Mkasi Show leo na Mwigulu Nchemba

Mkasi Show leo na Mwigulu Nchemba

Tema Mate

Senior Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
107
Reaction score
193
LEO HII KWENYE MKASI TV SHOW #Repost Mkasitv
・・・
.
Hakuna kipindi ambacho kimekuwa na hamasa ya kisiasa kwa vijana wa Kitanzania kama kipindi hiki cha pili cha Uongozi wa Awamu ya 4. Na moja kati ya viongozi vijana wanaotajwa sana ni Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge wa Iramba, Mh. Mwigulu Mchemba.

Msomi wa Taaluma ya Uchumi, Mchumi aliebobea katika taaluma akiwa bado kinda, na mwanasiasa mahiri, ni moja kati ya sifa chache za Mh Nchemba. Ni hivi majuzi tu alipata kusikika akiongea kwa ukali kuhusu misamaha ya kodi kwa mashirika makubwa lakini pia akiwa na msimamo thabiti dhidi ya makosa ya Kikodi yaliyofanyika sambaba na Sakata la Akaunti ya Escrow ya Tanesco na IPTL (Tegeta Escrow) iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania.

Tulikuwa na maswali mengi....anautaka Urais? Nini mafanikio yake? Majuto? Nani "role model" wake? Kuhusu Familia?

Kwa kadri ya nafasi na uwezo, Mh Nchemba ana majibu ya maswali na hoja zetu! Na kuzisikia, ungana nasi saa 3:30 usiku, EATV pekee upate majibu ya maswali haya na mengineyo!

Shukrani kwa Coca Cola, Tusker Lager na Airtel kwa kutupa nguvu tena leo!

#MwiguluNchemba #MkasiTV

Tukutane saa 3:30 Usiku.
Chanzo:Salama Jabir
 
Last edited by a moderator:
LEO HII KWENYE MKASI TV SHOW #Repost Mkasitv
・・・
.
Hakuna kipindi ambacho kimekuwa na hamasa ya kisiasa kwa vijana wa Kitanzania kama kipindi hiki cha pili cha Uongozi wa Awamu ya 4. Na moja kati ya viongozi vijana wanaotajwa sana ni Naibu Waziri wa Fedha na Mbunge wa Iramba, Mh. Mwigulu Mchemba.

Msomi wa Taaluma ya Uchumi, Mchumi aliebobea katika taaluma akiwa bado kinda, na mwanasiasa mahiri, ni moja kati ya sifa chache za Mh Nchemba. Ni hivi majuzi tu alipata kusikika akiongea kwa ukali kuhusu misamaha ya kodi kwa mashirika makubwa lakini pia akiwa na msimamo thabiti dhidi ya makosa ya Kikodi yaliyofanyika sambaba na Sakata la Akaunti ya Escrow ya Tanesco na IPTL (Tegeta Escrow) iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania.

Tulikuwa na maswali mengi....anautaka Urais? Nini mafanikio yake? Majuto? Nani "role model" wake? Kuhusu Familia?

Kwa kadri ya nafasi na uwezo, Mh Nchemba ana majibu ya maswali na hoja zetu! Na kuzisikia, ungana nasi saa 3:30 usiku, EATV pekee upate majibu ya maswali haya na mengineyo!

Shukrani kwa Coca Cola, Tusker Lager na Airtel kwa kutupa nguvu tena leo!

#MwiguluNchemba #MkasiTV

Tukutane saa 3:30 Usiku.
Chanzo:Salama Jabir

mbona tunasikia ndoa yake iko hatarini kuvunjika? ni kashfa hiyo .

au
tanzania ni tambara bovu kila mtu analikanyagia kanyagia tu?
acha kutania watu
 
Last edited by a moderator:
its one of the most interesting & knowledgeable tv shows that i admire.......Big up sana mamaa salama wewe ni "anadha level".
 
Alishindwa kuzuia uchotwaji wa mabilioni atatufanyia nini wananchi? Akiwa kama naibu waziri anajua kila kitu yeye sada waache unafiki wao
 
Ningemuona wa maana kama angetumia hizo nguvu kupitisha rasimu ya Warioba,kwa kuisigina na kuwa mstari wa mbele kuitetea basi anaunga mkono ufisadi,kwani tunajua yale mazuri ambayokamatiya Warioba iliyaweka ili kuzui ufisadi lakini akina Chenge na genge lao wakaifutikia mbali na tulikuwa tunamuona na kumsikia mh Mwigulu akiwa ndio kwanza akiitetea aache ujinga asiwe kama professor Tibaijuka ambaye baada ya kutupwa ndio anatuletea porojo zake.Ushauri wa bure kwa Mwigulu hivyo vijisenti vyake anavyovipoteza atakuja kuvikumbuka,asitegemee atakuwa kwenye madaraka milele eti kwa ''kuwa ni kijana anayetegemewa na asiyeogopa kitu''uraisi atusikia tu kwenye radio,kwanza itabidi Mangula amuweke kwenye kiti moto kwa kufanya kampeni kabla ya wakati,pia tumuulize Mwigulu hiyo jeuri ya vijisentikaipata kwa kufanya biashara gani?kwani mshahara wa Naibu Waziri hauwezi ukafanya hayo anayoyafanya au ndio kutumia madaraka vibaya,huku anasema yupo kikazi rasmi kumbe anapiga kampeni,naibu waziri wa fedha anachokagua nini?kila siku kijia na mguu.
 
Kuna neno moja alisema nataka kulipata vzr leo huyu jamaa kama hatabadirika yuko vzr nasali nae anaonekana kuwa tumain nililo lejea
 
Aende tu kila media wapo radio,nyu,radio 5,hata aje ya huku songea.lengo ajitangaze eti awe rais
 
Back
Top Bottom