Mkakati wa Kuihujumu CHADEMA kabla ya 2015 na Kuwabambikia Kesi Viongozi Wake Ulishaanza.


usiwakingie kifua hao wahuni kwa kufanya madhambi yao kuwa mema, je wewe na weredi wako upo tayari kumuunga mkono mtu mwenye makashfa rukuki akiwa hata ajapata dola? tubadilike tubadili taif.
 
Wale ambao wanawapiga chini kwenye chaguzi zote tangia baada ya uchaguzi wa 2010 ndio watawaingiza CDM ikulu ,midabwada ya CCM majambazi na wezi wa mali za umma waliokubuhu watu waliopoteza dira waliotuletea wachovu akina KIkwete Balali Pinda hata akina Sospeter MUhongo professor aliyejijengea heshima ya kutuka duniani kaingia kwenye genge la mumiani wa uchumi wa nchi yetu ana shuka hadhi kwa kasi ya upepo,akina Dr Kafumu walioingia kwenye uchaguzi kule Igunga kwa mbwembwe za Mbabe Mkapa leo hii kwa kinywa chake hataki hata kusikia CCM ni chambio gani sauti ipi tena unasema ipo CCM kama sio wote wafu leo hii Nape kakiri chama kingine kitaingia madarakani soon
 
usiwakingie kifua hao wahuni kwa kufanya madhambi yao kuwa mema, je wewe na weredi wako upo tayari kumuunga mkono mtu mwenye makashfa rukuki akiwa hata ajapata dola? tubadilike tubadili taif.
Ungettuamba tuu sasa yule aliyepo Ikulu amezaa watoto wa koo ngapi na rangi ngapi ana watoto wa kila toka kwa wanawake wa makabila mbalimbali aina 50 kuanzia wakihindi ,wasomali,waarabu,wandengereko,wakwere,waruguru,wahaya,wanyakyusa kila kabila achana na mambo binafsi ya watu bwana
 
Chadema kitakufa kifo cha kwaida kabisa wala hakuna mkakati wowote wakuwabambikia kesi Chadema siyo chama cha siasa ni kikundi cha watu fulani kama NGO.
Kumbe jina lako halijakosewa kwani akili yako inafanana sana na jina na avatar unayoitumia.
 
baada ya mbinu ya mauaji kuelekea kushindwa wamekuja na mbinu mpya ya kuifadhili CUF na kuiga mbinu CDM wanazotumia ili kuwachanganya wananchi
 
Usiwe na shaka mkuu, sahivi kila mkutano tunafunga infrared cctv cameras. mbona watatosha tuu. Ata pawe na giza la namna gani camera zitawanasa tuu na huo ndo utakuwa ushahidi wetu ata mtu avae skaf au gwanda tutamnasa tuu
 
Njia ya tatu ni kutumia njia ya udini hasa kuhakikisha kinasababisha mgogoro kati ya CDM na waislam na ya nne ni kusponsor CUF ​na NCCR MAGEUZI
 
ccm tumewachoka sana sema busara za viongozi wa cdm ndiyo inayoleta utulivu lakini isingekuwa hivyo leo tungekuwa tunaongea mengine kabisa.
 

sikiliza kijana naona tofauti ya kiongozi na raia mwingine wa kawaida wenda huijui, na ndio maana tupo hapa kwa ajili ya kutoa elimu ya uraia kwa watu wote wa namna kama yako. Wanachokosea CDM ni kuwekeza sana kwenye kuiponda serikali ila hawafikirii kutenga hata muda au rasilimali fulani kwa ajili ya kuelimisha umma juu ya siasa safi na uongozi bora sanasana wanachama wao.

kiongozi ni mtu anaengoza kwa mifano, yeye ni taswira ya kila jema ambalo binadamu tunapaswa kuwa, kuanzia tabia, maadili,usikivu na kukubali kukosolewa, ukweli na uwazi pia na uwajibikaji, utu na ushiriki wake katika jamii, yote hayo kiongozi anapaswa kuwa nayo. Angalieni hiyo migambo yenu inayovaa magwanda kama wanahizi sifa, labda kidogo Zitto.

Sasa unaposema niachane na maisha binafsi ya watu, ningekuelewa endapo ningekuwa nakuongelea wewe wenda ni malaya, changudoa au changa la jiji hapo ningeacha, ila tunaongelea viongozi ambao we are about to give them the power to rule our nation, halafu unasema mambo binafsi? hemu kajipange upya na hoja nyingine.
 

Unajisuta mwenyewe KIkwete ana mfano gani akisafiri anasafiri na vimwana kibao hata Prema mwandishi wake alikuwa mshikaji wake kwa maana ya mwanamke wake sijui sasa kama wameachana ndio maana tukakambia angalia usiingilie maisha binafsi ya mtu angalia uwezo wake wa kikazi na uadilifu sifa ambazo raisi wako wa sasa hana hata moja
 

Mkuu, hongera labda niseme "sana" kwa wewe kujitahidi kuchangia kwa jinsi hii!
Ila ninapata wasiwasi kidogo unaposema neno "changamoto zilizopo". Kwa mchango kama huo hapo juu, sidhani hata kama unaelewa maana halisi ya neno "changamoto", sembuse kujua mtu wa kuzitatua.

Mimi si shabiki wa hizo biashara ulizozitaja hapo juu, lakini sioni kama zina kasoro yoyote kwa mujibu wa sheria za TZ.

Kwa akili kama hiyo ya kwako ungebahatika kuwa marekani nadhani enzi hizo ungejiua walipokubali kuongozwa na mcheza sinema *kama sikosea akiitwa (Ronald Reagan).

Lakini alifanikiwa kuliongoza taifa hilo kubwa lenye nguvu zote ulimwenguni kwa mafanikio makubwa. Ukitilia maanani enzi hizo kulikuwepo na vita baridi kati ya NATO na WARSAW PACT!

Hao wafamaji wanaotapatapa, na ambao viongozi wao umewaita majina mabaya, kwa bahati mbaya kwako wamekuwa ndio kipenzi cha wa-TZ lukuki. Hususan wenye kipato cha chini, ambao ndio wengi zaidi katika jumuia ya wa-TZ.

Wakati wewe kwa ushabiki unawabeza, viongozi wa juu hawalali wakihaha namna ya kuwadhibiti.
Mfano uliowazi ni angalia polisi walivyotaka kuaminisha umma wa TZ eti kwamba marehemu Mwangosi alitokea upande wa wafuasi wa CDM akaja upande wa polisi, lengo likiwa ionekane ati alikuja na bomu lillilomlipua!
bahati mbaya kwao picha zikathibitisha vingine.

Acha ushabiki, tafakari.
 

Hayo unayoyasema kuhusu mwenyekiti wangu sikubaliani na wewe na hata taifa kwa ujumla litakataa wakiipata taarifa hii, mhe. Rais ana familia na mpaka mtu anaejitambua kama mhe. Rais anaamua kupata watoto ujue he knows how to be a good husband, jambo ambalo upande wa CDM hakuna aliyefanikiwa, kwa taratibu za kawaida ili uongoze taifa basi kiongozi atupatie first lady, jambo ambalo kile kibabu chenu kinasuasua, dr. aka kibabu chenu hana managerial skills ndio maana chama hakina muelekeo unaoeleweka, kila mtu anataka uongozi ndani ya chama, huoni kama kunaudhaifu fulani wa katibu wa chama?
 



Mkuu naona umefanya violation ya misingi, desturi na tamaduni za Afrika sanasana Tanzania. Ningependa nikukumbushe sakata ambalo limeikumba nchi yetu hivi karibuni, naamini kwa akili zako wenda ni timamu au sio timamu ungeliafiki jambo hilo ambalo ntaliongelea hapa chini.

Hivi karibuni Tanzania kama mwanachama wa nchi zilizowai kutawaliwa na jumuiya ya madola ilitakiwa kuwatambua MASHOGA katika taifa letu kwa kuruhusu ndoa za jinsia moja kukubalika kisheria, maana sheria iliyopo inasimama ikisema ndoa ni muunganiko wa watu wenye jinsia mbili tofauti (yani mwanamme na mwanamke).

Sasa nchi za magharibi ukizitumia kutolea mifano katika nchi zetu hizi za Africa, tutaishia kupata mashoga kama viongozi wetu wa taifa maana nchi za magharibi ni jambo linalowezekana na kusababisha kupeleka mijibaba miwili ikulu, ikiwa mmoja ni rais na mkewe ambae ni lijibaba kwa kigezo kuwa ataweza kuliongoza taifa letu vizuri. Swala la uwezo peke yake wa kuongoza halitoshi ndio maana wabunge wa chadema kila siku wanajitetea katika kamati ya haki, maadili na madaraka ya bunge, kwa kuwa awajafunzwa maadili huko walikotoka na kuwa kikwazo kwa bunge kuendesha shughuli zake kwa kanuni na taratibu. Swala la maadili ndilo tatizo la wahuni maana ni kitu ambacho hawawezi kukitekeleza, tunataka viongozi wasafi kuanzio mioyoni mwao, akilini mwao, miili yao mpaka maadili. Kama Chadema hawana hawa viongozi then CCM tunao.
 

Binadamu wote wameumbwa na kitu "kuchoka kwa hisia" mzuri na mrembo wa leo ukimchoka kihisia huwa mbaya kuliko. Na mbaya wa leo hisia zikiuchoka ubaya huo huwa mzuri mno tena mrembo. Muamar Ghadafi alikuwa mzuri miaka ya 70 lakini hisia zilipomchoka akaonekana mbaya tena shetani kabisa. Hali hii iko kwa watanzania wengi na hata wafadhili wengi waionavyo ccm na serikali zake. ni wale wale mfano, ni malechela, samweli sita, kingunge, pius msekwa, wasira. ni hao hao...hadi lini?

CCM kinang'oka kwa uchovu wa hisia vichwani mwa waliowengiu; damu mpya miongoni mwa wapiga kura ( unajua the new pharao does not know and recognise Joseph); ufisadi uliokubuhu, usultani ndani ya ccm na serikali zake (BOT pale kila kigogo amechopeka mtu wake, ukibisha msikilize Prof. Myuhongo akizindua bodi ya TPDC); makundi sugu na udini katika uteuzi wa mgombea 2015 awe mkristo au wiislam; migogoro kati ya serikali ya CCM na walimu-madaktari-wafugaji-wakulima wa pamba-wachimbaji wa madini,wanafunzi vyuoni,mfumuko wa bei....orodha ni ndefu....
 

Ushoga hapa TZ upo sana. miaka ya enzi za Alli Mwinyi, kiongozi fulani mkubwa (we unamjua) aliwahitajwa kwamba eti ni bwabwa la wakuba wakati huo. Pia ukiwa Zanzibar mashoga sehemu nyingine ndio wamekuwa Geographical/physical address, ni kawaida huko kusikia mtu akitoa anwani yake hivi:" Miye nakaa Bububu karibu na kwa mse***ge fulani".

Aidha, Nchi zote zilizosaini mkataba na azimio la UN la haki za raia hawatakwepa kuzingatia eti haki za mashoga. Tunhitaji kiongozi na chama cha wacha mungu ili kulikabiri hili. Ndani ya CCM watu hao hawamo, na wangekuwemo basi watanzania wasingetolewa kafara kwa miungu yao na wagaganga wa bagamoyo, lindi, sumbawanga , nigeria, beiruti nk.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…