Tuseme ukweli mkuu wa mkoa wa Dar alilala kwa kazi, hakufanya juhudi zozote za kuhakikisha upatikanaji wa magari ya kuzoa taka, nilitegemea angeomba magari ya polisi siku hiyo yangesaidia kufanyakazi ya kuzoa taka, nilitegemea angeenda kuomba magari ya jeshi nayo yaungane katika zoezi hili, nilitegemea angewaita wamiliki wa mafuso ya mchanga na kokoto nao wangeshiriki zoezi la kubeba taka.
Yapo mafuso yameegeshwa maeneo mbalimbali yakisubiria mizigo ya kwenda mikoani yangeombwa nayo yasaidie kupeleka taka dampo, yapo maroli ya jkt na magereza, sikuona ushirikishwaji wa wafungwa katika zoezi hili la kuzoa taka.
Naamini wadau niliowataja kama wangeshirikishwa sawa sawa basi mji ungekuwa safi zaidi ya hapa tulipo sasa.
hili zoezi liwe endelevu taka bado zipo mkazizoe maana mabulungutu mtayakuta hasa siku itakapotangazwa zinabadilishwaPicha haionekani.
Kwenye nyekundu: Unaonyesha ulivyo na akili finyu ya kimanamba! Jaribu kufikiria tena na kwa kina!Tarehe 09.12.2015 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania JPM aliagiza iadhimishwe kwa kufanya usafi wa mazingira ikiwa ni jitihada za kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu.
Mwitikio wa wananchi ulikuwa mkubwa hali iliyoonyesha kuwa huko nyuma hakukuwa na mwamko miongoni mwa viongozi ktk swala zima la kuhamasisha na kusimamia usafi.
Kinachonishangaza ni kuona takataka zilizojusanywa na kulundikwa sehemu moja hadi leo bado hazijazolewa na Mkuu wa Mkoa bado anacheka na watendaji wake.
Kwa mimi mwananchi wa kawaida tafsiri ninayopata kwa kutokuzolewa kwa taka hizo ni kumkwamisha mhedhimiwa Rais ili aonekane juhudi zake ni nguvu ya soda.
Mkuu wa Mkoa kama kiongozi uliyekabidhiwa rungu tunakutaka ujipime ktk nafasi uliyonayo iwapo unatosha kuendelea kuvaa viatu vya nafasi hiyo huku ukishindwa kuwawajibisha wa chini yako.
Hivi Mkuu wa Mkoa unashindwa nini kuwaandikia Wakurugenzi wa Halmashauri zote tatu kutaka wakupe maelezo kwa nini taka hazizolewi.
Mbona Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni angalau anajitutumua na kuwaweka watendaji wake ndani kwa utovu wa nidhamu.
Kwa hali hii TUWATUMIE JESHI LETU LA ULINZI MAGARI YAO YAFANYE OPERESHENI UZOAJI WA TAKA.HILI PIA LITAKUWA ONYO KWA WANANCHI WANAOTUPA UCHAFU OVYO OVYO WAKIWAHOFIA WANAJESHI WETU IWE KWA MUDA HUU TU KWANI HALMASHAURI WAMEZIDIWA NA HAO WAKANDARASI UCHWALA WA UZOAJI WA TAKATAKA WALIOLAMBA TENDA TUTAFAKARI TUSILAUMU TU TUTOE PLAN B
ndo maana wananchi wamewapa ukawa nao wajaribu angalau watakuja na mbinu nyingine japo tayari kuna malalamiko watendaji wa ukawa wanaomba pesa watu wanaokwenda kupata huduma pasipo kutoa risiti.
Hili zoezi lilikuwa na malengo mazuri na wote tulipenda lifanikiwe na liwe endelevu lakini inaonekana liliendeshwa pasipo mikakati na malengo maalumu.Labda kama kulikuwa na malengo ya PR ya kisiasa.Kwa nini wasingetenga mafungu kiasi toka pesa zilizo okolewa kutoka gharama za sherehe za uhuru kwa ajili ya kukodi agari ya kuzoa hizo taka?Kwa jinsi mambo yanavyoenda napata mashaka makubwa muda ukifika mipango ya kutoa elimu bure itakuwa na kasheshe la aina yake,only time will tell.