Mioyoni tunalia wengine wanacheka ila ipo siku

oruguyo

Senior Member
Jul 28, 2012
132
37
Ni kweli tunatakiwa kulaani vitendo vyote vinavyosababisha kumwagika kwa damu za watu wasio na Hatia lakini tukumbuke Mto Ruvu watu wameokotwa wameuwawa tukaambiwa ni wahamiaji Haramu. Ni kweli?

Saanane kapotea, wengine juzi wakasema amejiteka na anatafuta umaarufu. Bashe, Msukuma na Malima wametekwa, wamelalamika hawasikilizwi. Nape Bastola imetolewa mchana peupe, hakuna hatua iliyochukuliwa kwa huyo gaidi aliyetoa bastola.

Roma na wenzake wametekwa, tukaambiwa ni tukio kama matukio mengine ya kiuhalifu. Clouds Media wamevamiwa tukaambiwa ni vikosi maalum wakishirikiana na Bashite, Wawakilishi wakapaza sauti kuwaeleza wanaodhani nchi ni yao peke yao wakasema hakuna shida hayo ni maneno tu.

Sasa viongozi yawapasa wajitathimini. Raisi na familia yake wanatembea chini ya ulinzi, mawaziri vivyo hivyo, Wakuu wa Mikoa na Viongozi Waandamizi wa Jeshi Mnalindwa. Kumbukeni hao ndugu zetu wanaouawa ndo tuliokuwa tunawategemea katika koo na familia zetu. Maamuzi yenu na ukimya wenu unatusababishia majonzi mioyoni mwetu.

Hakika nimewahi kuandika hapahapa kwenye forum hii kama mngeweka kura za siri kwa watanzania na Jeshi la polisi wawaeleze yaliyoko mioyoni mwao hakika mngegundua hakuna aliye tayari kuitetea nchi hii. Shida ndo zimetuweka ktk kazi za Serikali. Isitoshe ninyi mnaodhani mmemilikishwa madaraka na Mungu aliye juu mmekuwa ni sehemu na chachu ya kuchukiwa kwa Polisi huku Mitaani.
 
As long as the rulers and their families are safe kila kitu kipo sawa. Haya matukio ilipaswa yawakute wale wanaoyaona ya kawaida ili wajue uchungu wake upoje.
 
Nikweli tunatakiwa kulaani vitendo vyote vinavyo sababisha kumwagika kwa damu za watu wasio na Hatia, Lakini tukumbuke Mto Ruvu Watu wameokotwa wameuwawa tukaambiwa niwahamiaji Haramu, Nikweli? Saanane Kapote , Wengine juzi wakasema Amejiteka na anatafuta umaarufu, Bashe, Msukuma na Malima Wametekwa, wamelalamika hawasikilizwi,Nape Bastora imetolewa mchana Peupe, Hakuna hatua ilochukuliwa kwa huyo gaidi aliye toa bastora, Roma nawenzake wametekwa, tukaambiwa ni tukio kama matukio Mengine yakiuhalifu.Clouds Media wamevamiwa tukaambiwa ni vikosi Maalum wakishilikiana na Bashite, Wawakilishi wakapaza sauti kuwaeleza wanao dhani nchi ni yao pekeyao wakasema hakuna shida hayo ni maneno tu, Sasa viongozi yawapasa wajitathimini Raisi na Familia yake Wanatembea chini ya ulinzi, Mwaziri vivyo hivyo, Wakuuwa mikoa na Viongozi Waandamizi wa Jeshi Mnalindwa, kumbukeni Haondugu zetu wanao uwawa ndo tuliokuwa tunawategemea katika koo na familia zetu Maamzi yenu na ukimya wenu unatusababishia majonzi mioyoni mwetu. Hakika nimewahi kuandika hapahapa kwenye forum hii kama mngeweka kura za siri kwa watanzania na jeshi la polisi wawaeleze yaliyoko mioyoni mwao hakika mngegundua hakuna aliye tayali kuitetea Nchi hii, Shida ndo zimetuweka ktk kazi za Serikali, Isitoshe ninyi mnaodhani Mmemilikishwa Madaraka na Mungu aliye juu Mmekuwa ni sehemu na Chachu ya kuchukiwa kwa Polisi huku Mitaani.
Wapiga ramli maarufu kutoka ukoo wa nyumbu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom