Misri ni jangwa 96% lakini Inaongoza Afrika kwa kuzalisha ngano, maembe, nyanya, machungwa, zabibu, viazi nk. Waafrika Tunajifunza nini?

Nilidhani utatetea hoja kwa kunipa link yenye mantiki kumbe unanipa porojo jlizoziandika mwenyewe. Kwani china ilivyoacha ujamaa imeacha kila kitu cha kijamaa? Au unadhani kumilikisha ardhi wageni ndio ufumbuzi wa tatizo la umaskini tanzania? Hata kenya wageni wana ardhi na bado wakenya ni maskini na wengine wanakufa njaa. Hata zambia wageni wana ardhi na umaskini upo mwingi sana.

Ingawa sipingi wageni kumiliki ardhi,lakini najua ujamaa si chanzo cha matatizo yote ya tanzania. Nilikupa mifano mingi ya uongozi mbovu na suluhisho lake,lakini kwa mtu kama wewe wa kusifia sifia huwezi ona hilo. Uduni wa fikra ni shida sana.Unadhani kumsifua samia ndio kutaondoa umaskin tanzania? Au mwenzetu hizi rushwa zilizoongezeka huoni ni kama tatizo kwa maendekeo ya nchi? Ina maana hata huoni aibu kuona mkuu wa mkoa au mbunge anayelipwa milioni kama 17 kila mwezi wakati wananchi wake hawana hata maji safi ya kunywa? Hapo utalaumu ujamaa?
70% ya matatizo ya Tanzania ni ujamaa mentality
 
Tunamsifia Kwa sababu Kuna Baadhi ya vitu anajaribu ku defy the Odd japo anapata ukinzani mkubwa sana
Hapana,mnamsifia kwa ajili ya matumbo yenu.

Na cha ajabu mnapinga ujamaa mentality wakati mnachofanya ni hikohiko mnachokipinga,ujamaa mentality ambayo ni kusifu kiongozi. Hii tabia ilianzishwa na nyerere ikaendekezwa na baadae alipokuja mkapa alijaribu kuipunguza. Lakini magufuli akaifufua,akasifiwa sana,na sasa samia kaiiga,naye anasifiwa na anapenda sifa.

Huo ni utamaduni wa wajamaa.Na CCM wamefuata hii tabia.Kiongozi mpya akija,atasifiwa kwa mabadiliko machache anayoyafanya,halafu yale mabaya anayofanya yanafunikwa. Baadae akija kiongozi mwingine atasifiwa kwa machache mazuri anyofanya na mabaya yake yanafunikwa. Imekua ni cycle hiohio toka enzi za nyerere.

Nyerere alipigana sana kuua ukabila na utengano katika jamii. Na hakuruhusu rushwa serikalini.Alifanya jambo sahihi.Akasifiwa sana. Akaleta ujamaa mwaka 67.Watu walitembea kwa miguu toka mikoani kuja Dar kumsifu nyerere na ujamaa wake,hayo yalifanyika sana miaka ya kuanzia 67 na miaka ya sabini mwanzoni wakati ujamaa upo motomoto. Walimwimbia sana nyimbo za sifa. Lakini alivyokuwa akiua uchumi wa nchi,watu wakifulia magome ya miti na pumba,watu wakivaa kaniki na mawingu chini wakiwa na matairi ya magari, ,hawakumkosoa.mambo yakafunikwa.

Mwinyi akaja.Akaondoa ujamaa uliokuwa ukidumaza uchumi na akaruhusu soko huria katika uchumi. Alifanya sahihi.Akasifiwa sana. Lakini mwinyi aliruhusu rushwa nyingi serikalini.Mashirika ya uma na mambo mengi ya serikali yakalemewa na rushwa na madhara yake yakawa makubwa. Hakuna aliyemkosoa. Mambo yakafunikwa.

Akaja mkapa. Huyu alifanya mabadiliko makubwa kiuchumi. Ndie aliyewezesha Tanzania kupiga hatua kubwa za kiuchumi kwa kufanya mageuzi ya kiuchumi na kubinafsisha mashirika ya uma. Uchumi ukakua sana. Aliingia akikuta GDP ya tanzania ikiwa 4 billion dollars, akaondoka na kuifikisha kama 17 billion dollars, yaani aliikuza zaidi ya mara tatu.Hakuna raisi yoyote wa tanzania aliyeweza kuvunja rekodi hii. Alifanya jambo sahihi.Akasifiwa sana.
Lakini alishindwa kupunguza rushwa iliyoletwa na mwinyi.Hata katika ubinafsishaji wa mashirika ya uma,rushwa ilitumika sana. Hakukosolewa katika uongozi wake.mambo yakafunikwa.

Akaja kikwete.Akaendekeza uchumi kwa misingi ileile ya mkapa. Alifanya sahihi.akasifiwa sana.Lakini rushwa ikaongezeka chini ya kikwete. Ilifikia hatua hata tembo mbugani walikuwa wanaisha kwa kuuawa kwa ajili ya pembe.wakubwa wengi walihusika. Kikwete hakukosolewa akiwa rais.alikosea.lakini mambo yakafunikwa.

Akaja magufuli. Alipigana sana na rushwa na ubadhirifu wa mali ya uma. Akahimiza uzalendo.Alifanya sahihi sana kwa hayo. Akasifiwa sana,naye alipenda sana sifa kama nyerere alivyopenda kusifiwa.Lakini wakati mazuri hayo yanatendeka,wapinzani na wakosoaji wake walikuwa na wakati mgumu.baadhi waliuawa,baadh walitekwa,baadhi walipotezwa,baadhi walifungwa.Magufuli alifanya yaleyale ya nyerere.Magufuli alidiriki hata kuufuta upinzani kama nyerere alivyoufuta.Alikosea. Hakukosolewa na chama chake.Mambo yakafunikwa.

Sasa leo hii samia anasifiwa kwa kuwapa uhuru wapinzani. Anafanya vizuri sana kwa hilo.Hata yale mambo ya utekaji hatuyasikii. Hapo kafanya vizuri sana. Lakini huyuhuyu samia hana mabaya? Kamwe hamtamkosoa. Mtasifu hata kama kukiwa na maovu yanatendeka. Huu ndio ujamaa.
Cha ajabu mnafanya mambo ya kijamaa na bado mnakosoa ujamaa. Na mpo kwenye cycle hiohio kwa miaka zaidi ya 60. Hata hamuoni makosa yenu. Hata hamna system ya kudhibiti na kukosoa viongozi wenu. Hamna hata systems nzuri za kuchagua viongozi.Akija mpya mnasifia. Akiharibu mambo hamumsemi,mnanyamaza kulinda hivyo viugali vyenu.
Very stupid beings.
 
Basi jana nikawa naangalia taarifa habari jioni. Ikafika wanaonyesha nanenane na mke wa rais mstaafu kikwete akiwa kwenye nanenane akashauri watu wa BOT warudishe kwenye mzunguko zile sarafu za zamani kwenye mzunguko ili watoto wa leo wazijue. Hapo anaongelea sarafu kama senti 50,20,10 na hata shilingi moja ambazo hazipo kwenye circulations.

Yule afisa wa BOT kwenye lile banda akakubali bila kupinga.Akaahidi kutimiza hilo.
Nilishangaa sana

Ndio hayo mambo ya ajabu ya kutokosoa viongozi. Hizo senti nani atazitumia huku hazina thamani? Hio gharama ya kusambaza nani alipie?

Ningekuwa ni mimi,ningefanya yafuatayo kufanya kizazi cha leo kijue sarafu za zamani za nchi hii na nitafanya hivyo bila kuingiza gharama zisizo na msingi.
Nitajenga majumba ya makumbusho kila mkoa. Ndani nitaweka sarafu zote zilizowahi kutumika tanzania na noti zake. Nitaweka vitu vingine vya kihistoria kwenye hayo makumbusho.Halafu kutakuwa na kiingilio ambacho kitarudisha hizo pesa zilizogharimia mambo yote hayo. Wanafunzi mashuleni,vyuoni na watu wengineo watahamasishwa kutembelea makumbusho.Baadhi ya sarafu za zamani ambazo bado BOT wanazo nyingi kwenye hifadhi zao zitapigwa mnada.
 
Elimu na Umasikini
Wala si umaskini ila vipaumbele nchi imekosaa vipaumbele vya wapi tuwekeze na kuinufaisha nchi wapi tuwekeze na kuinua vipato vya wananchi miaka zaidi ya 30 tungeamua kuvuta maji ya ziwa Victoria yaje hadi morogoro tu tungeshafanya ata kwa vipande ila tuko kama wendda wazimu tusiojielewa Leo hii ccm inapewa kila siku kura mwanza, Geita, shinyanga, Mara, kagera, na simiyu, na kkote uko kuna shida ya maji na mikoa yote hii imezungukwa za ziwa kubwa lenye maji kedekede unaisi kuna mabadiliko yatakujaa kutokea haitakaa itokee Leo hii morogoro kkuna mito kibao ila kuna shida ya maji kuliko Dodoma aisee Mungu atubariki ila kiuhalisia ccm imeshindwa kuunganisha rasilimali za nchi zilizopo na kuwaletea wananchi maendeleo
 
Siku flani basi nikaona wanajisifu kuwa tanzania wanazalisha asali karibia tani 33 kwa mwaka hizo ni kama lita elfu 33. Inaonekana tupo nafasi ya pili kwa uzalishaji wa asali katika bara la afrika tukiongozwa na ethiopia.

Angalao hapo wamejitahidi.
Lakini........

Kwa mapori na hifadhi zilizopo tanzania,hivi hawaoni kama tunazalisha kidogo sana?
Na ujue sababu kuu tunashindwa kuzalisha asali nyingi ni ukosefu wa mizinga ya kisasa.

Sasa jiulize, Tuna kundi la vijana wanajiunga JKT kila mwaka. Wakifika JKT sehemu kubwa ya muda wao unatumika kwenye kilimo kama cha mahindi.
Hapo ndipo wanapokosea. Wanakosea sana.
Mahindi yanaweza limwa,paliliwa,wekwa mbolea na kuvuna kwa mashine kama matrekta.Kwanini uharibu mikono ya vijana kufanya kitu ambacho trekta linaweza fanya tena kwa haraka sana?

JKT watumike kuzalisha asali na mazao mengine ambayo ni ngumu kutumia mashine.Asali ndio wangeweka mkazo zaidi kwasababu ni kitu ambacho ni kigumu kuzalishwa kwa mashine na asali ina soko la uhakika huko nje.Ingetupa pesa nyingi sana za kigeni.
Fikiria haya mapori yote ya uhifadhi yakitumika kwenye ufugaji nyuki.Ujue mzinga mmoja wa kisasa unaweza kukupa kama lita 15 au 20 kwa msimu,manake mwaka ni misimu miwili.

Sasa,unadhani JkT wangevamia mapori yote ya serikali hapa tanzania,na kusimamia vizuri ufugaji nyuki,unadhani kwa mwaka wangevuna asali tani ngapi?
Tani milioni?
Hapana.

Pengine hata milioni 50 au 100 za asali kwa mwaka. Kumbuka theluthi ya tanzania ni mapori. Kumbuka hata kwenye mbuga za wanyama unaweza fuga nyuki kama ukifanya ubunifu kidogo.Hapo angalau utakuwa umetumia ardhi na uhifadhi kwa kiwango cha juu. Ina maana baadhi ýa mbuga zitatumika pia kufugia nyuki hasa zile mbuga zisizo na watalii wengi.Ujue kwa sasa kuna mbuga za wanyama kama 4 au 5 tu zinajiendesha zenyewe. Nyingine zinapewa fedha kujiendesha.

Lakini hata ukiweza kuvuna tani milioni moja ya asali kwa mwaka,hio ni sawa na Shilingi Trilion moja kwa mauzo ya asali kwa bei ya elfu kumi kwa kilo. Na je ukizalisha tani milioni mbili,au tani milioni 5 au vipi kama zikiwa tani milioni 10 kwa maka za asali? Ni pesa ngapi za kigeni zitapatikana?
 
Najaribu kufikiri na kukumbushana kwamba watu Weusi mda wote ni kulalamika, kulaumu na kupinduana ila kichwani kumejaa matope.

Kama Egypt inaweza fanya yote hayo ilhali Ardhi yake Asilimia 96% ni jangwa tena sio kama la Dodoma Bali jangwa hasa na maji yanayotegemewa yanatoka Nile river plus mamilioni ya watu,Kwa nini sie tusiweze?

Badala ya kulaumu tukasomeshe watu Wetu kwenye Nchi zilizofanikiwa wakafanye kazi wapate uzoefu na warudi Nchini mwetu kuleta huo ujuzi Ili tutumie zaidi mazingira ambayo ni rafiki kwetu Kujikwamua kiuchumi.

Mwisho hakuna siku Watu Weusi tutaendelea Kwa kukumbatia mawazo ya Kijamaa na kuona mnaonewa na Wazungu na kukimbilia Russia ,utakuwa ni mwendelezo wa upumbavu tuu.

Umesahau na la kusifiana kwa afrika, kama mtu upo nje ya Tanzania ukawa unasikiliza jinsi Rais wa Tanzania anavyosifiwa mbona unaweza kudhani Tanzania imepiga hatua kimaendeleo kuliko hata hiyo Misri na ipo serious kweli.
 
Ukiangalia asilimia kubwa ya nchi za Africa tuna vitu vingi lakini Maendeleo duni ,ukiangalia nchi za uarabuni resource moja tu wameweza kutumia vizuri wako mbali sana .

Wao Ardhi zao ni majangwa tu asilimia kubwa hata ,lakini kwetu ukijani na ardhi zenye rutuba pamoja na mito ni mingi lakini inatokea uhaba wa maji ,chakula hali duni nk.
Hatupo serious kwenye kuleta maendeleo na bado masuala ya vyeo yana tushughulisha sana.
 
Waafrika tumechelewa sana hata siasa tungeachana nazo tukafanya maendeleo kwanza ,hii nchi kila mtu anajikuta mjuaji basi anakimbilia siasa.
Ndio unaona Kinana anawapigia debe wabunge kwamba mishahara yao ni kidogo waongezwe. Hayo ndio yametutawala siasa mwanzo mwisho ,kulipana mishahara mikubwa,kugombea mavyeo kuliko kufikiria jinsi ya kuondoa changamoto zetu na kujiletea maendeleo kwa kifupi hatupo serious kwenye kuwaza hayo maendeleo.
 
Ndio unaona Kinana anawapigia debe wabunge kwamba mishahara yao ni kidogo waongezwe. Hayo ndio yametutawala siasa mwanzo mwisho ,kulipana mishahara mikubwa,kugombea mavyeo kuliko kufikiria jinsi ya kuondoa changamoto zetu na kujiletea maendeleo kwa kifupi hatupo serious kwenye kuwaza hayo maendeleo.
Mbunge analipwa milioni 12 kwa mwezi,ukiongeza na posho za kuingia bungeni na vikao na safari,mwisho wa mwezi anapewa kama milioni 17. Na idadi ya wabunge ni kubwa sana,kuna hadi wale wa kuteuliwa. Kuna jumla ya wabunge kama 400 kwenye nchi maskini yenye watu milioni 60 na matatizo yanayofanana kila mkoa kila wilaya na kila jimbo la ubunge..

China yenye watu bilioni moja na nusu na maendeleo yote yale wana wabunge kama elfu 3 tuu.

Na hapohapo usisahau kuhesabu wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa ambao wote wameteuliwa.

Hivi najiuliza kuna haja ya mkoa kama Dar kuwa na mbunge wakati raisi na serikali ipo hapohapo na inaona matatizo yote ýa mkoa huo kila siku na kumbuka kuna madiwani pia na mameya wa jiji.
 
Sasa huku Raisi wa nchi anawaambia mawaziri wake wale kwa urefu wa kamba zao Alafu anawauliza wezi eti hamja tosheka tuu alafu ana maliza kwa kusema stupid, unadhani maendeleo kama hayo yatatokea wapi 🤔🤔🤔
Wakati huo huo wanamsifu ana upiga mwingi kwamba ana chapa kazi vizuri.
 
Mbunge analipwa milioni 12 kwa mwezi,ukiongeza na posho za kuingia bungeni na vikao na safari,mwisho wa mwezi anapewa kama milioni 17. Na idadi ya wabunge ni kubwa sana,kuna hadi wale wa kuteuliwa. Kuna jumla ya wabunge kama 400 kwenye nchi maskini yenye watu milioni 60 na matatizo yanayofanana kila mkoa kila wilaya na kila jimbo la ubunge..

China yenye watu bilioni moja na nusu na maendeleo yote yale wana wabunge kama elfu 3 tuu.

Na hapohapo usisahau kuhesabu wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa ambao wote wameteuliwa.

Hivi najiuliza kuna haja ya mkoa kama Dar kuwa na mbunge wakati raisi na serikali ipo hapohapo na inaona matatizo yote ýa mkoa huo kila siku na kumbuka kuna madiwani pia na mameya wa jiji.
Tupo kwenye utawala mkuu tunatawaliwa hivyo kipaumbele lazima yawe manufaa yao watawala hivyo hawawezi kuona kama hilo lundo la wabunge na hao wateuliwa ni mzigo kwa nchi wala hawajali.
 
Tupo kwenye utawala mkuu tunatawaliwa hivyo kipaumbele lazima yawe manufaa yao watawala hivyo hawawezi kuona kama hilo lundo la wabunge na hao wateuliwa ni mzigo kwa nchi wala hawajali.
Sijui unamaanisha nini kutawaliwa.Huko china wanatawaliwa lakini huoni huu upuuzi. Hata kama wanataka kula,kwani huwezi kula bila kuharibu nchi?l
Mbona wanaweza kuwapa maafisa wa serikali motisha kila wanapotimiza majukumu kwa weledi na wakala pesa huku nchi ikisonga mbele.
Mfano ukasema,wewe mkuu wa mkoa huu wa katavi ukisimamia ufugaji wa nyuki na ukaongeza uzalishaji hadi tani flani kwa mwaka utapewa milioni 200 kama motisha.
Au wewe balozi wa tanzania huko brazili,ukituletea wawekezaji wa kiasi hiki na wakawekeza nchini, tutakupa bilioni moja kama motisha.
Mbona wanaweza kula vizuri tu huku wakileta maendeleo?
 
Sema wezetu wanathamini vya kwao na huku tukiponda vya kwetu lakini kwani katika hivyo ulivyo orodhesha kwamba wa Egypt wanaongoza kulima kama maembe ,machungwa, nyanya,vitunguu,vitunguu, viazi ,zabibu and alikes si vinaozea mashambani huku kwetu na wakati flani tuna ignore kuvinunua na kukimbilia imported fruits kama machungwa ma apple kutoka South Africa na vingine vingi kutoka nje tukifikiri ndio ujanja .Watu weusi tunaweza sana tunachatakiwa tuthamini vyetu.
 
Najaribu kufikiri na kukumbushana kwamba watu Weusi mda wote ni kulalamika, kulaumu na kupinduana ila kichwani kumejaa matope.

Kama Egypt inaweza fanya yote hayo ilhali Ardhi yake Asilimia 96% ni jangwa tena sio kama la Dodoma Bali jangwa hasa na maji yanayotegemewa yanatoka Nile river plus mamilioni ya watu,Kwa nini sie tusiweze?

Badala ya kulaumu tukasomeshe watu Wetu kwenye Nchi zilizofanikiwa wakafanye kazi wapate uzoefu na warudi Nchini mwetu kuleta huo ujuzi Ili tutumie zaidi mazingira ambayo ni rafiki kwetu Kujikwamua kiuchumi.

Mwisho hakuna siku Watu Weusi tutaendelea Kwa kukumbatia mawazo ya Kijamaa na kuona mnaonewa na Wazungu na kukimbilia Russia ,utakuwa ni mwendelezo wa upumbavu tuu.
Unaambiwa eneo uwanda wa Mto Kagera uzalishwa wa sukari ukiwa wa kisasa tunaweza kusambaza Africa nzima,lkn angalia siasa tu hapa sukari inatoka maerufu ya kilometa Brasilian uko,hivyo kabisa
 
Hiyo ardhi ni nzuri kuliko inayotegemea mvua, unauhakika maji na wala mvua haipo ili kuharibu, lkn kwetu unaweza kuona jua kali ukaanza kumwagilizia wiki ijayo mvua ikalipuka na kuharibu mazao yote.
 
Kwa uwelewa wangu ni kuwa nchi zote ambazo zimezungukwa na ziwa Victoria ambacho ndio chanzo Cha maji ya mto Nile haziruhusiwi kufanya shughuli yoyote ya umwagiliaji kupitia maji ya ziwa Victoria Kwa makubaliano ya kupewa misaada mbali mbali na nchi ya misri hivo ukichunguza tunafungwa na mkataba na makubaliano Kwa maana misri wanategemea sana sana maji ya ziwa Victoria hivo tukiharibu kwao ni vilio swala la msingi tuna nufaika vipi na hayo makubaliano na je unufaikaji wetu unaendana na wanacho faidi wao

Ushauri
1. Pawe na project ya kuchukua hata wanafunzi 50 au 100 kwenda wakajifunze huko misri na wagaramiwe na misri Kwa makubaliano hata Kwa miaka 5
2. Serikali iandae maeneo totauti ambayo haya ingiliana na mkataba wa ziwa Victoria na misri maana mito ipo mingi na maziwa yapo mengi
3 .Tukubali kupata vifaa vya kisasa vya umwagiliaji Kwa ajili ya mradi huo
4.Wanasiasa wanaomiliki sehemu tengefu zote na wanafanya wao Kwa shughuli za umwagiliaji waporwe Kwa manufaa ya Taifa
5.Tukubali kubadilisha fikra zetu kabla ya kubadilisha Tanzania yetu (ujamaa>ubeberu)

Unawaza kupewa misaada tu, maajabu gani ya umwagiliaji ambayo hapa hatuwezi
 
Back
Top Bottom