Mishipa ya mwili

Mishipa ya mwili

Joined
Aug 20, 2025
Posts
80
Reaction score
98
Kuna mambo yananichanganya, mimi nlikuwa nafikiri mishipa ya mwili yote inafanana, lakini kuna baadhi ya watu naona wameni-prove wrong. Naona wako na mishipa yenye rangi ya KIJANI kama sio BLUU wataalamu mnijuze hiyo mishipa inapitisha damu nyekundu? Na je, ni kila mtu yuko na hiyo mishipa?
 
Mishipa hupitisha damu nyekundu na kwa mtu mwenye ngozi nyeupe huonekana kama kijani , hiyo husababishwa na rangi ya ngozi yake kuakisi taswira hiyo, hapo ni matokeo ya mwanga na rangi ya ngozi hutoa reflection za namna hiyo
 
Najibu swali lako Dodgers kama ifuatavyo Kwanza: Mishipa ya mwili haifanani,
kuna aina 2 kuu kwenye hii mishipa:


  1. Arteries (Mishipa ya damu inayotoka kwenye moyo) hii ndio hupitisha damu yenye oksijeni nyingi (damu ile nyekundu sanaaa). hii Kuta zake ni nene na huwa haionekani sana chini ya ngozi.
  2. Veins (Mishipa ya damu inayopeleka damu kutoka sehemu za mwili kurudi kwenye moyo) hii upitisha damu yenye oksijeni kidogo (damu nyekundu lakini inafanana kwa mbali na rangi ya bluu).
    • Kwa hiyo hapo bwana mdogo ule mwanga unapopenya kwenye ngozi ndio wewe unaona kama ya bluu au kijani ila kiuhalisia damu yenyewe bado ni nyekundu vilevile.
Kwa hiyo point hapo ichukue ni kuwa ngozi na tishu zinazozunguka Ile mishipa zinachuja mwanga Ndio maana unaona hivyo nq kila mtu ana veins, ila na zile rangi kuwa blue au kijani inategemea mambo kama Unene wa ngozi (watu wenye ngozi nyembamba au weupe huonekana zaidi hivyo uchujaji wa rangi huwa tofauti pia Kuna mambo kama kiwango cha mafuta chini ya Ngozi,kiwango cha mwanga hilo eneo,nk)
 
Mishipa hupitisha damu nyekundu na kwa mtu mwenye ngozi nyeupe huonekana kama kijani , hiyo husababishwa na rangi ya ngozi yake kuakisi taswira hiyo, hapo ni matokeo ya mwanga na rangi ya ngozi hutoa reflection za namna hiyo
Ooooh Kumbe!
 
Back
Top Bottom