Miujiza ya serikali zetu

Miujiza ya serikali zetu

albuluushiy

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2013
Posts
1,404
Reaction score
687
Nikiwa na masuali mengi kichwani na moyoni mwangu nimekuwa nikijiuliza na kuwaza lakini pia nakukumbuka zile enzi za mapambano ya kisiasa zidi ya vyama viwili vikubwa vya kisiasa kule kwetu Zanzibar C.C.M na C.U.F .Licha ya vituko na vichekesho lakini pia maudhi pamoja na kejeli yalinipa taaswira ambayo nitashindwa kuisahau maishani mwangu.

Nilishuhudia baadhi ya jamii ya watu hususani Wapinzani wa Serikali wakipata kile kilichoitwa joto ya jiwe lakini pia kwa wale majirani zetu kutoka kisiwa cha pili wakifungishwa virago na mbwa na mito akiongozwa kuelekea bandarini ili kuelekea kwao walikotoka yaani Pemba huku nyimbo na chereko zikirindima waso haya wana mji wao, kwa kweli hali hii ilinisononesha sana.

Yote haya yaliokuwa yakitokea Zanzibar, serikali ilikuwa kimya na hakuna kiongozi yeyote wa Serikali ambae alikemea hali hiyo ,fikra zangu ni kwamba wale wote waliohusika kutenda yale walifanya kwa bahati mbaya au pengine hamasa za kisiasa tu kibinaadam,hilo lingewezekana.Lakini baada ya kuona majadiliano kwenye mchakato wa katiba mpya na baadhi ya hoja za Wajumbe wa chama cha mapinduzi nimepata majibu ya masuala yangu yote yaliokuwa yakinisumbua.

Ni dhahiri kwamba vitendo vile vya kiharamia walivyokuwa wakifanyiwa baadhi ya Wapinzani na hasa ndugu zetu kutoka Pemba havikuwa kwa bahati mbaya bali ni sera maalum zilizoratibiwa na Chama chetu cha Mapinduzi na Serikali zake mbili kwa malengo maalum.Na ndio maana ukaona ya kwamba baadhi ya ya Viongozi wakuu wa Serikali wamefikia mahali wameshindwa kujizuia badala yake wanatoa kejeli, vitisho.vijembe,matusi pamoja na vitisho hadharani kama vile vijana wao wa Maskani wanavyofanya.

Kwa mimi kama raia napata picha halisi kwamba C.C.M na serekali zake zinaendeshwa kwa Miujiza. Nasema ni miujiza kwa sababu ni hivi karibuni tu tulimsikia Rais wa Nchi akiwakejeli jamii ya Watu wa Wapemba "walima vitunguu" lakini kama hilo halitoshi,tumeshuhudia katika bunge la kutunga sheria maneno ya kejeli na matusi ni yale yale, hii ni kusema huo ndio msimamo wa Serikali kwa jamii ya Wapemba kwamba hawana kheri waende kwao.

Lakushangaza, na la ajabu zaidi ni kuona Viongozi hao hao wanapanda madege na mameli kwenda kwa jamii ya Wapemba wanaowatukana kila uchao na huku wanawachukia kuliko kitu chengine chochote kile, hivi tuseme kulikoni ? Ama kweli huu ni muijiza wa C.C.M.

Kuna haja gani ya nyinyi kuwafuata kwao na ili-hali wao hawana haya wanamji wao na nyinyi muna miji yenu bora ? Hivi tuseme leo wamekuwa wema au munawapenda kiasi gani ?

Huu ni miujiza kweli wa Serikali zetu mbili '.

Wapemba jibu munalo wenyewe.
 
Naomba ufafanuzi kwa mwenye kujua jinsi muundo wa serikali tatu utakavyokuwa ama utakavyo fanya kazi...maana nasikia watu wanaongelea idadi tu, sasa likipita hilo la serikali 3 ndo mtakuja na mabunge matatu au? na wabunge watanganyika nao watapewa mashangingi kama wale wa lamuungano au? na kutakuwa jengo jipya la bunge la Tanganyika au wata-share?hizi serikali 3 ni kwa ajili ya kuongeza ufanisi au kutatua tatizo la muunguno? waheshiwa hawa wakianza kupanua wigo wa kodi hamtakuwa kwa kwanza kulia na mnajua wao siwalipa kodi..it's better to let Zanzibar go than inviting 3 corrupt governments in one of the poorest nations on earth. ...I thought we should be fighting for half government not 2 or 3....tatizo siyo maandiko mazuri, tatizo kutimiza hayo maandiko au sera...Labda kama wasomi (ma Dr and prof) wanapanua nafasi za kazi maana wote wanavikimbia vyuo kupanda majukwaa..
 
Naomba ufafanuzi kwa mwenye kujua jinsi muundo wa serikali tatu utakavyokuwa ama utakavyo fanya kazi...maana nasikia watu wanaongelea idadi tu, sasa likipita hilo la serikali 3 ndo mtakuja na mabunge matatu au? na wabunge watanganyika nao watapewa mashangingi kama wale wa lamuungano au? na kutakuwa jengo jipya la bunge la Tanganyika au wata-share?hizi serikali 3 ni kwa ajili ya kuongeza ufanisi au kutatua tatizo la muunguno? waheshiwa hawa wakianza kupanua wigo wa kodi hamtakuwa kwa kwanza kulia na mnajua wao siwalipa kodi..it's better to let Zanzibar go than inviting 3 corrupt governments in one of the poorest nations on earth. ...I thought we should be fighting for half government not 2 or 3....tatizo siyo maandiko mazuri, tatizo kutimiza hayo maandiko au sera...Labda kama wasomi (ma Dr and prof) wanapanua nafasi za kazi maana wote wanavikimbia vyuo kupanda majukwaa..

ndugu yangu let we tell u,sisi wazanzibari hatuna shida sana na muundo wa muungano sisi shida yetu ni full sovereignity of znz na sisi wazanzibari tulitaka serikali a mkataba mkapuuza mkatuona hatuna akili wakati huu ndio muumgano ambao sehemu yoyote ulimwenguni unadumu angalia eu muungano wake hauyumbi angalia usa,sasa huu muungano nchi zote zinajiwakilisha vizuri nationally&internationally halafu kunakua na idara ndogo inasimamia mambo ya Muungno kwa mkataba maalum na muda maalum na bila maamuzi ya kibabe km sasa
sasa hyo ndio main point yetu wazanzibari
km hujaelewa sema
 
ndugu yangu let we tell u,sisi wazanzibari hatuna shida sana na muundo wa muungano sisi shida yetu ni full sovereignity of znz na sisi wazanzibari tulitaka serikali a mkataba mkapuuza mkatuona hatuna akili wakati huu ndio muumgano ambao sehemu yoyote ulimwenguni unadumu angalia eu muungano wake hauyumbi angalia usa,sasa huu muungano nchi zote zinajiwakilisha vizuri nationally&internationally halafu kunakua na idara ndogo inasimamia mambo ya Muungno kwa mkataba maalum na muda maalum na bila maamuzi ya kibabe km sasa
sasa hyo ndio main point yetu wazanzibari
km hujaelewa sema
Ndugu unaweza nipa mfano wa nchi ambazo zimeungana kwa aina ya mkataba mnaoutaka ili nipate picha kamili? Hapo mlipo hampo mbali sana na full sovereignity...imepungua wizara ya mambo nje tu.. na mnaweza ipata bila serikali 3..mkiungana wa-znz wote na hasa viongozi wenu, mkasema sasa basi, it's sufficient to achieve your gall, mtakuwa mmemuoko JK kuitwa Gorbachev.
I dont see why do we need 3 governments , means kodi zetu zitaenda bunge la Tanganyika, bunge la muunguno, bunge la East Africa, sijui SADC mara AU...na hivi si viwanda kusema tuna invest, unapeleka pesa zinatafunwa na hazirudi, so what?
 
Back
Top Bottom