Mikopo ya Benki na Matumizi Sahihi kwa Watumishi

Hata wewe umeeleza point mkuu
Mkuu mimi nina zaidi ya miaka 10 kwenye ajira ya serikali hivyo nilishajenga kitambo tu kupitia mkopo wangu wa pili wa benki! Ule wa kwanza kama ilivyo kwa vijana wengi, nilinunulia gari (corolla kwa enzi zile, nilitisha sana).

Sema tu kuna jamaa hapo juu (bossless) ameelezea point yenye tija pia. Kuna baadhi ya watumishi wanaumia kwa sasa baada ya kukopa ili wajenge halafu kwa kutokujua, wakajenga majumba makubwa aidha kwa kuiga au kushindwa kuitafsiri ramani!

Mwisho wa siku nyumba imeshindwa kukamilika, halafu wanalipishwa deni na riba juu! Hapa lazima uuchukie ujenzi. Jambo la msingi ni kuanza na nyumba ndogo ya kawaida (ikibidi mabanda ya uwani) itakayotosheleza mahitaji ya pesa uliyokopa then unahamia kwako! Baadae ikishatulia, ndipo ujenge nyumba ya kustaafia. Mimi nilifanya hivyo na sijutii kwa hayo maamuzi yangu.
 
Kingine pia wanawake hamna pressure ya vitu alivyosema mdau plus kuongwa ndo maana huwezi kukopa bank.
Wanaume VICOBA haviwafai wengi hawaogopi madeni.

Kijana kabla ya kukopa ni vyema akiingia kazini aanze kufanya vibiashara vyenye mtaji mdogo ili kupata hela ambayo atasave anaweza hata kufungua fixed account akaweka huko.

Bila kufanya biashara au ujasiriamali wowote sioni njia mbadala zaidi ya kukopa.
 
Nachokiona watu wengi sana wanachukia kupanga nyumba, lakini unakuta hao wanaopanga sehemu zenyewe zinaanzia 70,000-200,000 sasa sijui huyu mtu anasikia uchungu gani kulipa hio hela...ila katika jambo ambalo ni gumu ni kukopa wakati ukiwa hauna gari, hauna kiwanja ila kwa mwanaume kua na kiwanja inakupa confidence hatari kazi ninayoofanya sasa hivi nilikua naichukia sana maana nilikua sioni la maana nililolifanya hadi pale niliponunua kiwanja walau sasa hivi naweza kuwaza kuvuta mashine kwa mkopo maana ni bora nione mkopo nimenunua gari na nyumba naisimamisha hadi kwenye linta/lenta mwakani nihamie kwangu na mchuma wangu mpya
 
Nachokiona watu wengi sana wanachukia kupanga nyumba, lakini unakuta hao wanaopanga sehemu zenyewe zinaanzia 70,000-200,000 sasa sijui huyu mtu anasikia uchungu gani kulipa hio hela...ila katika jambo ambalo ni gumu ni kukopa wakati ukiwa hauna gari, hauna kiwanja ila kwa mwanaume kua na kiwanja inakupa confidence hatari kazi ninayoofanya sasa hivi nilikua naichukia sana maana nilikua sioni la maana nililolifanya hadi pale niliponunua kiwanja walau sasa hivi naweza kuwaza kuvuta mashine kwa mkopo maana ni bora nione mkopo nimenunua gari na nyumba naisimamisha hadi kwenye linta/lenta mwakani nihamie kwangu na mchuma wangu mpya
Ningeshauri Uanzishe mradi, kuliko kukimbilia kununua Ilo gari mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nachokiona watu wengi sana wanachukia kupanga nyumba, lakini unakuta hao wanaopanga sehemu zenyewe zinaanzia 70,000-200,000 sasa sijui huyu mtu anasikia uchungu gani kulipa hio hela...ila katika jambo ambalo ni gumu ni kukopa wakati ukiwa hauna gari, hauna kiwanja ila kwa mwanaume kua na kiwanja inakupa confidence hatari kazi ninayoofanya sasa hivi nilikua naichukia sana maana nilikua sioni la maana nililolifanya hadi pale niliponunua kiwanja walau sasa hivi naweza kuwaza kuvuta mashine kwa mkopo maana ni bora nione mkopo nimenunua gari na nyumba naisimamisha hadi kwenye linta/lenta mwakani nihamie kwangu na mchuma wangu mpya
aisee . . . Mi nadhani suala la msingi katika mikopo ni vipaumbele tu. Kama ni kukopa kwa ajili ya kununua kiwanja basi fanya hivyo. Jamaa mmoja amekopa milioni 9 kanunua kiwanja katulia zake tu anasubiri mkopo uishe akope ya kujengea na kununua mkoko. Pia suala la gari ni kipaumbele tu maana ndio matumizi yenyewe hayo ya pesa
 
Kwani sisi tunaomkumbukaga JKIKWETE ni wajinga? Jamaa kiana aliruhusu wizi wa kisela utumishini na ofisi zilikuwa zinajiendesha ila huyu kabana wizi kwa hiyo mshahara unakuwa mgumu kuugawanya ila sio mbaya tunaongezewa akili
 
Last week kuna mdau alizungumzia kuhusu kufanya maamuzi ya kuacha kazi ili akapige mishe zingine mtaani, kwenye mjadala ikaibuka point ya makato ya mikopo kuwa mikubwa kiasi cha kusababisha net kuwa ndogo kiasi cha kutokidhi mahitaji.

Nikawaza kwamba hili tunaweza kulijadili kama topic inayojitegemea.

Hii itawahusu zaidi wale wanaoanza kazi kwa mara ya kwanza, baada ya kutokea vyuoni. Ingawa pia hata wale ambao tuko makazini tayari na tumeshauingia huu mtego tunalo la kujifunza na kuangalia namna sahihi ya kudili nalo.

Unapoanza kazi kunakuwa na changamoto kuu mbili, makazi na usafiri; hizi ndizo kwangu nimeona kama ndizo hasa zinaongoza kwenye mlolongo wa mahitaji.

Nitaiandika kwa kutumia mfano wa kijana wa kiume ambaye ameanza kazi na Gross Salary ya Tshs 1,000,000/- kila mmoja ataiweka kulingana na mazingira yanayomhusu.

Gross ya 1m makato ya NSSF ni 100,000, kodi ni 150,000/- kwa hiyo jumla ya makato ni shilingi 250,000/- bila kuweka Loan Board. So, take home ni 750,000/-.

Familia zetu nyingi, kijana anapoanza kazi anatakiwa kuondoka nyumbani kwenda kukaa kivyake, pia kuna wale tunaotokea mikoa tofauti na tulipopata kazi hivyo zoezi la kupanga linahusika.
Kwa net ya 750,000/- unaweza kupanga chumba kimoja chenye self-contained kwa 100,000-150,000 kwa mwezi maisha yakaenda. Hapo ndani ya mwaka mzima utajikuta una zoezi la fridge, makochi, redio, TV, nk. Matumizi ya kila siku ni yaleyale, msosi, nauli, mavazi, kwa wale wa moja moto moja baridi pia.

Soon mawazo ya gari ama kiwanja yanakuja kichwani, maana unajikuta washkaji wana magari wewe unazunguka on foot, au washkaji wanakwambia issue za kununua kiwanja ili ujenzi uanze. Hizi pia zinakuwa influenced na wapenzi (partners), unapoanza kazi na ukawa na mshahara mzuri, ndicho kipindi cha kutafuta mtu au cha kuwa na mtu ambapo mnaweza hata kutoka mkaenda sehemu za starehe, za kupunga upepo au ukamnunulia baadhi ya vitu, swala la usafiri linakuja pale ambapo mnalazimika kupanda daladala wakati mmependeza, hapo utaanza kuona umuhimu wa kutafuta gari.

Mawazo ya kununua gari au kiwanja yakishakuja, kwa mshahara huo na matumizi niliyoyataja, uwezekano wa kwamba umesevu 5m za ndani ya miaka hata 3 ni ngumu, hivyo, unaamua kwenda benki kukopa.

Kwa net ya 750,000/- bank unaweza kupata mkopo wa shilingi 14,500,000/ na makato ya mwezi yatakuwa ni around 370,000/- kwa rate ya 18%. Maana yake hapo utabaki na net isiyozidi 400,000/-.

Kazi ni kwako, ununue gari 10,000,000/- au ununue kiwanja. Kwa options zote mbili hakuna lenye faida;-
  • Ukinunua gari, tayari una makato ya 350,000/-, gari kwa mwezi linakula zaidi ya 150,000/- na siyo gari la biashara, hapo tayari umeshajipa kifungo cha miaka 5 cha kuhangaika na gari na mkopo, unaanza kuwaza nyongeza za mishahara, ulipo huongezewi unaanza kutafuta kuhama kazi, unajikuta ndani ya miaka 5 huna kazi uliyoweza kui-master kwa sababu hutulii sehemu moja ukajifunza.
  • Ukinunua kiwanja ukaanza kujenga, hiyo hela haitoshi kumaliza nyumba, hivyo utakuwa unakaa kusubiri top up ili uendeleze, kumbuka pango linakudai, makato ya benki yapo yanakudai pia. Frustrations za nyongeza za mishahara zinaanza, unajikuta matumizi pia yanazidi. Pressure zinakupeleka kule kule kuanza kutafuta kazi.
Kuna exceptions, kuna wale ambao kazi zao zinawapa nafasi ya kupata allowances katikati ya mwezi na hivyo maisha kusonga.

Nini cha kufanya:
Saving, hii ni kitu muhimu sana, mfano ukijiwekea malengo ya kusema nitanunua gari/kiwanja bila mkopo, unafanya saving mdogo mdogo bila pressure, hata kazi unakuwa unaipenda na uko likely ku-grow kwa sababu akili yako umeiweka hapo.

Kuna wale wenye minds za entrepreneurship, kopa fanya biashara ambayo unajua itakuwa inarudisha makato ya benki na unabaki na faida kiasi, baada ya muda unaweza kufanya vitu vikubwa. One thing to note, business is not everyones’ cup of tea.

Kuna umuhimu wa kupata ushauri kwa watu mbalimbali na kuufanyia upembuzi ili ikitokea ukaamua kuchukua mkopo iwe ni kwa matumizi sahihi ambayo hayakuingizi kwenye kukufix.
Nafungua mjadala wa nini kinaweza kufanyika ili kuepukana na hili janga la kujifix kwenye mikopo ya benki na kuishia kuiona kazi ni chungu, maana mwezi mzima unafanyia makato tu.
Umeandika kitu ambacho kinagusa watu wengi nikiwepo Mimi Ila mi nina fikra tofauti kwamba katika vitu vinavyosaidia kuboost maisha ya wafanyakazi basi uwezi kusahau mikopo.

Ukweli ni kuwa kibongo kumiliki nyumba au gari ni sign ya maendeleo kama sio utajiri so kwa nature ya mishahara na mfumo wa maisha yetu bila mikopo kumiliki hivyo vitu inabaki kuwa ndoto.

Kuishi maisha ya shida huku umetimiza shauku yako it's okay kuliko kuishi vizuri wakati vitu ambavyo una interests navyo havipo.

Pointi yangu ni kuwa as long unaona mkopo wako umefanya kitu flani ni sawa kuliko kukaa muda mrefu bila kutimiza dreams zako maisha yenyewe mafupi.
 
Umeandika kitu ambacho kinagusa watu wengi nikiwepo Mimi Ila mi nina fikra tofauti kwamba katika vitu vinavyosaidia kuboost maisha ya wafanyakazi basi uwezi kusahau mikopo.

Ukweli ni kuwa kibongo kumiliki nyumba au gari ni sign ya maendeleo kama sio utajiri so kwa nature ya mishahara na mfumo wa maisha yetu bila mikopo kumiliki hivyo vitu inabaki kuwa ndoto.

Kuishi maisha ya shida huku umetimiza shauku yako it's okay kuliko kuishi vizuri wakati vitu ambavyo una interests navyo havipo.

Pointi yangu ni kuwa as long unaona mkopo wako umefanya kitu flani ni sawa kuliko kukaa muda mrefu bila kutimiza dreams zako maisha yenyewe mafupi.

True, it's all about daring. Otherwise, you won't meet ¼ of your dreams.

Calculated risks should be put in place though.
 
Mleta mada asante kwa kutufungua akili.
Naona ile presha ya kuhudumia ndugu I mean kusomesha ndugu hujaiweka. Yaan tupo vijana tulioanza kazi na familia baba, mama na wadogo zetu ndio wanatuangalia hujaitaja kabisa na hii sababu inatuvuna sio kidogo na tunaizoea maana inatuweka mbali na vishawishi na tunakuwa makini.

Umetolea mfano wa mtu aliopo kuajiriwa kwenye mashirika ya Umma na mashirika mengine ya watu binafsi. Sidhani kama juniour staff wa huku serikalini nikiwa namaanisha kwenye wizara na idara nyingine anaweza anza na mshahara huobwa milioni na take home ya 750k.....
Mwalimu wa degree anaanza na 716k na take home ya 454k hapo ni baada ya makato yoote hadi bodi ya mikopo(HESLB).

Ukijikuta una fikiria sana na kupata mawazo kama ulioanzisha na wadau wanayochangia akili inafunguka na sana utapata majawabu ya maswali vijana tunayojiuliza.

Ukijikita unatamani sana kununua gari utajikuta makampuni na qnet, aim global forever yanakuteka fasta.
Nimeona vijana wengi wanakopa hadi milioni 5 wanapeleka huko qnet.
Aiseeee....
 
Mkuu ogopa sana kuwa 1st born, mtoto wa mjane utaingia mtegoni tu.
 
Mleta mada asante kwa kutufungua akili.
Naona ile presha ya kuhudumia ndugu I mean kusomesha ndugu hujaiweka. Yaan tupo vijana tulioanza kazi na familia baba, mama na wadogo zetu ndio wanatuangalia hujaitaja kabisa na hii sababu inatuvuna sio kidogo na tunaizoea maana inatuweka mbali na vishawishi na tunakuwa makini.

Hii point sijui hata niliisahau vipi, maana ni point muhimu sana aisee.

Shukrani kwa kuiongezea.
 
Last week kuna mdau alizungumzia kuhusu kufanya maamuzi ya kuacha kazi ili akapige mishe zingine mtaani, kwenye mjadala ikaibuka point ya makato ya mikopo kuwa mikubwa kiasi cha kusababisha net kuwa ndogo kiasi cha kutokidhi mahitaji.

Nikawaza kwamba hili tunaweza kulijadili kama topic inayojitegemea.

Hii itawahusu zaidi wale wanaoanza kazi kwa mara ya kwanza, baada ya kutokea vyuoni. Ingawa pia hata wale ambao tuko makazini tayari na tumeshauingia huu mtego tunalo la kujifunza na kuangalia namna sahihi ya kudili nalo.

Unapoanza kazi kunakuwa na changamoto kuu mbili, makazi na usafiri; hizi ndizo kwangu nimeona kama ndizo hasa zinaongoza kwenye mlolongo wa mahitaji.

Nitaiandika kwa kutumia mfano wa kijana wa kiume ambaye ameanza kazi na Gross Salary ya Tshs 1,000,000/- kila mmoja ataiweka kulingana na mazingira yanayomhusu.

Gross ya 1m makato ya NSSF ni 100,000, kodi ni 150,000/- kwa hiyo jumla ya makato ni shilingi 250,000/- bila kuweka Loan Board. So, take home ni 750,000/-.

Familia zetu nyingi, kijana anapoanza kazi anatakiwa kuondoka nyumbani kwenda kukaa kivyake, pia kuna wale tunaotokea mikoa tofauti na tulipopata kazi hivyo zoezi la kupanga linahusika.
Kwa net ya 750,000/- unaweza kupanga chumba kimoja chenye self-contained kwa 100,000-150,000 kwa mwezi maisha yakaenda. Hapo ndani ya mwaka mzima utajikuta una zoezi la fridge, makochi, redio, TV, nk. Matumizi ya kila siku ni yaleyale, msosi, nauli, mavazi, kwa wale wa moja moto moja baridi pia.

Soon mawazo ya gari ama kiwanja yanakuja kichwani, maana unajikuta washkaji wana magari wewe unazunguka on foot, au washkaji wanakwambia issue za kununua kiwanja ili ujenzi uanze. Hizi pia zinakuwa influenced na wapenzi (partners), unapoanza kazi na ukawa na mshahara mzuri, ndicho kipindi cha kutafuta mtu au cha kuwa na mtu ambapo mnaweza hata kutoka mkaenda sehemu za starehe, za kupunga upepo au ukamnunulia baadhi ya vitu, swala la usafiri linakuja pale ambapo mnalazimika kupanda daladala wakati mmependeza, hapo utaanza kuona umuhimu wa kutafuta gari.

Mawazo ya kununua gari au kiwanja yakishakuja, kwa mshahara huo na matumizi niliyoyataja, uwezekano wa kwamba umesevu 5m za ndani ya miaka hata 3 ni ngumu, hivyo, unaamua kwenda benki kukopa.

Kwa net ya 750,000/- bank unaweza kupata mkopo wa shilingi 14,500,000/ na makato ya mwezi yatakuwa ni around 370,000/- kwa rate ya 18%. Maana yake hapo utabaki na net isiyozidi 400,000/-.

Kazi ni kwako, ununue gari 10,000,000/- au ununue kiwanja. Kwa options zote mbili hakuna lenye faida;-
  • Ukinunua gari, tayari una makato ya 350,000/-, gari kwa mwezi linakula zaidi ya 150,000/- na siyo gari la biashara, hapo tayari umeshajipa kifungo cha miaka 5 cha kuhangaika na gari na mkopo, unaanza kuwaza nyongeza za mishahara, ulipo huongezewi unaanza kutafuta kuhama kazi, unajikuta ndani ya miaka 5 huna kazi uliyoweza kui-master kwa sababu hutulii sehemu moja ukajifunza.
  • Ukinunua kiwanja ukaanza kujenga, hiyo hela haitoshi kumaliza nyumba, hivyo utakuwa unakaa kusubiri top up ili uendeleze, kumbuka pango linakudai, makato ya benki yapo yanakudai pia. Frustrations za nyongeza za mishahara zinaanza, unajikuta matumizi pia yanazidi. Pressure zinakupeleka kule kule kuanza kutafuta kazi.
Kuna exceptions, kuna wale ambao kazi zao zinawapa nafasi ya kupata allowances katikati ya mwezi na hivyo maisha kusonga.

Nini cha kufanya:
Saving, hii ni kitu muhimu sana, mfano ukijiwekea malengo ya kusema nitanunua gari/kiwanja bila mkopo, unafanya saving mdogo mdogo bila pressure, hata kazi unakuwa unaipenda na uko likely ku-grow kwa sababu akili yako umeiweka hapo.

Kuna wale wenye minds za entrepreneurship, kopa fanya biashara ambayo unajua itakuwa inarudisha makato ya benki na unabaki na faida kiasi, baada ya muda unaweza kufanya vitu vikubwa. One thing to note, business is not everyones’ cup of tea.

Kuna umuhimu wa kupata ushauri kwa watu mbalimbali na kuufanyia upembuzi ili ikitokea ukaamua kuchukua mkopo iwe ni kwa matumizi sahihi ambayo hayakuingizi kwenye kukufix.
Nafungua mjadala wa nini kinaweza kufanyika ili kuepukana na hili janga la kujifix kwenye mikopo ya benki na kuishia kuiona kazi ni chungu, maana mwezi mzima unafanyia makato tu.
Asante sana mtoa hoja;
Suala la kukopa sio baya, cha msingi ni kujiuliza unakopa ili ufanye nini?? kwa mishahara ya Kitanzania na aina ya maisha ya utegemezi uliopo ni ngumu sana kuweka akiba kutoka ktk mshahara kwa kiwango cha kupata kiasi cha kufanya jambo kubwa kwa muda mfupi. Hivyo ukitaka kukamilisha jambo lako la muhimu, kukopa hakukwepeki. Muhimu ni kukopa kwa malengo yenye tija.
 
Wakuu
Nilianza kazi ni basic ya laki 3 mwaka 2011 katika kampuni binafsi ya wahindi,hakuna mkopo katka benk niliyokuwepo. Nadhan mnaweza kuelewa hali ilivyokua japo sikua na familia,baada ya mwaka ikaja bank inatoa mkopo wa mwaka mmoja nilikua napata kama mil 1.5 na huo nikiupata unanikuta na madeni ya kutosha kwahyo najikuta nabaki na kama sh laki 6 au 7. Nimesota sana kwa mua wa kama miaka 6 na mkopo huo wa mwaka mwaka,nikiangalia ndan sina chochote cha thaman na tayar nina familia,madeni ndo yalikua yananipa stress sio za kawaida. Juzi kati kuna bank ilikuja ikatoa mikopo nashukuru nilipata kama mil 12 na hii inatokana mshahara wangu kwa kipindi hicho basic ilikua laki 8.5 na pia nina mkataba wa kudumu. Niseme ukwel sikukopa ili nijenge au ninunue gar au nifanye biashara,lengo langu la kwanza nilikopa kwanza nilipe madeni mengne niliyokua nayo maana nadhan weng wetu mnajua kudaiwa kunavyotoa kwenye mchezo,pili nilitaka ninunue vitu ndani angalau hata nikipata mgeni akija ndani aone kuna mtu anafanya kazi na hapa ndo kwake. Suala ka kulipa madeni nimefanikiwa kwa asilimia 90 na la kununua vitu nimefanikiwa kwa asilimia 97 naweza kusema,kiasi kidogo kilichobaki ilikua ni matumizi madogomadogo ya hapa na pale. Makato ndo maumivu mapya kwasasa lakini hamna namna nasubir baada ya miaka mitatu nimalize mkopo afu nikope tena kwa ajili ya wazo ntakalokua nalo kwa kipindi hicho. Labda niulize kwenye matumizi ya huo mkopo kuna mahali nimekosea?
Asanteni
 
Back
Top Bottom