Mapengo 17
R I P
- Mar 28, 2014
- 1,232
- 609
Habari wanajamvi,
Nimeamini usemi usemao usione watu wanaangua vicheko barabarani na wakati mwingine hadi machozi yanawamwagika kutokana na sababu mbalimbali, Ni kweli kwamba yapo machozi ya furaha lakini pia machozi mengine ni uchungu unaoonekana kama aina fulani ya furaha.
Mtu anaweza kucheka lakini siyo kweli anacheka kutoka moyoni bali anajaribu kuficha yanayomkera lakini katika kujipa moyo anashiriki kicheko pale anapozungumza na jamaa au rafiki yake.Huo ni ukweli.
Ushiriki huu wa kicheko, hakika humpunguzia mawazo fulani kwani vile nijuavyo mimi kicheko ni afya. Hufanya hata makunyanzi kwenye uso kupotea kwa muda.
Lakini pia kipo kicheko cha ukweli kinachotokana na jambo fulani la kufurahisha alilokujulisha mwenzako na katika kuonyesha wingi wa furaha, chozi nalo hujikuta likimwagika. Je, imewahi kukutokea hivyo? Mimi Yes!mara nyingi tu.
Naam, nimeanza hivyo ili kukuweka sawa kwa kile tutakachojadili hapa chini kwamba usione watu wanapita barabarani, wako maofisini wakichapa kazi ukadhani wana furaha tele moyoni.
Pale kazini wanajitahidi au niseme wanajitutumua tu kutimiza wajibu lakini baadhi wanapofikiria kule majumbani wanakotoka, mapigo ya moyo huenda mbio na afadhali kama angeambiwa apige mbio lakini yanamdunda wakati katulia tuli. Kisa amekumbuka vitimbi vya nyumbani kwake.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28, nimejaliwa kufunga ndoa na mke wangu miaka 4 iliyopita, ingawa tumechelewa kupata mtoto lakini ndoa yetu ina upendo na amani ninaishi Dar.
Mwezi wa Machi mwaka huu, mke wangu alifanikiwa kupata ujauzito kitu ambacho kimeongeza upendo ndani ya nyumba yetu na mimi najitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha mke wangu anapata mahitaji yake yote muhimu kiasi kwamba hakuna kitu anachokikosa.
Hata hivyo, kilichonifanya niombe ushauri kutoka kwenu wana JF kwa ujumla, ni kwamba hivi karibuni nimemfuma mke wangu kwenye kabati lake la nguo nimekuta ana kadi mbili za kliniki, moja ina jina langu na ya pili ina jina la bwana mwingine hizo kadi zote kaziandikisha vituo tofauti vya Afya (Majina ya yule bwana mwingine ninayo).
Angalia Mungu alivyo mwema, amenielekeza hadi nikaziona kadi zile kunidhihirishia kuwa mke wangu siyo mwaminifu na lipo au yapo mambo mengi labda bado ananificha.
Kwa kweli baada ya kuzifuma kadi hizo nilichokifanya nilizirudisha nilipozikuta na mpaka hivi sasa mke wangu hajui chochote kinachoendelea.
Ndugu wanajamvi Madam B, Watu8, @KakaKiiza, KakaJambzi, FROWIN, Tutor, ASHUA, na wengineo, mwenzenu yamenikuta nimebaki njia panda kiasi kwamba nashindwa la kufanya. Naombeni ushauri wenu kabla sijachukua uamuzi wowote.
Wasalaam.
Nimeamini usemi usemao usione watu wanaangua vicheko barabarani na wakati mwingine hadi machozi yanawamwagika kutokana na sababu mbalimbali, Ni kweli kwamba yapo machozi ya furaha lakini pia machozi mengine ni uchungu unaoonekana kama aina fulani ya furaha.
Mtu anaweza kucheka lakini siyo kweli anacheka kutoka moyoni bali anajaribu kuficha yanayomkera lakini katika kujipa moyo anashiriki kicheko pale anapozungumza na jamaa au rafiki yake.Huo ni ukweli.
Ushiriki huu wa kicheko, hakika humpunguzia mawazo fulani kwani vile nijuavyo mimi kicheko ni afya. Hufanya hata makunyanzi kwenye uso kupotea kwa muda.
Lakini pia kipo kicheko cha ukweli kinachotokana na jambo fulani la kufurahisha alilokujulisha mwenzako na katika kuonyesha wingi wa furaha, chozi nalo hujikuta likimwagika. Je, imewahi kukutokea hivyo? Mimi Yes!mara nyingi tu.
Naam, nimeanza hivyo ili kukuweka sawa kwa kile tutakachojadili hapa chini kwamba usione watu wanapita barabarani, wako maofisini wakichapa kazi ukadhani wana furaha tele moyoni.
Pale kazini wanajitahidi au niseme wanajitutumua tu kutimiza wajibu lakini baadhi wanapofikiria kule majumbani wanakotoka, mapigo ya moyo huenda mbio na afadhali kama angeambiwa apige mbio lakini yanamdunda wakati katulia tuli. Kisa amekumbuka vitimbi vya nyumbani kwake.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28, nimejaliwa kufunga ndoa na mke wangu miaka 4 iliyopita, ingawa tumechelewa kupata mtoto lakini ndoa yetu ina upendo na amani ninaishi Dar.
Mwezi wa Machi mwaka huu, mke wangu alifanikiwa kupata ujauzito kitu ambacho kimeongeza upendo ndani ya nyumba yetu na mimi najitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha mke wangu anapata mahitaji yake yote muhimu kiasi kwamba hakuna kitu anachokikosa.
Hata hivyo, kilichonifanya niombe ushauri kutoka kwenu wana JF kwa ujumla, ni kwamba hivi karibuni nimemfuma mke wangu kwenye kabati lake la nguo nimekuta ana kadi mbili za kliniki, moja ina jina langu na ya pili ina jina la bwana mwingine hizo kadi zote kaziandikisha vituo tofauti vya Afya (Majina ya yule bwana mwingine ninayo).
Angalia Mungu alivyo mwema, amenielekeza hadi nikaziona kadi zile kunidhihirishia kuwa mke wangu siyo mwaminifu na lipo au yapo mambo mengi labda bado ananificha.
Kwa kweli baada ya kuzifuma kadi hizo nilichokifanya nilizirudisha nilipozikuta na mpaka hivi sasa mke wangu hajui chochote kinachoendelea.
Ndugu wanajamvi Madam B, Watu8, @KakaKiiza, KakaJambzi, FROWIN, Tutor, ASHUA, na wengineo, mwenzenu yamenikuta nimebaki njia panda kiasi kwamba nashindwa la kufanya. Naombeni ushauri wenu kabla sijachukua uamuzi wowote.
Wasalaam.