Mifuko ya plastiki kupigwa marufuku

Mifuko ya plastiki kupigwa marufuku

Jemmie

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2018
Posts
216
Reaction score
285
Serikali ya Tanzania imesema iwapo watakubaliana na taasisi mbalimbali wanazotarajia kukutana nazo wiki hii wanaweza kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kuanzia Julai mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Aprili 8, 2019 na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kaliua (CUF) Magdalena Sakaya. Sakaya amesema majibu ya Serikali kuhusu upigaji marufuku wa mifuko hiyo hayaonyeshi dhamira ya dhati ya kupiga marufuku.

“Mifuko mbadala ipo, wakinamama wanasuka vikapu vya ukili lakini haina masoko, mifuko ya plastiki inatolewa bure. Tatizo si mifuko mbadala bali kulinda viwanda vinavyoharibu mazingira,” amesema.

Amesema hakuna asiyejua madhara ya mifuko ya plastiki na kuhoji Serikali ina mpango gani wa kupiga marufuku mifuko hiyo badala ya kupoteza muda na gharama kama nchi nyingine zilivyofanya za na kufanikiwa.

Akijibu swali hilo, Makamba amesema bajeti inayokuja ya ofisi yake Aprili 16 mwaka huu wanaweza kutangaza hatua watakayoichukua.

Amesema kuwa wiki hii Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza kukutana na taasisi mbalimbali ikiwemo Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Baraza la Mazingira Nchini (Nemc) na Wizara ya Mambo ya Ndani kujadili suala hilo. “Kanuni tayari zinangoja kuchapishwa kwenye gazeti la Serikali.

Kama tukikubaliana inaweza Mei ukawa mwisho wa matumizi ya plastiki,”
 
Wanahongwa na wahindi wanaotengeneza hii mifuko huko viwandani ndo maana hili suala linapigwa danadana.
Ni miaka 10 sasa tangu huu mchakato uanze, lakini wahindi hutembeza sana rushwa na kuendeleea kuua watu na hizo sumu
 
Ukiwa na waziri hana maamuzi yoyote zaidi ya kupiga sarakasi, tumbua haraka sana ni bora hata Mpina apelekwe huko. Kuna kiwanda kipo morogoro wanatumia magogo ya miti kuendesha kiwanda, unakuta fuso kama 20 zimejaza magogo zinasubiri kushusha. Hapo unaambiwa kuna wizara ya mazingira, kuna watu wana masihara nchi hii
 
Heri yangu nimetoka kula wali maharagwe kwa mama Kidawa, sijui kaweka hamira, utasema nimepiga K-Vant, fulu usingizi. Senema za mifuko ya pulasitiki nimeshachoka
 
Mifuko ya plastic inaleta ugonjwa wa cancer maana siku hizi wakina mama lishe wanapopika wali wanaifunikia na mifuko ya pastic juu ya moto ili joto lisitoke ivee haraka ile joto linayayusha kemikali ya plastc na kungia kwenye wali nakuwa sumu hata wanaochemsha mihogo na viazi au mahindi ni hivyohivyo wanasababisha ugonjwa wa cancer kuenea sijui mabwana afya wako wapi
 
Sasa mkuu unatarajia nini kama umeonyeshwa bank payee tshs 570mil kwa kamati yako?
Ofisi ya waziri wa mazingira na hata Nemc hawako serious katika hili suala zaidi ya danadana za kisiasa tu,
Wanalinda masilahi ya wenye viwanda vya plastic.
 
Wakati sasa umefika kuchagua, kuharibu mazingira ya nchi yetu au kuwahurumia wenye viwanda vya Mifuko ya Plastiki. Lakini tukumbuke wazalishaji wote wa Mifuko ya Plastiki waliopigwa marufuku kwenye nchi za wenzetu Afrika ya Mashariki kama Kenya, Uganda na Rwanda watakimbilia TZ ili wayahatibu mazingira yetu. It’s time now to make positive decision.
 
Back
Top Bottom