Mishahara ya walimu ni utata

Mnaacha kuzungumzia wafanyakazi wengi wanaonyonywa mko na walimu tu. Au kwa kuwa ni wengi? Kuna wafanyakazi viwandani wanafanya kazi Muda mrefu malipo kiduchu, walioko kwenye sekta ya ujenzi wanateseka mno nyie kila mara ni walimu. Walimu mishahara inapanda kila baada ya miaka na wengi wamejiwekeza katika shughuli nyingine nyingi. Walimu wapo wanaolipwa mpaka sh milion 1.8 baada ya makato sasa huyo mtu akishindwa kuwekeza huo ni ujinga wake. Acheni kukariri mambo.
 
Sijapingana na hoja yako mkuu!! Huo ni kama ushauri kwa wale wanaoweza kuona furs a na kuchomoka mapema kwenye utumwa.

Sipendi na sijawahi nyanyasa MTU, na kwa wnaojitambua hua tunawaonyesha njia kwakua haina haja ya wao kututumikia milele.
ila tambua kila mtu haiwezekani akajiajiri, na hata kama wewe umejiajiri, lazima kuna uliyemwajiri na kama yupo mtendee haki aridhike. Hata Marekani kuna waajiriwa, hata kwa Mungu kuna walioajiriwa bosi.
 
Kuna tofauti kubwa kati ya Skilled na Unskilled labor mkuu!
BORA WALIMU HUKO KWENYE VIWANDA,MAGODOWN,UJENZI WA MAGHOLOFA WATU WANALIPWA 3000 MASAA 12 TENA KAZI ZA HATARI MNO NA SERIKALI INALIJUA HILI
 
Aliyeleta mada ni inawezekana ni mwalimu hivyo anatetea kada yake wewe kama unafanya kazi huko kwenye viwanda watetee pia.
 
Umeanza vizuri lakini umeharibu ulipogusa Bunge live
 
Ivi waalimu wana mishahara midogo kwa kiwango hiki ambacho mnajaribu kutuaminisha?ni kweli wao tu wana maisha magumu au ndio wanaotegemea mshahara tu?
Hii thread ni hadithi yenye ujumbe kua mshahara umechelewa tofauti na mazoea lakini hili la uji and blah blah ni uzushi ambao una lengo la kumuonyesha mwalimu kua ni mtu duni sana kitu ambacho ni uongo.
 
hali hiyo si kwa walimu pekee,ni karibu wafanyakazi wote wa kada ya chini.tena kuna wengine hawafiki hata hiyo 520/-
 
Mkuu ukizungumzia MTU anayekatwa HESLB,obvious huyo basic yake ni 716000,na take home yake ni 557000,(mwalimu) kwa hiyo hapo kwenye analysis ya matumizi ktk mfano wako wawezafanyia marekebisho!!!
Nami nilitaka kumsahihisha. Tena hiyo 716000 ni kwa waajiriwa ambao hawana zaidi ya miaka mitatu
 
Kwani
 
Nami nilitaka kumsahihisha. Tena hiyo 716000 ni kwa waajiriwa ambao hawana zaidi ya miaka mitatu
Na Kwamba hajapanda daraja hata mara moja. Mleta mada ungefanya kautafiti japo kidogo ili uweze kuongea mbele za watu. Waliosema no research no right to speak walijua kuna watu km mleta mada waliokariri story za abunuwasi...km unasubiri mshahara subir kimyakimya acha mawenge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…