Girland
JF-Expert Member
- Jan 24, 2016
- 2,672
- 4,560
Limekuwepo tatizo la ajira nchini kwa kipindi kirefu,hata hapa jamiiforums kuna idadi ya watu ambao hawajaajiriwa au kujiajiri.ukienda kwenye jukwaa la Biashara na fursa za kiuchumi hapa Jamiiforums utakutana na michanganuo mingi ya jinsi ya kuanzisha miradi mbalimbali ya kimaendeleo lakini changamoto kubwa inakuwa jinsi ya kupata fedha za mtaji yaani (Capital).Ningependa kuwasilisha hoja binafsi hapa jukwaani ili ikiwa na mashiko iweze kuibua mjadala utakaosaidia kupunguza tatizo hili .
Kutokana na taarifa kutoka google mtandao wa jamiiforums una watumiaji zaidi ya laki nne hawa ni registered users,kama kila mtu akitoa shilingi Elfu moja itakuwa ni jumla ya shilingi milioni mianne yaani [400000*1000=400000000].Na fedha hii ikiwa elfu 10 kwa kila mwana jamiiforums itafikia shilingi bilioni nne fedha ambazo zainaweza kutumika kuanzisha miradi mbalimbali .
Nimefikiria wazo hili kwakuwa hapa jamiiforums tumekuwa kama ndugu na hivyo pamoja tunaweza kujadili changamoto mbalimbali zainazotukabili,ikumbukwe kuwa tuna wataalamu wa kutosha wa kila idara ikiwemo uhasibu,ualimu,udaktari,ufundi mbalimbali,sheria,madini,biashara kwa ujumla,uwekezaji, na zangine nyingi na hii itakuwa fursa ya kuutumia utaalam wao kwa manufaa mapana ya taifa na mtandao huu kwa ujumla.Wanansheria wanaweza kutusaidia kuandaa andiko la kuanzishwa kwa kampuni au saccos au kwa namna yoyote itakavyokubalika na katiba itakayotuongoza na chombo hicho kijielekeza kuinua uchumi wa wanachama na kijitegemee kiuendeshaji .
Kwa hali ya kawaida ni ngumu ila kwa nia thabiti tunaweza kwa pamoja kutumia utaalam tulionao na ushirikiano wetu kuhakikisha tunafanikiwa,hivyo basi nawakaribisha kwa michango yenu,kwa jinsi gani tunaweza kupunguza tatizo hili la ajira au kwa namna gani tutashirikiana kulipunguza tatizo hili .
Niko tayari kukosolewa,kupokea mawazo mbadala na fikra mpya juu ya swala hili hivyo karibuni kwa michango ya mawazo .Mods muiweke ifikie wanajamii wote Mshama Jr Maxence Melo Ontuzu the banker The bold Nifah Zitto zitto junior Mtzed Wakiafrika King Bannizzo JamiiForums MODA Watunduru DeepPond An Enterpreneur mmuru ericka mtzmweusi Mo Genius Gebo2 Leyaleah na wanachama wote wa JF .
GIRLAND
Kutokana na taarifa kutoka google mtandao wa jamiiforums una watumiaji zaidi ya laki nne hawa ni registered users,kama kila mtu akitoa shilingi Elfu moja itakuwa ni jumla ya shilingi milioni mianne yaani [400000*1000=400000000].Na fedha hii ikiwa elfu 10 kwa kila mwana jamiiforums itafikia shilingi bilioni nne fedha ambazo zainaweza kutumika kuanzisha miradi mbalimbali .
Nimefikiria wazo hili kwakuwa hapa jamiiforums tumekuwa kama ndugu na hivyo pamoja tunaweza kujadili changamoto mbalimbali zainazotukabili,ikumbukwe kuwa tuna wataalamu wa kutosha wa kila idara ikiwemo uhasibu,ualimu,udaktari,ufundi mbalimbali,sheria,madini,biashara kwa ujumla,uwekezaji, na zangine nyingi na hii itakuwa fursa ya kuutumia utaalam wao kwa manufaa mapana ya taifa na mtandao huu kwa ujumla.Wanansheria wanaweza kutusaidia kuandaa andiko la kuanzishwa kwa kampuni au saccos au kwa namna yoyote itakavyokubalika na katiba itakayotuongoza na chombo hicho kijielekeza kuinua uchumi wa wanachama na kijitegemee kiuendeshaji .
Kwa hali ya kawaida ni ngumu ila kwa nia thabiti tunaweza kwa pamoja kutumia utaalam tulionao na ushirikiano wetu kuhakikisha tunafanikiwa,hivyo basi nawakaribisha kwa michango yenu,kwa jinsi gani tunaweza kupunguza tatizo hili la ajira au kwa namna gani tutashirikiana kulipunguza tatizo hili .
Niko tayari kukosolewa,kupokea mawazo mbadala na fikra mpya juu ya swala hili hivyo karibuni kwa michango ya mawazo .Mods muiweke ifikie wanajamii wote Mshama Jr Maxence Melo Ontuzu the banker The bold Nifah Zitto zitto junior Mtzed Wakiafrika King Bannizzo JamiiForums MODA Watunduru DeepPond An Enterpreneur mmuru ericka mtzmweusi Mo Genius Gebo2 Leyaleah na wanachama wote wa JF .
GIRLAND

