Mid bakery industry

aseenga

Senior Member
Joined
Jul 13, 2011
Posts
106
Reaction score
86
Salaam wanaJF

Nataman sana kujua gharama za uanzishwaji wa kiwanda kidogo cha kutengeneza mikate. Yapo mambo ya msingi ninayotaka kujua zaid.

Jambo kubwa zaidi ni gharama ya uanzishwaji wake hasa katika mashine. Mf gharama ya mixing, mashine ya kuoka, cutting mashine na mashine nyinginezo kama zipo.

Msaada wenu utanijenga mm na wengine pia.
 
Sangoa orodhesha mashine zote mkuu kwa msaada zaid
 
Kwa mikate unatakiwa mashine nne
1.mixer mashine bei zake start from 1.5 mill and above. Nzuri standard for commercial business ni around 3 mill
2.Oven mashine. Hapa zipo za gas na umeme. Zina start from deck 1,2 or 3 Na bei zake zinaanzia mill 1.2 hadi 9 mill
3.cake improver zinaanzia Laki 8 hadi 1.6, hii ni kwa ajili ya kuumulia dough ya mkate pia unaweza tumia local methods
4.slicer mashine kwa ajili ya kukatia sless Za mikate
 
Local method ni zipi?
Vipi Kama nataka nitengeneze sconsi Kama 300 hivi kwa siku nikiwa na mixer pamoja na oven ndogo si zinatosha?
 
Local method ni zipi?
Vipi Kama nataka nitengeneze sconsi Kama 300 hivi kwa siku nikiwa na mixer pamoja na oven ndogo si zinatosha

Local method ni zipi?
Vipi Kama nataka nitengeneze sconsi Kama 300 hivi kwa siku nikiwa na mixer pamoja na oven ndogo si zinatosha?
Ili uwe confortable, Kwa sconsi 300 tafuta
1) oven ya deck 3 ya umeme ni 4m na gesi ni 4.5m
2) dough mixer ya 15kg au 20kg ni 2m -3m
3) proofer ni 2.5m
4) makopo/scons cans 100pcs@8,000(aluminum nzr) 800,000
5) meza iwe kubwa napendelea 6×3ft
6)mzani digital scale 150,000
7)kifungio plastic bag sealer ni 50,000
8)mifuko minimum kiwandani ni 50kg @ 7,000 = 350,000
9) maandalizi ya kutengeneza hiyo mifuko kadiria 100,000
10) kweny wiring tumia Fundi mzr na vifaa vya ukweli maana oven ni heater sio mota, inakula umeme vzr na ni hatari kutumia vifaa magumashi
11) sasa mkuu hayo yote chamtoto ngoma ipo kwa TBS na ndugu zake ila kiurahisi pitia sido ndo mambo yako yatanyooka kimtindo.
ANGALIZO: BEI ZA VITU INATEGEMEA UNANUNULIA WAPI, UBORA GANI, UKUBWA GANI, MAKE YA WAPI NA KAMA NI USED AU VIPYA.
 
Umetisha kamanda...
 
Asante. Umejibu maswali yangu. Ninatamani sana kuwa na kiwanda cha mikate
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…