Siasa zetu zinazidi kutupeleka mbali hadi kwenye familia zetu.Nilipita mitaa flani Kimara mama mmoja akawa anagombana na mumewe na kumuita au kumtukana mumewe msisiem yaani ccm.Kilichonishangaza ni huyo mama kurudia msisiemu kila mara na kumwambia mumewe nimechoshwa na ahadi hewa tangu unioe sioni maendeleo zaidi ya wewe kunenepa na mimi kuwa mwembamba kama fimbo!!mwisho wa kunukuu.Onyo kwa wachangiaji mimi sio mwanachama wa chama chochote ila navutwa na sera