Mke wangu anakemea mapepo ile mbaya

Mke wangu anakemea mapepo ile mbaya

Bado kidogo na wewe utaijua kweli ni suala la mda tu.
 
Salamu wandugu, juzi hapa niliwaletea malalamiko yangu wana mmu namna gani nnavyoteseka nyumbani kwangu baada ya kuoa mke asiyejua kupika wali (ubweche) hadi nnajihisi kuloose weight maana ni chakula nnachokipenda kuliko vyote duniani, ila sikuwaeleza tatizo jingine la huyu mwanamke, mwanzoni wote tulikuwa wakatoliki, ila naona mwenzangu sikuhizi kaokoka mwenyewe anasema 'ameijua kweli', kinachonikera zaidi ni tabia yake ya kusali kupita kiasi, yaani daily anaspend at least masaa matatu kanisani mida ya jioni, na akitoka church sio kwamba ndo kamaliza, akirudi nyumbani kabla ya kulala anasali na kukemea mapepo karibu nususaa, akistuka usiku anakemea mapepo, akiamka asubuhi anakemea mapepo, na ole bahati mbaya akatize paka karibu yake, atamkemea hadi majirani watajua. Je hii ni nini, ni dalili ya kutanuka kwa expansion joint yake ama ndio upako?
 
Bora huyo anayekemea pepo kuliko ungempata wa kukunywesha limbwata ya damu ya hedhi!!
Kuna vitu simple siyo lazima ulete Jamvini!!siku akiwa kafurahi mueleze kwa hekima kelele zinakuboa najua ataelewa!!Ngumu mwanzo kuomba maombi ya kukemea bila kelele lakini akizoea atakuwa hashout

Kuhusu kukemea paka ni uchanga kiroho
BTN acheni kuwananga wake zenu mtandaoni be like Man... Kuna hja ya jando kurudishwa Aisee!Mwanaume kifua!!! Hivi ubwabwa hauwez mfundisha Mkeo? Miye kupika kanifundisha baba yang!!!
 
Salamu wandugu, juzi hapa niliwaletea malalamiko yangu wana mmu namna gani nnavyoteseka nyumbani kwangu baada ya kuoa mke asiyejua kupika wali (ubweche) hadi nnajihisi kuloose weight maana ni chakula nnachokipenda kuliko vyote duniani, ila sikuwaeleza tatizo jingine la huyu mwanamke, mwanzoni wote tulikuwa wakatoliki, ila naona mwenzangu sikuhizi kaokoka mwenyewe anasema 'ameijua kweli', kinachonikera zaidi ni tabia yake ya kusali kupita kiasi, yaani daily anaspend at least masaa matatu kanisani mida ya jioni, na akitoka church sio kwamba ndo kamaliza, akirudi nyumbani kabla ya kulala anasali na kukemea mapepo karibu nususaa, akistuka usiku anakemea mapepo, akiamka asubuhi anakemea mapepo, na ole bahati mbaya akatize paka karibu yake, atamkemea hadi majirani watajua. Je hii ni nini, ni dalili ya kutanuka kwa expansion joint yake ama ndio upako?
Anakuombea wewe hapo
 
Kama kelele zinakuzingua mpe chumba chake halafu kiwekee sound proof, akitaka kuomba tu mwambie aende kwenye hicho chumba. Hapo utaondokana na hizo unazoziita kelele. Lakini vipi? Muda wa kwichi kwichi hafukuzi mapepo?
 
Hahaha duuh sina mbavu aisee, hata sina che kukushauri,nimecheka kupita maelezo
 
Back
Top Bottom