Mjadala: Shule za Kata kulikomboa taifa

Mjadala: Shule za Kata kulikomboa taifa

Mbavu mbili

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2011
Posts
1,457
Reaction score
874
Wakuu

Nimetafakari sana wazo la kuanzishwa shule za Kata na kubaini kuwa lilikuwa zuri, licha ya changamoto za hapa na pale. Ni dhahiri tangu kuanza kwake zimesaidia Watanzania baadhi kutimiza ndoto zao za kielimu.

Ukichunguza shule hizi zimejengwa walau karibu kila kata kuanzia mijini hadi vijijini. Pia kumekuwa na idadi ya wanafunzi wengi wanaofeli mitihani ya kidato cha NNE ukilinganisha na idadi ya ufaulu wao.

Wazo langu:

Tubadili baadhi ya shule za Kata ziwe shule za Ufundi. Wanafunzi watakaofeli kidato cha PILI na cha NNE wahamishiwe katika shule hizo Mpya za ufundi. Huko masomo mbalimbali ya ufundi yafundishwe kwa miaka mitatu au miwili.

Ninafikiri hili litasidia sana kupunguza wimbi la ukosefu wa ajira nchini mwetu. Pia litaongeza uwezo wa vijana kujitegemea wao wenyewe pindi wamalizapo masomo yao, na Mwisho itapunguza athari mbaya za makundi ya vijana wanaomaliza kidato cha NNE na kupata alama zisizokuwa na msaada wowote katika maisha husika.

Imani yangu ni kuwa si kila mtoto anayefeli masomo darasani basi hana uwezo wa kujifunza masuala mengine katika maisha. Hili litaongeza idadi na chachu ya vijana wasio tegemezi .

Ni imani yangu Shule hizi zikitumika vizuri zitalikomboa taiifa katila masuala mbalimbali.

Naomba kuwasilisha.
 
Umenena vyema sana mkuu... shule za ufundi zikiwa nyingi ajira binafsi zinatengenezwa kwa wingi na uchumi wa watu binafsi unakua. Sio kama ilivyo hivi sasa shule za kata imekua kama sehemu za kujifunzia bongofleva
 
Hatuwezi kufanya mambo yote wa wakati mmoja nadhani nia ya serikali ni mjema tu baada ya hapo tuhamie kwenye shule za ufundi sasa.
 
Hivi kumbe ufundi unahitaji watu waliofeli? nilidhani ufundi unahitaji watu wenye uelewa mzuri wa masomo ya sayansi na hesabu, hii dhana ya kuwa kila anayefeli apelekwe kwenye ufundi ndiyo inachangia sekta hii kutokua au kuwa na mafundi vihiyo katika nchi hii. Ufundi ni taaluma inayohitaji watu makini,
 
Ni wazo jema coz si kila anayeshindwa shuleni atashindwa na ufundi
 
Hatuwezi kufanya mambo yote wa wakati mmoja nadhani nia ya serikali ni mjema tu baada ya hapo tuhamie kwenye shule za ufundi sasa.

tupo pamoja, vyuo vya ufundi vinahitajika sana, tumefanya vizuri ktk shule za kata, tatizo la ajira litaisha.
 
Elimu kwanza nadhani itatimiza ndoto zako.
 
Hivi kumbe ufundi unahitaji watu waliofeli? nilidhani ufundi unahitaji watu wenye uelewa mzuri wa masomo ya sayansi na hesabu, hii dhana ya kuwa kila anayefeli apelekwe kwenye ufundi ndiyo inachangia sekta hii kutokua au kuwa na mafundi vihiyo katika nchi hii. Ufundi ni taaluma inayohitaji watu makini,

unacomplecate sana mkuu, kutengeneza furniture kweli kunahitaji watu makin kiasi kwamba mwenye division 4 anakuwa haqualify? tukiwa na vyuo vingi vya ufundi nadhani hatutategemea sana bidhaa za nje, na vijana wengi watajiajiri.
 
Nadhani hili ni wazo bora kabisa. Lakini je lina mashiko?? Unajua unaposema kubadili baadhi ya shule za kata kuwa shule za ufundi stadi ,unatakiwa uweke akili mambo kama;
1. Walimu wa shule husika kuhamishwa kupelekwa shule nyingine,~kuna balaa hapo
2. Kuongeza facilities za ufundi ili kukidhi haja~ shida nyingine kwa serikali yetu
3. Je wanafunzi hao waliofeli wengi tayari wana nyimbo 500 za ubongo fleva na script za bongo movie wako tayari kujifunza useremala~ kuwa kama Yusuph baba ake na Yesu? Au umakenika~ kuchezea oil??
all in all this is the splendid and magnificent proposal.
 
Wazo zuri lakini hizo shule za kata zenyewe zana za kufundishia ni za kutafuta na manati!!maabara hakuna,vitabu ni ishu.
Hivyo vyuo si ndio itakuwa balaa!!basi VETA ife ili vianzishwe vyuo hivi vya ufundi
Mawazo yangu tu haya!!!!
 
Wakuu

Nimetafakari sana wazo la kuanzishwa shule za Kata na kubaini kuwa lilikuwa zuri, licha ya changamoto za hapa na pale. Ni dhahiri tangu kuanza kwake zimesaidia Watanzania baadhi kutimiza ndoto zao za kielimu.

Ukichunguza shule hizi zimejengwa walau karibu kila kata kuanzia mijini hadi vijijini. Pia kumekuwa na idadi ya wanafunzi wengi wanaofeli mitihani ya kidato cha NNE ukilinganisha na idadi ya ufaulu wao.

Wazo langu:

Tubadili baadhi ya shule za Kata ziwe shule za Ufundi. Wanafunzi watakaofeli kidato cha PILI na cha NNE wahamishiwe katika shule hizo Mpya za ufundi. Huko masomo mbalimbali ya ufundi yafundishwe kwa miaka mitatu au miwili.

Ninafikiri hili litasidia sana kupunguza wimbi la ukosefu wa ajira nchini mwetu. Pia litaongeza uwezo wa vijana kujitegemea wao wenyewe pindi wamalizapo masomo yao, na Mwisho itapunguza athari mbaya za makundi ya vijana wanaomaliza kidato cha NNE na kupata alama zisizokuwa na msaada wowote katika maisha husika.

Imani yangu ni kuwa si kila mtoto anayefeli masomo darasani basi hana uwezo wa kujifunza masuala mengine katika maisha. Hili litaongeza idadi na chachu ya vijana wasio tegemezi .

Ni imani yangu Shule hizi zikitumika vizuri zitalikomboa taiifa katila masuala mbalimbali.

Naomba kuwasilisha.
sidhani kama umetafakari kwa kina, unataka kutuambia wanaofeli kidato cha 2 na 4 ndo wanasifa za kua mafundi. Yaani mafundi ni watu waliofeli shule.
 
sidhani kama umetafakari kwa kina, unataka kutuambia wanaofeli kidato cha 2 na 4 ndo wanasifa za kua mafundi. Yaani mafundi ni watu waliofeli shule.


nakushauri soma tena nilichokiandika kisha urudi kuchangia upya!
" si kila anaefeli masomo hana uwezo wa kijifunza masuala mengine"
 
Nadhani hili ni wazo bora kabisa. Lakini je lina mashiko?? Unajua unaposema kubadili baadhi ya shule za kata kuwa shule za ufundi stadi ,unatakiwa uweke akili mambo kama;
1. Walimu wa shule husika kuhamishwa kupelekwa shule nyingine,~kuna balaa hapo
2. Kuongeza facilities za ufundi ili kukidhi haja~ shida nyingine kwa serikali yetu
3. Je wanafunzi hao waliofeli wengi tayari wana nyimbo 500 za ubongo fleva na script za bongo movie wako tayari kujifunza useremala~ kuwa kama Yusuph baba ake na Yesu? Au umakenika~ kuchezea oil??
all in all this is the splendid and magnificent proposal.

haina haja ya kubadili baadhi ya shule za kata, kulikuwa na mpango wa kujenga vyuo vya ufundi kila wilaya, ila speed yake ni ndogo sana, tungeongeza speed ktk hilo ingesaidia pia,
 
hizo shule zikipelekwa walimu wa kutosha na walimu wakapewa makazi na mshahara mzuri, zikajengwa maabara n.k, zitatusaidia sana kuinua elimu nchini. tatizo ni kwamba, tangu lowasa aondoke zimesinyaa, hakuna maabara, nyumba za walimu hamna, walimu hamna na mwalimu anayeenda pale anahisi ametolewa kafara. tukipata mtu wa kuziendeleza zikapata heshima yake watu watazigombania hizo. hata kina mzumbe walianza kama kata tu hadi kuwa special schools. nimefurahi kuwa wamepeleka walimu wenye degree kwenye shule za kata ktk hizi ajira mpya za juzi, degree tena anafundisha undergraduate. pamoja na kwamba waalimu hawatoshi, shule moja unakuta ina waalimu sita...wanatakiwa walimu walau si chini ya kumi.
 
sidhani kama umetafakari kwa kina, unataka kutuambia wanaofeli kidato cha 2 na 4 ndo wanasifa za kua mafundi. Yaani mafundi ni watu waliofeli shule.

hawajafeli shule, wamefeli mtihani, kipaji mtu anazaliwa nacho ila kinahitaji kukuzwa, ucfungwe kimawazo ukaamini ktk kufaulu mitihani.
 
Hivi kumbe ufundi unahitaji watu waliofeli? nilidhani ufundi unahitaji watu wenye uelewa mzuri wa masomo ya sayansi na hesabu, hii dhana ya kuwa kila anayefeli apelekwe kwenye ufundi ndiyo inachangia sekta hii kutokua au kuwa na mafundi vihiyo katika nchi hii. Ufundi ni taaluma inayohitaji watu makini,

Wapo sana kwenye magari,wanaoita fenebiliti badala ya fan belt,huku uzoefu ndo wenyewe wanasema unamata teh
 
unacomplecate sana mkuu, kutengeneza furniture kweli kunahitaji watu makin kiasi kwamba mwenye division 4 anakuwa haqualify? tukiwa na vyuo vingi vya ufundi nadhani hatutategemea sana bidhaa za nje, na vijana wengi watajiajiri.

Mkuu huo si ufundi ni stadi za kazi
 
Back
Top Bottom