karantini na hatuna Uhuru wa kutembea tupendavyo.
Baadhi ya waliowaweka gerezani wametangulia mbele ya haki na wale waliopo magerezani ipo siku watatoka na kuishi uraia wakati karantini imeisha.
Tulitamani watoto wao wakose ada na wasiendelee na masomo, ila sasa hata watoto wenu wapo nyumbani kama walivyo watoto wao.
Mlikataza watu kwenda kuwasalimia magerezani mkawagombanisha na kuwaogofya watu wasitoe msaada wowote kwao. Leo hakuna anayekuja majumbani kwenu, mmebaki kama yatima kwa kuogopo wageni.
Mlituaminisha kwamba wao waliomagerezani siyo wazalendo na hawaitakii mema Tanzania, leo mmetutenga na kila mmoja wenu anatetea nafsi yake ipate kuishi.
Mwenyenzi Mungu anatoa adhabu kwa haki ninyi mnatoa adhabu kwa kuyatumia madaraka mliyopewa vibaya. Msihukumu nanyi amtohukumiwa, mnaowatesa kwa kuwaweka ndani Wana amani kulipo ninyi mlio huru mtaani.
Baadhi ya waliowaweka gerezani wametangulia mbele ya haki na wale waliopo magerezani ipo siku watatoka na kuishi uraia wakati karantini imeisha.
Tulitamani watoto wao wakose ada na wasiendelee na masomo, ila sasa hata watoto wenu wapo nyumbani kama walivyo watoto wao.
Mlikataza watu kwenda kuwasalimia magerezani mkawagombanisha na kuwaogofya watu wasitoe msaada wowote kwao. Leo hakuna anayekuja majumbani kwenu, mmebaki kama yatima kwa kuogopo wageni.
Mlituaminisha kwamba wao waliomagerezani siyo wazalendo na hawaitakii mema Tanzania, leo mmetutenga na kila mmoja wenu anatetea nafsi yake ipate kuishi.
Mwenyenzi Mungu anatoa adhabu kwa haki ninyi mnatoa adhabu kwa kuyatumia madaraka mliyopewa vibaya. Msihukumu nanyi amtohukumiwa, mnaowatesa kwa kuwaweka ndani Wana amani kulipo ninyi mlio huru mtaani.