Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Leo mida ya jioni nilitoka na mama Ngina kupata mchesho wa kuku mahali fulani. Mara kaingia mlevi mmoja akasogelea meza yetu na kuniuliza.
Samahani mzee, naomba uniwe radhi kwa kuuliza
Mimi nikamwambia uliza tu
Huku akiungalia mkono wangu uliofungwa POP, eti huo mkono ni ajali au vibaka?
Nikamjibu ni ajali ..
Akakunja mkono wa shati lake na kuonesha mkono wake wa kulia ambao ulikuwa na majeraha mengi.
Kisha akasema .. mkubwa hii ni ajali, niliuguza huu mkono kwa miezi sita, yaani ninavyokuangalia hapo
nakusikitikia . Pole sana mkubwa
Nikamjibu ahsante . Akaendelea huku akiwa amemgekia mama Ngina . samahani shemeji , ukitaka mumeo apone basi kaa naye mbali, maana nyie hamuishi uchokozi, mwenzio mgonjwa, lakini wewe ndio kwanza utamchokonoa mpaka atake, ..na kama akijaribu kufanya tu hatapona huyu na huo mkono utakatwa
Watu waliokuwa karibu acha wavunjike mbavu kwa kicheko ..
Mie na mama ngina tukabaki kutazamana ..
Hakuishia hapo, aliendelea kubwabwaja kilevi, yaani ilikuwa ni burudani.
Samahani mzee, naomba uniwe radhi kwa kuuliza
Mimi nikamwambia uliza tu
Huku akiungalia mkono wangu uliofungwa POP, eti huo mkono ni ajali au vibaka?
Nikamjibu ni ajali ..
Akakunja mkono wa shati lake na kuonesha mkono wake wa kulia ambao ulikuwa na majeraha mengi.
Kisha akasema .. mkubwa hii ni ajali, niliuguza huu mkono kwa miezi sita, yaani ninavyokuangalia hapo
nakusikitikia . Pole sana mkubwa
Nikamjibu ahsante . Akaendelea huku akiwa amemgekia mama Ngina . samahani shemeji , ukitaka mumeo apone basi kaa naye mbali, maana nyie hamuishi uchokozi, mwenzio mgonjwa, lakini wewe ndio kwanza utamchokonoa mpaka atake, ..na kama akijaribu kufanya tu hatapona huyu na huo mkono utakatwa
Watu waliokuwa karibu acha wavunjike mbavu kwa kicheko ..
Mie na mama ngina tukabaki kutazamana ..
Hakuishia hapo, aliendelea kubwabwaja kilevi, yaani ilikuwa ni burudani.