Wakuu amani iwe kwenu
Mimi ni afisa utumishi kwenye kampuni moja hivi hapa dar
Hivi karibuni bodi ilitengeneza nafasi 12 Mpya za kazi na kuzitangaza
Viongozi waligawana nafasi nafasi tatu kila mmoja na Mimi kuniachia 3
Huwa inakua hivyo kila tunapoajiri, katika hizo nafasi tatu nilizopewa nilipanga moja nimpe wife ambae amemaliza chuo mwaka Jana, nyingine ni Mshikaji wangu ambae aliniandalia pesa, na ya mwisho nimpe Rafiki Wa wife ambae wife mwenyewe aliniomba
Mimi na wife tulioana akiwa na elimu ya form six hakuweza kuendelea kuna matatizo yalijitokeza, hivyo baada ya kumuoa ndipo nikampeleka chuo baada ya kukaa miaka 3 nyumbani
Mwaka Jana ndo amemaliza, so hivi juzi tukamwita kwa mtihani pamoja na wenzie kama 100 hivi tuliowachuja
Matokeo yalipotoka akawa amepata 2 ya 50 mi naita sifuri maana nilimuongezea Mimi hizo mbili wakati nasahihisha
Bosi wangu akasema niamue nwenywe kama namchukua na matokeo hayo siku wakija auditors jumba bovu litaniangukia ni vyema nikasubiri nafasi zingine
Hivyo wale wengine 11 akiwemo na Rafiki yake wakaitwa kwa kazi
Sasa ndani kuna ugomvi kati yangu na mke wangu anasema ningemchykua hivyo hivyo hata kama kafeli
Nimemwelewesha hataki kuelewa kaninunia wiki sasa, hatuongeleshani tunaamka kama mabubu
Usiku saa ya kulala anavaa suruali za tight mbili na jeans juu na mkanda ndo analala tena kwenye kona ya kitanda
Nikimgusa ni ugomvi
Anasema ninatembea na Rafiki yake niliempa kazi, nikimwelewesha kuwa yule alifaulu mtihani anadai tunamsaliti
Nyumba haina amani sasa
Wadau najiuliza maswali kadhaa
(1) inakuaje graduate akapata 2 ya 50 kwa maswali ambayo wote tuliyasoma sekondari?
Mengine ya primary school?
(2)inakuaje mtu anashindwa hesabu za ratio, kuandaa balance sheet, statement of Acc wakati chuo amepita mitihani na Ku graduate au ndo zile degree za chupi?
Nalazimika kuwaza hivyo maana hainiingii akilini
Nikijaribu kumuuliza haya maswali anakua mkali anasema hataki maongezi
Kwa kweli nimechoka juzi nilikua naongea na Rafiki yake kuhusu huu mgogoro kwa kweli alinifariji vizuri hadi nikafikria kuwa ni bora niwepo nae tu ukichukulia kuwa kwa sasa sipati conjugal rights
Naomba mwongozo wenu
NB
Yaan na kujibeba kote kufanya interview kumbe mshagawana kazi..pole yake mim