Mjue mnyama Anteanter

Mjue mnyama Anteanter

Mpauko

R.I.P
Joined
Jan 19, 2019
Posts
2,323
Reaction score
3,451
Anaitwa ANTEATER
.
NI moja ya mnyama mwenye uwezo mkubwa sana wa kuvuta harufu
.
Kitaalam anaitwa " vermilingua" anaurefu wa 1.5- 2.5 na anauzito wa kg 35 -43, lakini anapua ndefu sana inayofikia 2 feet na ikiwa na misuli mingi sana
.
Anamwili mdogo ila pua na mkia ndio huongeza urefu wake, na mkia wake huwa unanywele nyingi ndefu
.anamacho dhaifu sana ambayo huona kwa mbali sana hivyo mara nyingi hutumia pua
.
Ni moja ya mnyama mwenye uwezo mkubwa sana wa kunusa na kuvuta harufu anaweza kuvuta harufu mara 30 zaidi ya binadamu ( yaani ukiwa na pua ya huyu mnyama daah hulali njaa
)
.
Kitaalam tunamwita "edentate" yaani wanyama wasio na meno walao mchwa na siafu (vibogoyoo)
.lakini anakula sana siafu na mchwa na kwasiku moja anakula mpka wadudu 30,000
.
Sasa anachofanya ni kutupia yaani yuko fasta kama umeme c unajua kwamba siafu wang'ata afu wanamjua kwamba huyu ndio israel so huwa wanategeana ,
.anachofanya anatoa ulimi alafu anawanasa kwa haraka na kuwatupia tumboni chap sana
.
Ni mnyama tofauti sana kwenye mmeng'enyo wa chakula yeye anatumia acid inayoitwa FORMIC ACID (hii acid mdudu akiingia tu sekunde 0 kashakufa ni kali sana)
.ila wanyama wengine wao hutumia hydrochloric acid
.
Ni mnyama anayeishi kivyake sana yaani hamna familia wala undugu hvyo hupelekea kuwa mvivu sanaa na hulala masaa 15 - 18 kwa siku
.lakini muda mwingi hukutana na wenzake japo ni mara chache sana na grup lao huitwa "PARADE"
.(kama kabila flani hivi kusign kila mwisho wa mwaka )
.
Muda wa mating dume humfata jike na kabla ya mating huwa wana-andaana sana maana ni moja ya wanyama wenye kiwango kidogo zaidi cha joto 32'c
.na hurudia mara kadhaa kwa siku
.
Jike anashika mimba kwa siku 190 na huzaa mtoto mmoja na mtoto wake hukaa nae mpaka muda ambao mtoto atapata mimba
.ndio hufukuzwa sasa aende kwa baby wake
.
Wanaishi miaka 15 wakiwa porini na wakifugwa hufika miaka 25 adui yao mkubwa ni jaguar
.
VIDEO
.umeona mama yuko na mtoto wake mgongoni wanatafuta chakula usikute dume huko kalalaa tu anakoroma ila uzuri hamna kubebeana chakula
.
Mama hutakiwa kumbeba mtoto kwa muda wa mwaka mmoja yaani dogo atazaliwa na atabebwa kwa mwaka mmoja bila kutembea
.(ingekuwa binadamu sasa daah)
 
upo vizuri mkuu, umenikumbusha course moja inaitwa mammalogy.
 
Picha zake hzooo
images%20(1).jpeg
images.jpeg
 
Back
Top Bottom