Mifumo ya Uchaguzi Nchini Tanzania imeparalysis

Mifumo ya Uchaguzi Nchini Tanzania imeparalysis

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,715
Reaction score
59,249
Sasa ni rasmi kwamba Mifumo ya Uchaguzi Tanzania imeparalysis.

Mfano:
CCM ni chama kinachotawala( Chama cha Mapinduzi)

Mchengerwa ni Mpiga kura wa CCM, Mwanachama wa CCM na Mbunge wa CCM lakini ndo anasimamia Uchaguzi ambao CCM inagombea na vyama vingine. Aibu sanaa..

Mchengerwa ni Mkwe wa Mwenyekiti wa CCM na Huyu Mwenyekiti anataka chama chake Kishinde. Ujinga.

Wasimamizi wa Sheria hata wakiiba kura, wakifanya wakitangaza mgombea ambaye hajashinda hakuna cha kuwafanya kwani Sheria inawalinda.

Wasimamizi wa Uchaguzi ambao ni wanachama wa CCM, wanateuliwa na mwenyekiti wa CCM.

Naiandika hii ili Vizazi vijavyo vijue Nchi yao imepitia mapito gani.

Kizazi hiki tunamlaumu Mangungo, lakini Vizazi vijavyo vitatushangaa sana. Wataulizana iliwekekanaje ukaitwa Uchaguzi?

Watu wanasema nenda Mahakamani. Huko mahakamani unamkuta mteule wa Mwenyekiti wa CCM ambaye simu ikipigwa na Mwenyekiti anafuata Maelekezo.

Soma zaidi: Rostam Aziz: Hakuna mwekezaji atakubali kuwekeza halafu umwambie aende Mahakama ya Kisutu ambapo Majaji wanaweza kupigiwa simu na watu wa Serikali

Kuu wa Polisi anateuliwa na Mwenyekiti wa CCM.

Tunashuhudi jinsi Vyama pinzani vinasurubiwa na Polisi ili Anayefsnya uteuzi afurahi.
Bado naamini Tanzania tutafika pamoja na mapungufu yote.

So huu ni Ujumbe kwa Watoto wetu. Wasiache kutuheshimu ila Utawala wa Sheria ulivyo Tanzania. Kama unataka utawala wa Sheria kubaliana na haya otherwise ingia msituni.

Pia soma; Huu ndio mkataba wa Karl Peters na Chifu Mangungo ulitufanya tunawekwa chini ya Mjerumani
 
Alhamdulilah, tumemaliza uchaguzi wetu kwa amani, Utulivu wa hali ya juu, hakika Tanzania ni mfano mwema hata kwa mataifa mengine!
 
Ni aibu kubwa kwa Rais Samia, uchaguzi wa hovyo kabisa huu bora hata ule wa JIWE yeye alisema wazi wazi ole wake atakayemtangaza mgombea wa upinzani eti kapita.
 
Back
Top Bottom