aliyetegwa
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 320
- 525
Wadau nimekutana na hii sijajua malijali wenzangu mko na maoni gani, kavipi tupia machache hapa.
*MKE MMOJA HATOSHI*
Mke Mmoja Si
Mke,
waume Nawaambia.
Mke Apendae
Peke,
mahaba Hajayajua,
anaogopa
Wenzake,
wasije Kumpindua.
Mke Mmoja hatoshi,
kwa Mume Alotimia..
Ndoa Yataka Makeke,
mke Kujifaragua..
Huba Mshike Mshike,
mizungu Kuipindua..
Sasa Yuko PekeYake,
vipi Atajitambua..
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia..
Akisema kasirike,
kichura tajilalia..
Siku kisemaAchoke,
mto Utakumbatia..
Ikifika Ada Yake,
wiki Yote Utalia..
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia.
Pia akijifungua,
Au kwa maradhi pia.
Mume hapo utajua,
Hekima yake jalia.
Wanne walotimia,
Uadilifu kujua.
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia.
Allah na hekima zake,
Amri hio kutoa.
Idadi ya wanawake,
Mara nne yapitia.
Kila mmoja na wake,
Wengine wapi takua.
Sitara kwa wote wake,
Kuliko kuchepukia.
Haiwi kwa waja wake,
Allah kuwadhulumia.
Ety kuongeza mke,
Ni dosari kweny ndoa.
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia;
*MKE MMOJA HATOSHI*
Mke Mmoja Si
Mke,
waume Nawaambia.
Mke Apendae
Peke,
mahaba Hajayajua,
anaogopa
Wenzake,
wasije Kumpindua.
Mke Mmoja hatoshi,
kwa Mume Alotimia..
Ndoa Yataka Makeke,
mke Kujifaragua..
Huba Mshike Mshike,
mizungu Kuipindua..
Sasa Yuko PekeYake,
vipi Atajitambua..
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia..
Akisema kasirike,
kichura tajilalia..
Siku kisemaAchoke,
mto Utakumbatia..
Ikifika Ada Yake,
wiki Yote Utalia..
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia.
Pia akijifungua,
Au kwa maradhi pia.
Mume hapo utajua,
Hekima yake jalia.
Wanne walotimia,
Uadilifu kujua.
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia.
Allah na hekima zake,
Amri hio kutoa.
Idadi ya wanawake,
Mara nne yapitia.
Kila mmoja na wake,
Wengine wapi takua.
Sitara kwa wote wake,
Kuliko kuchepukia.
Haiwi kwa waja wake,
Allah kuwadhulumia.
Ety kuongeza mke,
Ni dosari kweny ndoa.
Mke Mmoja Hatoshi,
kwa Mume Alotimia;