Mke wangu anakemea mapepo ile mbaya

Mke wangu anakemea mapepo ile mbaya

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,902
Reaction score
15,932
Salamu wandugu,

Juzi hapa niliwaletea malalamiko yangu wanaMMU namna gani ninavyoteseka nyumbani kwangu baada ya kuoa mke asiyejua kupika wali (ubweche) hadi nnajihisi kuloose weight maana ni chakula nnachokipenda kuliko vyote duniani, ila sikuwaeleza tatizo jingine la huyu mwanamke,

Mwanzoni wote tulikuwa wakatoliki, ila naona mwenzangu siku hizi kaokoka mwenyewe anasema 'ameijua kweli', kinachonikera zaidi ni tabia yake ya kusali kupita kiasi, yaani daily anaspend at least masaa matatu kanisani mida ya jioni, na akitoka church sio kwamba ndo kamaliza, akirudi nyumbani kabla ya kulala anasali na kukemea mapepo karibu nususaa,

Akistuka usiku anakemea mapepo, akiamka asubuhi anakemea mapepo, na ole bahati mbaya akatize paka karibu yake, atamkemea hadi majirani watajua.

Je hii ni nini, ni dalili ya kutanuka kwa expansion joint yake ama ndio upako?
 
Hafanyi vibaya, ila kila kitu kwa kiasi, kama kuna kanisa watu wanakaa masaa matatu huko kila siku na kusahau majukumu yao ya Nyumbani, hiyo si expansion joint, NI UFA NA GOROFA LITADONDOKA!
 
Lol. Ifike mahali muwaletage na wenzenu tuje tupate side B ya story.
 
Keshadata huyo...Mbaya zaidi hela zake na zako zitaishia kanisani na Pasta atakapoanza kula mzigo, kumkataza kwenda Kanisani issue, aache kusali issue, mwambie divorce, labda akili zake zitarudi..
Mmmmmmh! Ushauri gani mkuu?
 
Ni vizuri kuomba lakini kama anazido mdhibiti. Kila kitu ni kiasi, vikizidi ni kero
 
Mara baada ya kununua dala dala, nilianza tabia ya kukemea pepo la ajali! Kilichotokea, dala dala yangu ikapata ajali ndani ya siku tatu! Tangu siku hiyo niliachana na biashara ya kukemea mapepo!
 
Mara baada ya kununua dala dala, nilianza tabia ya kukemea pepo la ajali! Kilichotokea, dala dala yangu ikapata ajali ndani ya siku tatu! Tangu siku hiyo niliachana na biashara ya kukemea mapepo!
🙂🙂🙂🙂🙂🙂Hahahahahahahahah.....Asante kwa kunichekesha mkuu...Hahahahahah...
 
Back
Top Bottom