sepema
JF-Expert Member
- Jun 13, 2019
- 591
- 1,000
Salaam kwenu japo sitamani wahusika watukio hili waitikie Salam yangu.
Uuzaji wa nafaka ni moja Kati ya harakati ninazozifanya ili kuutafuta mkate wangu wakila siku.
Huwa nasafirisha mahindi kutoka hapa mkoani kwangu kwenda mikoa mbalimbali ikiwemo mkoa wa Singida.
Wiki iliyopita nikawa sipo vizuri kiafya hivyo nikamuomba mdogo wangu anisaidie kupeleka mzigo Singida.Yalikua magunia 70 yamahindi ambapo Kuna mteja nilipatana nae kumpelekea.
Dogo anadai alifika na mzigo salama, akapakua na gari iliyoyabeba ikajiondokea zake akabaki yeye na mzigo.
Kwa kuwa muda Ulikua umeenda akaona aende kulala gesti jirani na alipopakulia mzigo. Katika Hali ya kushangaza hakukabidhi mzigo kwa mtu yeyote na aliamini asubuhi atakuta mzigo wake Kama alivyouweka.
Asubuhi anaenda kucheki mzigo anakuta patupu, hakuna hata alama kuonyesha kulikua na magunia70 ya mahindi eneo hilo.
Hapa nimechanganyikiwa kwani nahisi Kama sio uzembe basi Kuna kamchezo dogo kanichezea.
Amenipigia simu kunieleza hayo huku akionekana na yeye kachanganyikiwa kwani anauliza "broo nirudi huko nyumban utanisamehe au nitafute tu pakwenda?"
Nimemwambia aendelee kuulizia labda atapata fununu yahayo mahindi yalipo.Wakati anaendelea kuyatafuta naomba mnisaidie;Huyu dogo atafute pakwenda Kama alivyoomba au nimwambie arudi nyumbani nilipo.
Kama nihasara nimeipata yakutosha wakuu.
Wasalaam!
Uuzaji wa nafaka ni moja Kati ya harakati ninazozifanya ili kuutafuta mkate wangu wakila siku.
Huwa nasafirisha mahindi kutoka hapa mkoani kwangu kwenda mikoa mbalimbali ikiwemo mkoa wa Singida.
Wiki iliyopita nikawa sipo vizuri kiafya hivyo nikamuomba mdogo wangu anisaidie kupeleka mzigo Singida.Yalikua magunia 70 yamahindi ambapo Kuna mteja nilipatana nae kumpelekea.
Dogo anadai alifika na mzigo salama, akapakua na gari iliyoyabeba ikajiondokea zake akabaki yeye na mzigo.
Kwa kuwa muda Ulikua umeenda akaona aende kulala gesti jirani na alipopakulia mzigo. Katika Hali ya kushangaza hakukabidhi mzigo kwa mtu yeyote na aliamini asubuhi atakuta mzigo wake Kama alivyouweka.
Asubuhi anaenda kucheki mzigo anakuta patupu, hakuna hata alama kuonyesha kulikua na magunia70 ya mahindi eneo hilo.
Hapa nimechanganyikiwa kwani nahisi Kama sio uzembe basi Kuna kamchezo dogo kanichezea.
Amenipigia simu kunieleza hayo huku akionekana na yeye kachanganyikiwa kwani anauliza "broo nirudi huko nyumban utanisamehe au nitafute tu pakwenda?"
Nimemwambia aendelee kuulizia labda atapata fununu yahayo mahindi yalipo.Wakati anaendelea kuyatafuta naomba mnisaidie;Huyu dogo atafute pakwenda Kama alivyoomba au nimwambie arudi nyumbani nilipo.
Kama nihasara nimeipata yakutosha wakuu.
Wasalaam!