Baba wa Mariga apanga timu Simba
DORIS MALIYAGA
NOAH Wanyama ambaye ni baba wa kiungo wa Inter Milan ya Italia, Mc Donald Mariga amemwambia kocha wa Simba Patrick Phiri kama anataka kufanya vizuri kwenye michuano ya Kimataifa apange kikosi walichoanza nacho kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya FC Leopard ya Kenya.
Kikosi hicho kilikuwa na Juma Kaseja,Salum Kanon, Juma Nyoso, Jerry Santo, Ally Shiboli, Mbwana Samatta, Abdulhalim Humud, Aziz Gilla, Juma Jabu, Shija Mkina na Nico Nyagawa na akasema kama watashirikiana vilivyo watashangaza kwenye Ligi ya Mabingwa.
Wanyama ambaye ni kocha wa FC Leopard "Kikosi hicho ndicho kitamfaa kina ubora japo wanachoka haraka na ulinzi pia ufanyiwe marekebisho lakini cha pili kilikuwa na makosa mengi sana,
��alisema Wanyama akizungumzia kikosi cha pili ambacho waliongezeka Amir Maftah, Rashid Gumbo, Hillary Echessa, Mohamed Banka, Meshack Abel, Kelvin Chale, Mussa Mgosi na Ally Mustapha �Barthez�.