Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,637
SEHEMU YA KWANZA
Vincent yupo katika furaha baada ya kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi aitwaye Vera, wapo kwenye fungate lao, ikiwa ni saa chache tu baada ya kutoka ukumbini. Wote wana furaha sana na Vice ana hamu sana ya kukutana na mkewe kimwili baada ya kuwa waaminifu kwa kipindi chote cha uchumba wao.
Ajabu ni kwamba, Vera hataki kumpa mumewe haki yake ya tendo la ndoa, jambo linalompa hasira Vincent na kutaka kumpiga. Katika hali ya kushangaza, mkono wake ukawa mzito na kurudi wenyewe. Ghafla Vera anapiga magoti chini na kuaomba msamaha.
Macho yake yanatoa machozi, lakini cha kushangaza zaidi, machozi yale siyo ya kawaida. Yalikuwa machozi ya damu, tena damu mbichi! Je, nini kitatokea? Fuatilia...
MACHO yalimtoka Vincent akiwa haamini kilichokuwa mbele yake. Mkewe wa ndoa kulia halikuwa tatizo, labda ilikuwa ni maumivu ya makosa ambayo alifanya kwa mumewe, lakini tatizo ni kule kulia machozi ya damu. Vincent akasimama kwa woga akizidi kutetemeka.
“Nisamehe mume wangu Vincent, nisamehe please, sitarudia tena, nakubali nimefanya makosa mume wangu,” Vera akasema huku akizidi kulia.
Katika hali ya maajabu, damu ikaanza kuchuruzika mashavuni mwake na baadaye kushuka hadi kwenye matiti. Anazidi kulia akisisitiza anaomba kusamehewa kwa kosa alilofanya.
“Vera, una nini?”
“Nisaheme Vice.”
“Ok, lakini mbona unatoa damu?”
“Damu?”
“Ndiyo damu.”
“Wapi?”
“Machoni.”
Vera akashtuka sana, papo hapo akayatupa macho kwenye matiti yake na kuona damu ikichuruzika kutoka machoni mwake. Punde damu ikatoweka, machozi ya kawaida yakaonekana!
“Mbona sikuelewi, iko wapi basi hiyo damu uliyokuwa unasema?” Vera akasema akionekana kushtushwa na kauli ya Vice.
“Ilikuwa hapo muda huu huu, lakini nashangaa imetoweka.”
“Imetoweka kivipi?”
“Sijui.”
“Unataka kusema kwamba nilikuwa nalia machozi ya damu? Na kama ndiyo inawezekana vipi sasa jamani Vice? Mbona unanishtua sana?”
“Sikushtui Vera, ni kweli!”
“Lakini yako wapi sasa?”
“Haya tuachane na hayo, labda ni macho yangu tu, lakini kwanini unanifanyia hivyo mpenzi wangu?”
“Vipi?”
“Unaninyima penzi?”
“Nina maana yangu, tena sababu za msingi sana, na unatakiwa kuelewa kila ninachokuambia, kwa leo haitawezekana, lakini kesho saa nne, nitakufurahisha.”
“Saa nne?”
“Ndiyo!”
“Asubuhi au usiku?”
“Asubuhi darling!”
“Poa, twende basi bafuni.”
“Sawa.”
Wakaongozana hadi bafuni kuoga, huko walifanya kila aina ya michezo ya kimahaba, lakini si tendo la ndoa. Baadaye wakarudi zao chumbani. Wakalala kwa mtindo wa kupendeza sana. Vincent alikuwa amelala kwa mgongo, Vera akiwa amelala kwa ubavu pembeni yake, kichwa chake akiwa amekilaza kifuani mwa Vincent.
Usingizi mnono!
***
Vicheko vile havikuwa vya kawaida kabisa, kwa dakika ishirini nzima, bado alikuwa amesimama akiwa na wasiwasi na mawazo mengi mbele ya umati ule mkubwa wa watu ambao hakuwafahamu! Hakujua kama ilikuwa mchana au usiku, maana ukumbi mzima ulikuwa unang’ara kwa taa kubwa za kupendeza.
Manukato ya kuvutia na harufu nzuri ya vyakula. Vicheko vinaendelea. Akiwa katika hali ile ya kuduwaa, kijana mmoja mnene, mrefu, anamfuata na kumpiga begani. Vincent akageuka katika hali ya kugutuka kidogo!
“Karibu sana kaka, katika ufalme wetu,” kijana yule akasema kwa sauti ya kitetemeshi kidogo, akimuonesha ishara kwamba amfuate.
Katika hali ambayo Vincent hakuitarajia, alijikuta akimfuata. Bila hiyari yake. Safari yao ikaishia chini kidogo ya meza kuu. Akaambiwa aketi, Vincent akatii agizo, akionekana bado ana wasiwasi mwingi sana.
Vicheko vikaendelea.
Punde, akashangaa kumuona mwanamke akiwa analetwa eneo lake akiongozwa na mabinti warembo sana. Juu ya mwanamke huyo aliyekuwa amefungwa kitambaa usoni asionekane, kulikuwa kunawaka moto, ukimfuata kila anapokwenda!
Mara akamfikia na kupewa ishara kwamba asimame. Akasimama. Akapewa ishara kwamba amfungue kile kitambaa usoni, kwa taratibu kabisa, bila hiyari yake akajikuta anafanya hivyo! Haaaaa! Alikuwa ni Vera ambaye aliacha tabasamu mwanana na kumkumbatia.
Akawa kama amenaswa na sumaku!
Hakuwa na hiyari na kitu chochote kile, Vera akaanza kumfanyia kila aina ya michezo anayoijua yeye. Vincent akiwa kimya akishangaa kila kitu. Alipoachiwa, akashangaa kumuona Vera akiwa mtu. Hata wale wasichana waliomsindikiza, wakawa utupu ghafla!
Akiwa bado anashangazwa na hali ile, Vera na wale wapambe wake, wakaanza kubadilika taratibu, macho yao yakawa yanatazama kwa juu, huku meno yao yakianza kutoka kama ngiri. Vincet akataka kupiga kelele.
Lakini hakuweza!
Je, ni wapi hapo na nini kitatokea?
MAPIGO ya moyo wa Vincent yakabadilika kadri nukta moja ilipozidi kwenda, akiwa yupo katika mshangao wa hali ya juu. Kwanini Vera wake amebadilika, kwanini amekuwa mtupu? Kwanini ametoka meno kama ngiri?
Kwanini amebadilika?
Kuna nini?
Ulikuwa mfululizo wa maswali lakini yasiyo na majibu. Aliposhindwa kupiga kelele, akataka kuanza kulia, lakini kwa bahati mbaya sana, machozi nayo yakagoma kutoka. Hakuweza kufanya kitu chochote. Akabaki anashangazwa na jinsi Vera na wenzake walivyobadilika.
Mara ukumbi mzima ukalipuka kwa makofi na vigelegele! Vincent akazidi kushangaa. Akiwa katika mshangao ule, kijana mmoja mtanashati sana, akatokea katikati ya umati wa watu na kusogea eneo walilokuwa wamesimama wale wasichana akiwemo Vera na Vincent. Akawapiga wale wasichana mgongoni, mara wakaonekana wamevaa nguo zao!
Vincent akazidi kupigwa na butwaa kuliko awali.
“Safi sana...” yule kijana akasema kisha akawapiga tena.
Mara wakabadilika, meno na macho yao kurudi katika hali ya kawaida. Vicheko vikasikika tena. Mara akasikia mlio wa king’ora kikali. Watu wote mle ukumbini wakapiga magoti. Mara akasikia muungurumo mkali, upepo na kelele zisizoeleweka. Ghafla likatokea jitu ambalo lilitisha sana hakika.
Lile jitu likapiga kofi mara moja. Wale watu wote wakakaa. Bado Vincent anashangazwa na sehemu aliyopo, matukio yanayotokea yanayosisimua, kushtusha na kuogofya huku akiwa bado hana la kufanya. Kwa mbali zilianza kumuingia hisia kwamba alikuwa kwenye ufalme wa majini!
Wazo hilo lilimwingia, lakini akalikataa. Haikuwa rahisi sana kukubaliana na wazo hilo hasa kutokana na ukweli kwamba hakuwa na kumbukumbu yoyote kama alianza safari ya kwenda huko. Lakini mara moja, akawaza huenda alikuwa katika ndoto ya kutisha!
Ndoto?
Mara zote ndoto huwezi kujua na wala huwezi kuifananisha ndoto na ndoto, sasa iweje kwake? Alikuwa katika wakati mgumu sana wa kujiuliza maswali na kujijibu mwenyewe. Akiwa katika mfululizo ule wa maswali, lile jitu la kutisha, likapiga makofi tena, mara akabadilika na kuwa binadamu wa kawaida, akiwa amevalia suti nyeusi.
Akapiga hatua za taratibu mpaka alipokuwa amesimama Vincent. Akampa mkono, bila hiyari yake, mkono wake ukaenda kwa yule mtu.
“Karibu sana nyumbani, karibu...” akamwambia, Vincent akizidi kutetemeka kwa woga.
“Ahsante sana, ahsante...” bila kutarajia kinywa chake kilifunguka na kutoa maneno hayo.
Hata yeye alishangaa kusikia sauti yake akiwa hana nia ya kuyataamka.
“Tunashukuru sana kwa kututembelea, sijui niseme nini juu ya shukrani zetu, lakini labda niseme ahsante sana. Umekuwa ukitupatia chakula mara nyingi sana, hata tukiwa tumekaukiwa kabisa, wewe umekuwa mkombozi wetu. Ahsante sana Vincent mwanangu...” yule mtu wa maajabu akasema akitabasamu.
Yalikuwa maneno mazito ya kuchanganya kidogo. Hakujua ni chakula kipi hasa ambacho alikitoa kwa yule mtu.
“Kwa bahati mbaya sana, nia yako haiwezi kutimia, lakini tutakupa zawadi nyingine. Tunafahamu kuwa nia yako ilikuwa ni kumuoa binti yetu Vera, lakini hilo halitawezekana!”
“Haitawezekana?” Vincent akang’aka, sasa kwa hiyari yake mwenyewe.
“Ndiyo, hutaweza kumuoa Vera. Hata kama tukikuruhusu, mtashindwana. Ni heri kama unataka kuishi na jamii yetu, tukupatie mwanamke mwingine, tena uishi huku!”
“Huku ni wapi?”
“Utajua baadaye, lakini labda nitangaze kuwa, tangu sasa nimefungua rasmi sherehe hii...Vincent, sherehe hii ni kwa ajili ya kukupongeza...nitakupa ofa ya kulala na Vera kwa siku moja tu na utakuwa hapa kwa siku mbili halafu baada ya hapo utarudishwa kwenu, uendelee na shuguli zako kama kawaida, ambazo zitakuwa na mafanikio makubwa sana,” akasema makofi yakipigwa.
Vincent hakujibu kitu!
Ikatolewa amri kuwa watu wote wafumbe macho, wakafumba. Walipoambiwa wafumbue, Vincent akashangaa akiwa tayari ameshaketi kwenye kiti cha kupendeza, Vera na wapambe wake wakiwa karibu yake. Vyakula vya kila aina mezani. Kwakuwa alikuwa anahisi njaa sana, hakuona sababu ya kujivunga. Akala nao kwa pamoja, huku muziki ambao mpaka sasa hawezi kuuelezea, ukisikika!
Hakuona sababu za kushtuka tena wala kushangaa, maana alishaona kwamba sehemu ile ni ya maajabu tu! Akaamua kuyaacha mambo yaende yenyewe, kama ni ndoto iishe yenyewe na kama ni kweli basi uendelee mpaka mambo yatakavyokuwa vinginevyo.
Katikati ya chakula, akashangaa wahudumu wakipitisha vinywaji, kwa macho ilionekana kama ni maji ya matunda. Akamiminiwa kwenye glasi na kupeleka kinywani moja kwa moja. Akagutushwa na rangi za midomo ya Vera na rafiki zake, ilikuwa myekundu kabisa, alipowachunguza vizuri, akagundua ilikuwa ni damu!
Alipoangalia glasi yake, ilikuwa ni damu!
“Juisi ya damu, hapana siwezi kunywa!” Vincent akasema.
“Acha ujinga, baba akisikia atakuua, kunywa...” Vera akamnong’oneza Vincent ambaye aliamua kunywa japo kwa shingo upande.
Baada ya chakula, yule baba akamfuata na kumpatia kipande cha kitambaa chekundu, akimwambia; “Huu ndiyo utajiri wako, ndiyo zawadi pekee ambayo tunakupatia kwa kazi uliyotufanyia....sasa mnaweza kwenda kupumzika na Vera, kesho asubuhi utarudishwa kwenu. Nata ujue kwamba, uko kwenye ufalme wa giza, sisi ni majini na mimi ndiye mkuu wao, binti yangu alikupenda sana, na mimi nikamwagiza awe na wewe kwa muda, lakini ahakikishe tunapata chakula, muda wenyewe umeshaisha.”
Ukumbi mzima ukalipuka kwa makofi, mbinja na vigelegele. Mara Vera akasimama, katika hali ya maajabu sana, Vincent naye akajikuta amesimama na kumshika Vera mkono, katika maajabu yale yale, akashanga akitembea tena kwa kumwongoza Vera kuelekea lango kuu la kutokea. Makofi yakiendelea.
Vincent akashangaa akihisi kichwa chake kuwa kizito kidogo, mara akahisi kama furaha fulani hivi moyoni. Wakiwa wanatokeza kwenye lango kuu, gari la kifahari likafunguka milango. Vincent ndiye aliyempakiza Vera garini. Safari ikaanza.
Haikuwa safari ndefu sana, kwani dakika kumi tu baadaye waliingia kwenye geti kubwa la kifahari, mlangoni kukiwa na walinzi. Vera akamwongoza mpaka chumbani. Wakavua nguo zote na kuwa watupu! Wakaenda bafuni kuoga, waliporudi wakaanza michezo ya kimahaba. Haukupita muda mrefu sana, walikuwa wameshahamia katika ulimwengu mpya wa kupendeza. Ulimwengu wa mahaba.
***
Kwa dakika tano sana anaendelea kukazia macho darini, ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi, kwani hakuelewa chochote kilichokuwa kikiendelea. Alipotingisha kichwa kwa nguvu, akagundua wazi kwamba alikuwa hotelini, akafungua pazia na kuangalia nje, akaoga jua changa la asubuhi likipendezesha Jiji la Dar es Salaam.
Akayarudisha macho yake kitandani, Vera alikuwa amelala usingizi kabisa. Vincent akashtuka sana. Hapo akahisi kwamba alikuwa kwenye ndoto mbaya ya kutisha. Akamtingisha Vera na kumtaka aamke, akashutuka.
“Vipi Vincent, mbona unanishtua hivyo mpenzi wangu?” Vera akasema akimwangalia Vincent kwa jicho la uchovu.
“Amka...hukumbuki ahadi yetu?” Vincent akasema akipuuza matukio yote aliyoyaona usingizini.
“Ahadi gani?”
“Uliniahidi nini jana?”
“Ok! Angalia saa ukutani, ni saa ngapi saa hizi?”
“Saa 4:45 asubuhi!”
“Na muda mfupi uliopita tulikuwa tunafanya nini? Mbona Vincent una vituko hivyo, hujafanya mapenzi na mimi mume wangu? Kwanza nimekupeleka mpaka kwetu, tumekaa siku mbili nzima na tumeondoka na gari pamoja, tukaenda chumbani...” Vera akasema huku uso wake ukijenga makunyanzi makubwa.
“Vera una nini?” Vincent akasema akiamka na kuvaa haraka.
Akashuka ngazi haraka na kwenda barabarani ambapo alichukua taxi, safari yake ilikuwa moja kwa moja Kanisani. Akaenda ofisini kwa Mchungaji, lengo lake likiwa moja tu, kuvunja ndoa yake na Vera. Alipofika kwenye mlango wa ofisi ya Mchungaji, Vincent akagonga akiwa anatweta kwa hofu.
“Yes, come inn!” Mchungaji akasema.
Vincent akaingia!
Alichokutana nacho ofisini kwa Mchungaji, ilikuwa nusu azimie. Mchungaji alikuwa anaongea na Vera ambaye alikuwa akilia muda wote. Akashangaa sana, Vera alimuacha hotelini.
Amefikaje?
“Noooo Pastor, nooooo.....” Vincent akasema akitoka nje mbio.
Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia simulizi hii ya kusisimua
Vincent yupo katika furaha baada ya kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi aitwaye Vera, wapo kwenye fungate lao, ikiwa ni saa chache tu baada ya kutoka ukumbini. Wote wana furaha sana na Vice ana hamu sana ya kukutana na mkewe kimwili baada ya kuwa waaminifu kwa kipindi chote cha uchumba wao.
Ajabu ni kwamba, Vera hataki kumpa mumewe haki yake ya tendo la ndoa, jambo linalompa hasira Vincent na kutaka kumpiga. Katika hali ya kushangaza, mkono wake ukawa mzito na kurudi wenyewe. Ghafla Vera anapiga magoti chini na kuaomba msamaha.
Macho yake yanatoa machozi, lakini cha kushangaza zaidi, machozi yale siyo ya kawaida. Yalikuwa machozi ya damu, tena damu mbichi! Je, nini kitatokea? Fuatilia...
MACHO yalimtoka Vincent akiwa haamini kilichokuwa mbele yake. Mkewe wa ndoa kulia halikuwa tatizo, labda ilikuwa ni maumivu ya makosa ambayo alifanya kwa mumewe, lakini tatizo ni kule kulia machozi ya damu. Vincent akasimama kwa woga akizidi kutetemeka.
“Nisamehe mume wangu Vincent, nisamehe please, sitarudia tena, nakubali nimefanya makosa mume wangu,” Vera akasema huku akizidi kulia.
Katika hali ya maajabu, damu ikaanza kuchuruzika mashavuni mwake na baadaye kushuka hadi kwenye matiti. Anazidi kulia akisisitiza anaomba kusamehewa kwa kosa alilofanya.
“Vera, una nini?”
“Nisaheme Vice.”
“Ok, lakini mbona unatoa damu?”
“Damu?”
“Ndiyo damu.”
“Wapi?”
“Machoni.”
Vera akashtuka sana, papo hapo akayatupa macho kwenye matiti yake na kuona damu ikichuruzika kutoka machoni mwake. Punde damu ikatoweka, machozi ya kawaida yakaonekana!
“Mbona sikuelewi, iko wapi basi hiyo damu uliyokuwa unasema?” Vera akasema akionekana kushtushwa na kauli ya Vice.
“Ilikuwa hapo muda huu huu, lakini nashangaa imetoweka.”
“Imetoweka kivipi?”
“Sijui.”
“Unataka kusema kwamba nilikuwa nalia machozi ya damu? Na kama ndiyo inawezekana vipi sasa jamani Vice? Mbona unanishtua sana?”
“Sikushtui Vera, ni kweli!”
“Lakini yako wapi sasa?”
“Haya tuachane na hayo, labda ni macho yangu tu, lakini kwanini unanifanyia hivyo mpenzi wangu?”
“Vipi?”
“Unaninyima penzi?”
“Nina maana yangu, tena sababu za msingi sana, na unatakiwa kuelewa kila ninachokuambia, kwa leo haitawezekana, lakini kesho saa nne, nitakufurahisha.”
“Saa nne?”
“Ndiyo!”
“Asubuhi au usiku?”
“Asubuhi darling!”
“Poa, twende basi bafuni.”
“Sawa.”
Wakaongozana hadi bafuni kuoga, huko walifanya kila aina ya michezo ya kimahaba, lakini si tendo la ndoa. Baadaye wakarudi zao chumbani. Wakalala kwa mtindo wa kupendeza sana. Vincent alikuwa amelala kwa mgongo, Vera akiwa amelala kwa ubavu pembeni yake, kichwa chake akiwa amekilaza kifuani mwa Vincent.
Usingizi mnono!
***
Vicheko vile havikuwa vya kawaida kabisa, kwa dakika ishirini nzima, bado alikuwa amesimama akiwa na wasiwasi na mawazo mengi mbele ya umati ule mkubwa wa watu ambao hakuwafahamu! Hakujua kama ilikuwa mchana au usiku, maana ukumbi mzima ulikuwa unang’ara kwa taa kubwa za kupendeza.
Manukato ya kuvutia na harufu nzuri ya vyakula. Vicheko vinaendelea. Akiwa katika hali ile ya kuduwaa, kijana mmoja mnene, mrefu, anamfuata na kumpiga begani. Vincent akageuka katika hali ya kugutuka kidogo!
“Karibu sana kaka, katika ufalme wetu,” kijana yule akasema kwa sauti ya kitetemeshi kidogo, akimuonesha ishara kwamba amfuate.
Katika hali ambayo Vincent hakuitarajia, alijikuta akimfuata. Bila hiyari yake. Safari yao ikaishia chini kidogo ya meza kuu. Akaambiwa aketi, Vincent akatii agizo, akionekana bado ana wasiwasi mwingi sana.
Vicheko vikaendelea.
Punde, akashangaa kumuona mwanamke akiwa analetwa eneo lake akiongozwa na mabinti warembo sana. Juu ya mwanamke huyo aliyekuwa amefungwa kitambaa usoni asionekane, kulikuwa kunawaka moto, ukimfuata kila anapokwenda!
Mara akamfikia na kupewa ishara kwamba asimame. Akasimama. Akapewa ishara kwamba amfungue kile kitambaa usoni, kwa taratibu kabisa, bila hiyari yake akajikuta anafanya hivyo! Haaaaa! Alikuwa ni Vera ambaye aliacha tabasamu mwanana na kumkumbatia.
Akawa kama amenaswa na sumaku!
Hakuwa na hiyari na kitu chochote kile, Vera akaanza kumfanyia kila aina ya michezo anayoijua yeye. Vincent akiwa kimya akishangaa kila kitu. Alipoachiwa, akashangaa kumuona Vera akiwa mtu. Hata wale wasichana waliomsindikiza, wakawa utupu ghafla!
Akiwa bado anashangazwa na hali ile, Vera na wale wapambe wake, wakaanza kubadilika taratibu, macho yao yakawa yanatazama kwa juu, huku meno yao yakianza kutoka kama ngiri. Vincet akataka kupiga kelele.
Lakini hakuweza!
Je, ni wapi hapo na nini kitatokea?
MAPIGO ya moyo wa Vincent yakabadilika kadri nukta moja ilipozidi kwenda, akiwa yupo katika mshangao wa hali ya juu. Kwanini Vera wake amebadilika, kwanini amekuwa mtupu? Kwanini ametoka meno kama ngiri?
Kwanini amebadilika?
Kuna nini?
Ulikuwa mfululizo wa maswali lakini yasiyo na majibu. Aliposhindwa kupiga kelele, akataka kuanza kulia, lakini kwa bahati mbaya sana, machozi nayo yakagoma kutoka. Hakuweza kufanya kitu chochote. Akabaki anashangazwa na jinsi Vera na wenzake walivyobadilika.
Mara ukumbi mzima ukalipuka kwa makofi na vigelegele! Vincent akazidi kushangaa. Akiwa katika mshangao ule, kijana mmoja mtanashati sana, akatokea katikati ya umati wa watu na kusogea eneo walilokuwa wamesimama wale wasichana akiwemo Vera na Vincent. Akawapiga wale wasichana mgongoni, mara wakaonekana wamevaa nguo zao!
Vincent akazidi kupigwa na butwaa kuliko awali.
“Safi sana...” yule kijana akasema kisha akawapiga tena.
Mara wakabadilika, meno na macho yao kurudi katika hali ya kawaida. Vicheko vikasikika tena. Mara akasikia mlio wa king’ora kikali. Watu wote mle ukumbini wakapiga magoti. Mara akasikia muungurumo mkali, upepo na kelele zisizoeleweka. Ghafla likatokea jitu ambalo lilitisha sana hakika.
Lile jitu likapiga kofi mara moja. Wale watu wote wakakaa. Bado Vincent anashangazwa na sehemu aliyopo, matukio yanayotokea yanayosisimua, kushtusha na kuogofya huku akiwa bado hana la kufanya. Kwa mbali zilianza kumuingia hisia kwamba alikuwa kwenye ufalme wa majini!
Wazo hilo lilimwingia, lakini akalikataa. Haikuwa rahisi sana kukubaliana na wazo hilo hasa kutokana na ukweli kwamba hakuwa na kumbukumbu yoyote kama alianza safari ya kwenda huko. Lakini mara moja, akawaza huenda alikuwa katika ndoto ya kutisha!
Ndoto?
Mara zote ndoto huwezi kujua na wala huwezi kuifananisha ndoto na ndoto, sasa iweje kwake? Alikuwa katika wakati mgumu sana wa kujiuliza maswali na kujijibu mwenyewe. Akiwa katika mfululizo ule wa maswali, lile jitu la kutisha, likapiga makofi tena, mara akabadilika na kuwa binadamu wa kawaida, akiwa amevalia suti nyeusi.
Akapiga hatua za taratibu mpaka alipokuwa amesimama Vincent. Akampa mkono, bila hiyari yake, mkono wake ukaenda kwa yule mtu.
“Karibu sana nyumbani, karibu...” akamwambia, Vincent akizidi kutetemeka kwa woga.
“Ahsante sana, ahsante...” bila kutarajia kinywa chake kilifunguka na kutoa maneno hayo.
Hata yeye alishangaa kusikia sauti yake akiwa hana nia ya kuyataamka.
“Tunashukuru sana kwa kututembelea, sijui niseme nini juu ya shukrani zetu, lakini labda niseme ahsante sana. Umekuwa ukitupatia chakula mara nyingi sana, hata tukiwa tumekaukiwa kabisa, wewe umekuwa mkombozi wetu. Ahsante sana Vincent mwanangu...” yule mtu wa maajabu akasema akitabasamu.
Yalikuwa maneno mazito ya kuchanganya kidogo. Hakujua ni chakula kipi hasa ambacho alikitoa kwa yule mtu.
“Kwa bahati mbaya sana, nia yako haiwezi kutimia, lakini tutakupa zawadi nyingine. Tunafahamu kuwa nia yako ilikuwa ni kumuoa binti yetu Vera, lakini hilo halitawezekana!”
“Haitawezekana?” Vincent akang’aka, sasa kwa hiyari yake mwenyewe.
“Ndiyo, hutaweza kumuoa Vera. Hata kama tukikuruhusu, mtashindwana. Ni heri kama unataka kuishi na jamii yetu, tukupatie mwanamke mwingine, tena uishi huku!”
“Huku ni wapi?”
“Utajua baadaye, lakini labda nitangaze kuwa, tangu sasa nimefungua rasmi sherehe hii...Vincent, sherehe hii ni kwa ajili ya kukupongeza...nitakupa ofa ya kulala na Vera kwa siku moja tu na utakuwa hapa kwa siku mbili halafu baada ya hapo utarudishwa kwenu, uendelee na shuguli zako kama kawaida, ambazo zitakuwa na mafanikio makubwa sana,” akasema makofi yakipigwa.
Vincent hakujibu kitu!
Ikatolewa amri kuwa watu wote wafumbe macho, wakafumba. Walipoambiwa wafumbue, Vincent akashangaa akiwa tayari ameshaketi kwenye kiti cha kupendeza, Vera na wapambe wake wakiwa karibu yake. Vyakula vya kila aina mezani. Kwakuwa alikuwa anahisi njaa sana, hakuona sababu ya kujivunga. Akala nao kwa pamoja, huku muziki ambao mpaka sasa hawezi kuuelezea, ukisikika!
Hakuona sababu za kushtuka tena wala kushangaa, maana alishaona kwamba sehemu ile ni ya maajabu tu! Akaamua kuyaacha mambo yaende yenyewe, kama ni ndoto iishe yenyewe na kama ni kweli basi uendelee mpaka mambo yatakavyokuwa vinginevyo.
Katikati ya chakula, akashangaa wahudumu wakipitisha vinywaji, kwa macho ilionekana kama ni maji ya matunda. Akamiminiwa kwenye glasi na kupeleka kinywani moja kwa moja. Akagutushwa na rangi za midomo ya Vera na rafiki zake, ilikuwa myekundu kabisa, alipowachunguza vizuri, akagundua ilikuwa ni damu!
Alipoangalia glasi yake, ilikuwa ni damu!
“Juisi ya damu, hapana siwezi kunywa!” Vincent akasema.
“Acha ujinga, baba akisikia atakuua, kunywa...” Vera akamnong’oneza Vincent ambaye aliamua kunywa japo kwa shingo upande.
Baada ya chakula, yule baba akamfuata na kumpatia kipande cha kitambaa chekundu, akimwambia; “Huu ndiyo utajiri wako, ndiyo zawadi pekee ambayo tunakupatia kwa kazi uliyotufanyia....sasa mnaweza kwenda kupumzika na Vera, kesho asubuhi utarudishwa kwenu. Nata ujue kwamba, uko kwenye ufalme wa giza, sisi ni majini na mimi ndiye mkuu wao, binti yangu alikupenda sana, na mimi nikamwagiza awe na wewe kwa muda, lakini ahakikishe tunapata chakula, muda wenyewe umeshaisha.”
Ukumbi mzima ukalipuka kwa makofi, mbinja na vigelegele. Mara Vera akasimama, katika hali ya maajabu sana, Vincent naye akajikuta amesimama na kumshika Vera mkono, katika maajabu yale yale, akashanga akitembea tena kwa kumwongoza Vera kuelekea lango kuu la kutokea. Makofi yakiendelea.
Vincent akashangaa akihisi kichwa chake kuwa kizito kidogo, mara akahisi kama furaha fulani hivi moyoni. Wakiwa wanatokeza kwenye lango kuu, gari la kifahari likafunguka milango. Vincent ndiye aliyempakiza Vera garini. Safari ikaanza.
Haikuwa safari ndefu sana, kwani dakika kumi tu baadaye waliingia kwenye geti kubwa la kifahari, mlangoni kukiwa na walinzi. Vera akamwongoza mpaka chumbani. Wakavua nguo zote na kuwa watupu! Wakaenda bafuni kuoga, waliporudi wakaanza michezo ya kimahaba. Haukupita muda mrefu sana, walikuwa wameshahamia katika ulimwengu mpya wa kupendeza. Ulimwengu wa mahaba.
***
Kwa dakika tano sana anaendelea kukazia macho darini, ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi, kwani hakuelewa chochote kilichokuwa kikiendelea. Alipotingisha kichwa kwa nguvu, akagundua wazi kwamba alikuwa hotelini, akafungua pazia na kuangalia nje, akaoga jua changa la asubuhi likipendezesha Jiji la Dar es Salaam.
Akayarudisha macho yake kitandani, Vera alikuwa amelala usingizi kabisa. Vincent akashtuka sana. Hapo akahisi kwamba alikuwa kwenye ndoto mbaya ya kutisha. Akamtingisha Vera na kumtaka aamke, akashutuka.
“Vipi Vincent, mbona unanishtua hivyo mpenzi wangu?” Vera akasema akimwangalia Vincent kwa jicho la uchovu.
“Amka...hukumbuki ahadi yetu?” Vincent akasema akipuuza matukio yote aliyoyaona usingizini.
“Ahadi gani?”
“Uliniahidi nini jana?”
“Ok! Angalia saa ukutani, ni saa ngapi saa hizi?”
“Saa 4:45 asubuhi!”
“Na muda mfupi uliopita tulikuwa tunafanya nini? Mbona Vincent una vituko hivyo, hujafanya mapenzi na mimi mume wangu? Kwanza nimekupeleka mpaka kwetu, tumekaa siku mbili nzima na tumeondoka na gari pamoja, tukaenda chumbani...” Vera akasema huku uso wake ukijenga makunyanzi makubwa.
“Vera una nini?” Vincent akasema akiamka na kuvaa haraka.
Akashuka ngazi haraka na kwenda barabarani ambapo alichukua taxi, safari yake ilikuwa moja kwa moja Kanisani. Akaenda ofisini kwa Mchungaji, lengo lake likiwa moja tu, kuvunja ndoa yake na Vera. Alipofika kwenye mlango wa ofisi ya Mchungaji, Vincent akagonga akiwa anatweta kwa hofu.
“Yes, come inn!” Mchungaji akasema.
Vincent akaingia!
Alichokutana nacho ofisini kwa Mchungaji, ilikuwa nusu azimie. Mchungaji alikuwa anaongea na Vera ambaye alikuwa akilia muda wote. Akashangaa sana, Vera alimuacha hotelini.
Amefikaje?
“Noooo Pastor, nooooo.....” Vincent akasema akitoka nje mbio.
Je, nini kitatokea? Endelea kufuatilia simulizi hii ya kusisimua