Mlivuta bangi?

Mlivuta bangi?

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
MLIVUTA BANGI ?

1)Mlifanya ukatili,adhabu ni haki yenu.
Mlitenda ubatili,mkazika ndoto zenu.
Ulikuwa ujahili,mwajua taluma yenu ?
Hivi mlivuta bangi ?.

2)Mmeshakuwa mgambo,kuyatembeza mangumi.
Sasa namchapwe fimbo,mkajifiche mikumi.
Harobaini ni fumbo,zenu tena siyo kumi.
Hivi mlivuta bangi ?

3)walimu ni taaluma,vipi mwaidhalilisha.
Ni nani alowatuma,mkapata kujishusha.
Japo kweli inauma,tena mmejiangusha.
Hivi mlivuta bangi ?.

4)ualimu na hasira,kama tembo na bahari.
Hivi hamjui dira,ama mlisha kariri.
Kama nyoka mkafura,mkavimba kama ngiri.
Hivi mlivuta bangi ?.

5)mnamkabia chini,kwani jambazi a mwizi.
Na makofi ya usoni, kama mnavunja nazi
Waziri wa wizarani,sasa kawafuta kazi.
Hivi mlivuta bangi ?

6)wambieni na wengine,shuleni wawe makini.
Msije siku nyingine,mkashia mtaani.
Na wananchi wengine,wa sheria mkononi.
Hivi mlivuta bangi ?

Shairi= MLIVUTA BANGI.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha
+25562401016.
iddyallyninga@gmail.com
Facebook page=Idd ninga mashairi.
 
MLIVUTA BANGI ?

1)Mlifanya ukatili,adhabu ni haki yenu.
Mlitenda ubatili,mkazika ndoto zenu.
Ulikuwa ujahili,mwajua taluma yenu ?
Hivi mlivuta bangi ?.

2)Mmeshakuwa mgambo,kuyatembeza mangumi.
Sasa namchapwe fimbo,mkajifiche mikumi.
Harobaini ni fumbo,zenu tena siyo kumi.
Hivi mlivuta bangi ?

3)walimu ni taaluma,vipi mwaidhalilisha.
Ni nani alowatuma,mkapata kujishusha.
Japo kweli inauma,tena mmejiangusha.
Hivi mlivuta bangi ?.

4)ualimu na hasira,kama tembo na bahari.
Hivi hamjui dira,ama mlisha kariri.
Kama nyoka mkafura,mkavimba kama ngiri.
Hivi mlivuta bangi ?.

5)mnamkabia chini,kwani jambazi a mwizi.
Na makofi ya usoni, kama mnavunja nazi
Waziri wa wizarani,sasa kawafuta kazi.
Hivi mlivuta bangi ?

6)wambieni na wengine,shuleni wawe makini.
Msije siku nyingine,mkashia mtaani.
Na wananchi wengine,wa sheria mkononi.
Hivi mlivuta bangi ?

Shairi= MLIVUTA BANGI.
Mtunzi=Idd Ninga wa Tengeru Arusha
+25562401016.
iddyallyninga@gmail.com
Facebook page=Idd ninga mashairi.
Tatizo ni hasira, zilitujaa mioyoni,
Jitoto kam tahira, haliambiliki asilani,
Hajapitia tohara, funzo jema duniani,
Mzazi mkanye mwanao, walimu mwatupa tabu.

Mtoto kanshika koo, ataka kuniumiza,
Hajui nalisha ukoo, hii singeeza kumeza,
Km kuku yeye koo, namchinj nammeza,
Mzazi mkanye mwanao, walimu mwatupa tabu.

Mshairi naulizia, kwa swalilo liso njia,
Bange metununulia, au ndo wataka wakia?
Umekurupuka najua, kwa kuskia kwa media,
Mzazi mkanye mwanao, walimu mwatupa tabu.

Kaa chini ufikiri, alitenda kosa gani?!
Sijitie ufakiri, kujifanya majinuni,
Maisha hatukariri, chunguza kwa undani,
Eti walivuta bange, ni ww ulitupatia?!

Wakurupuka ndotoni, kalamu wakimbilia,
Kwa kuona videoni, hukumu wajitolea,
Lichungue kwa yakini, ukweli utaujua,
Eti walivuta bange, ni ww liwapatia?!

Nimechok kukujibu, malenga najilalia,
Njoo huku nikutibu, uvivu wa kufikiria,
Kwan mie ndo tabibu, wa kunga kuzitumia,
Eti walivuta bange, ni wewe mewapatia?!

Jina langu ni Bakari, Mhina wangu ukoo,
Utanikuta Sanawari, ukinikosa matejoo,
Huwaga sitaki shari, kwa ushairi njoo,
Eti walivuta bange, ni wewe uliwapatia??
0752 815 647
 
Toba...😱😱😱

kaeni mfanye yenu,ya ngoswe mwachieni
bado tuna safari ndefu,ya milima na mabonde
waalimu fundisheni yenu,muilinde taaluma yenu
kusoma sio ununda, mwanafunzi acha ujinga

mzazi mtambue,mtoto umjue
hekima isikose kwakwe, mfundishe ili ajue
nawaambia na mfikiri,uzito wa shairi

kujielewa kitu muhimu,ndimu haifanani na simu!
punda arushae mateke,huipata fimbo ya bwanae
weka nami niweke,maamuzi yasiyo abadani

fanya maamuzi ya kweli,achana na utepe
weka yako thamani,maisha usitetereke
mwendawazimu haishi wazimu,mpaka ajitambue!

OVER
 
Back
Top Bottom