MLIMAU
Member
- Feb 2, 2017
- 17
- 2
Mimi ni mkazi wa Kjiji cha Makuyuni wilaya ya Monduli naomba kumweleza Mkurugenzi wa Wilay ya Monduli kuwa Mtendaji wa Kijiji cha Makuyuni Mzee Mwenda anatuvuruga na amekuwa chanzzo cha vurugu eneo la Makuyuni kwa sababu amesahau wajibu wake.
Mzee Mwenda amefanya mambo ya kusikitisha baada ya kusimamisha wajumbe wa serikali ya Kijiji walipwe fidia na TANESCO kwenye eneo la Kanisa Katoliki na eneo la chuo cha VETA ambacho ni mali ya Halmashauri ya Monduli.
Fidia hii ni ile inayotolewa na TANESCO kupitia kupitisha msongo mkubwa wa umeme yalipo mashamba ya taasisi za dini, serikali na mashamba ya watu binafsi.
Bila aibu Mwenda badala ya kuwataarifu wahusika kuja kusimama wakati wa tathmini aliamua kufanya wizi wa mchana kwa kuwasimamisha marafiki zake ili wakishalipwa fidia wagawane.
Cha kusikitisha hata lililokuwa eneo la Halmashauri ya Monduli kilipo chuo cha VETA Makuyuni amesimamisha mtu binafsi ili achukue fidia ambayo kuhalali ni ya Halmashauri. Hapa ameamua kupanga na kuiibia Halmashauri wazi wazi ambayo kimsingi ndiyo iliyomwajiri.
Ni ushahidi gani tena Mkurugenzi wa Halmashauri ya monduli anautafuta ili kumwajibisha huyu Mtendaji mwovu wa Kijiji . Lichofanya Mwenda ni hujuma dhidi ya mwajiri wake na sioni kama ana sifa ya kuendelea kuwepo Makuyuni.
Sijui kwa nini Mkurugenzi anasita kumchukulia hatua kali wakati malalamiko yanayomlenga ni mengi haswa kuhusu udanganyifu wa fidia alioufanya pale Makuyuni akishirikiana na serikali ya Kijiji haswa Mwenyekiti mzee Sulle.
Mtendaji amekuwa hafuati tena taratibu za serikali na sheria za nchi na badala yake anaongozwa na Mwenyekiti mzee Sulle.
Mwenyekiti wa kijiji cha makuyuni amemfanya Mwenda kuwa kama msukule wake kwani hawezi tena kufanya maamuzi kama yanapingana na mawazo ya mwenyekiti wa kijij. Kuna ombwe la uongozi Makuyuni na ndiyo maana vutrugu zinazoepukika za ardhi zimekuwa nyingi.
Namshauri Mkurugenzi amchukulie hatua la sivyo hizo hela za Halmashauri zikiondoka DED utakuwa ktk wakati mgumu. Tunakuangalia kwa karibu tuone busara na hekima zako zikifanya kazi baba.
Mzee Mwenda amefanya mambo ya kusikitisha baada ya kusimamisha wajumbe wa serikali ya Kijiji walipwe fidia na TANESCO kwenye eneo la Kanisa Katoliki na eneo la chuo cha VETA ambacho ni mali ya Halmashauri ya Monduli.
Fidia hii ni ile inayotolewa na TANESCO kupitia kupitisha msongo mkubwa wa umeme yalipo mashamba ya taasisi za dini, serikali na mashamba ya watu binafsi.
Bila aibu Mwenda badala ya kuwataarifu wahusika kuja kusimama wakati wa tathmini aliamua kufanya wizi wa mchana kwa kuwasimamisha marafiki zake ili wakishalipwa fidia wagawane.
Cha kusikitisha hata lililokuwa eneo la Halmashauri ya Monduli kilipo chuo cha VETA Makuyuni amesimamisha mtu binafsi ili achukue fidia ambayo kuhalali ni ya Halmashauri. Hapa ameamua kupanga na kuiibia Halmashauri wazi wazi ambayo kimsingi ndiyo iliyomwajiri.
Ni ushahidi gani tena Mkurugenzi wa Halmashauri ya monduli anautafuta ili kumwajibisha huyu Mtendaji mwovu wa Kijiji . Lichofanya Mwenda ni hujuma dhidi ya mwajiri wake na sioni kama ana sifa ya kuendelea kuwepo Makuyuni.
Sijui kwa nini Mkurugenzi anasita kumchukulia hatua kali wakati malalamiko yanayomlenga ni mengi haswa kuhusu udanganyifu wa fidia alioufanya pale Makuyuni akishirikiana na serikali ya Kijiji haswa Mwenyekiti mzee Sulle.
Mtendaji amekuwa hafuati tena taratibu za serikali na sheria za nchi na badala yake anaongozwa na Mwenyekiti mzee Sulle.
Mwenyekiti wa kijiji cha makuyuni amemfanya Mwenda kuwa kama msukule wake kwani hawezi tena kufanya maamuzi kama yanapingana na mawazo ya mwenyekiti wa kijij. Kuna ombwe la uongozi Makuyuni na ndiyo maana vutrugu zinazoepukika za ardhi zimekuwa nyingi.
Namshauri Mkurugenzi amchukulie hatua la sivyo hizo hela za Halmashauri zikiondoka DED utakuwa ktk wakati mgumu. Tunakuangalia kwa karibu tuone busara na hekima zako zikifanya kazi baba.