Mifuko ya plastiki ni janga la mazingira

Mifuko ya plastiki ni janga la mazingira

kasinge

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2011
Posts
1,259
Reaction score
319
Enyi wanamazingira, hivi Serikali inapata kiasi gani katika mifuko ya plastiki. Hata kama wanasema kwamba siku hizi wanazalisha mifuko inayooza, bado mifuko imeendelea namba moja katika uchafuzi wa mazingira hasa Dar es salaam. Na kama inaoza, basi inachukua muda mrefu. Mimi nadhani mifuko hii ipigwe marufuku kuzalishwa. Nchi hii bana, kila mtu anafanya anachotaka.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Enyi wanamazingira, hivi Serikali inapata kiasi gani katika mifuko ya plastiki. Hata kama wanasema kwamba siku hizi wanazalisha mifuko inayooza, bado mifuko imeendelea namba moja katika uchafuzi wa mazingira hasa Dar es salaam. Na kama inaoza, basi inachukua muda mrefu. Mimi nadhani mifuko hii ipigwe marufuku kuzalishwa. Nchi hii bana, kila mtu anafanya anachotaka.
Kaka Nakuunga mkono mia kwa mia tupaze sauti kusema hapana kwa plaatiki angalia jiji la dar Barbara mpya Imejengwa mamifuko kila mahali hivi waziri huaika anataka na hili Raid alitolee kauli?
 
Nyie wenyewe mjiulize ustarabu wenu uko wapi??wangapi kati yenu hawatupi.uchafu ovyo barabarani au pahala.popote pasipostahili...serikali ni wewe na na mimi tuunganishe nguvu badili tabia kwanza..
 
plastic-bags.png
 
Nyie wenyewe mjiulize ustarabu wenu uko wapi??wangapi kati yenu hawatupi.uchafu ovyo barabarani au pahala.popote pasipostahili...serikali ni wewe na na mimi tuunganishe nguvu badili tabia kwanza..
Katika jamii ya watu ambao sio wastarabu, hatua ya kwanza ni kupiga marufuku mifuko. Ustaarabu wetu hauji leo wala kesho. Mi nadhani tuipige marufuku huku tukiendelea kupeana Ustaarabu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hapo kwenye ustaarabu umeongea neno kubwa sana. Kuna miji mingi duniani ambayo mifuko hii ya plastic hutumika katika supermarkets na maduka mbali mbali mengine lakini wenzetu wamekuwa na ustaarabu wa hali ya juu kwenye usafi kiasi ambacho huwezi kuona hata mfuko mmoja wa plastick umezagaa hovyo hovyo.

Katika jamii ya watu ambao sio wastarabu, hatua ya kwanza ni kupiga marufuku mifuko. Ustaarabu wetu hauji leo wala kesho. Mi nadhani tuipige marufuku huku tukiendelea kupeana Ustaarabu.
 
Zanzibar ukikamatwa na mfuko wa plastiki faini yake utatamani huo mfuko uutafune ule
 
Inaskitisha sana uchafuzi wa mazingira imekuwa sehemu ya utamaduni wetu sababu kila siku unaongeke uchafuzi has a plastiki katika miji yeti. Namkumbuka Mkuu WA Mkoa Kagera kwa jitihada zake.
 
Nyie wenyewe mjiulize ustarabu wenu uko wapi??wangapi kati yenu hawatupi.uchafu ovyo barabarani au pahala.popote pasipostahili...serikali ni wewe na na mimi tuunganishe nguvu badili tabia kwanza..

umenena! sio tu mifuko, unakuta mtu anakunywa soda, maji then anatupa tu 'container', tena barabarani. au vocha, tikiti za daladala na takataka nyingine kama hizo! hapa cha kufanya ni watu kuamua kubadilika; mamlaka husika ziweke sehemu za kuhifadhi taka njiani, ukiwa na takataka vumilia mpaka ukute mahali pa kutupa. ukiwa kwenye daladala wacha takataka ndani; nimeona kuna daladala zina 'dust-bins', ambazo hazina waweke. usafi huvutia, angalia miji misafi ulimwenguni ilivyo, ukiwa humo unajisikia ahueni!
 
Solution ni kufanya recycle tu kuzuia matumizi so hard sababu matumizi yake ni makubwa coz of durability which is affordable kwa lower class
 
Mimi nashangaa nchi hii bunge lilipiga marufuku kuhusu hii mifuko ya plastic yenye kipenyo kidogo (mifuko ya kondomu) lakini mpaka leo inazagaa mtaani au wakati ule walifanya kumkomoa Bakheresa na maji yake aliyokuwa anayoifunga kwenye mifuko ya plastiki ya sh 50.
 
Mimi nashangaa nchi hii bunge lilipiga marufuku kuhusu hii mifuko ya plastic yenye kipenyo kidogo (mifuko ya kondomu) lakini mpaka leo inazagaa mtaani au wakati ule walifanya kumkomoa Bakheresa na maji yake aliyokuwa anayoifunga kwenye mifuko ya plastiki ya sh 50.
Kiwanda cha mifuko inayooza kiko wapi
 
Kuna documentary moja nimeiona RT television ya urusi ikizungumzia chupa zs plastic hizi aiseee kwa afrika hakuna dampo la coca cola kama Tanzania.
.
Majamaa walivyo na dharau wakaanza na title ya ile filamu ya wanyama "Unforgettable Tanzania" wakaonyesha uzuri wa dar es salaam kwa view ya juu mara paap nikasikia "This is the real Tanzania eee bwana weee ni milima ya plastic bottle kuna jina wanaziita limenitoka beach chafu mitaro haifai kila mahala ni plastic bottles.
Mkurugenzi wa coca cola duniani alivyoonyeshwa ile clip alianza kujing'ata anaulizwa kwanini mnaiharibu " Tanzanie" hana jibu
 
Kuna documentary moja nimeiona RT television ya urusi ikizungumzia chupa zs plastic hizi aiseee kwa afrika hakuna dampo la coca cola kama Tanzania.
.
Majamaa walivyo na dharau wakaanza na title ya ile filamu ya wanyama "Unforgettable Tanzania" wakaonyesha uzuri wa dar es salaam kwa view ya juu mara paap nikasikia "This is the real Tanzania eee bwana weee ni milima ya plastic bottle kuna jina wanaziita limenitoka beach chafu mitaro haifai kila mahala ni plastic bottles.
Mkurugenzi wa coca cola duniani alivyoonyeshwa ile clip alianza kujing'ata anaulizwa kwanini mnaiharibu " Tanzanie" hana jibu
Mnapomuweka waziri wa mazingira asiejitambua mnategemea nini? Nendeni Rwanda mkaone..
 
Back
Top Bottom