Michepuko matatizo kwa wanandoa

4/46 ni nyingi mkuu, hii ni karibu 10%, na hizo ni zile tu unazozijua wewe. Kumbuka lengo la Mungu ni kuwa watu waishi pamoja mpaka kifo kiwatenganishe. Kwahiyo ukiona 10% ya ndoa zinavunjika ujue kuna tatizo. Ukweli ni kwamba ndoa nyingi ziko kwenye matatizo sana na isingekuwa kuogopa sheria ya Mungu ya kutoachana basi naamini nyingi sana zingevunjika. Kitu kingine kinachosababisha watu wavumilie kwenye ndoa ni complications zinazotokana na kuachana, kwa mfano kugawana mali, mustakabali wa watoto, n.k. Tulio kwenye ndoa tunafahamu ndoa nyingi ziko matatizoni, na sababu kubwa ni kukosa uaminifu kati ya wanandoa.
 
Bora umesema mkuu...Hiki ni kizazi hatari sana
 
Kwa hyo ndoa ni mtihani..Na wengine hatupendi mitihani sasa sijui itakuwaje. Nilitegemea ndoa iwe ni furaha na sio mtihani au unaonaje mkuu
Ndo maana yake,hakika ndoa ni Mtihani,Ikiwa wewe utaifurahia ndoa yako basi ujue wewe umeufauru huo mtihani.
 
Hivi na kile cheti kinakuwaga na pass marks.

Yaani kitu kama grade au gpa.

Maana huo mtihani wa kupewa cheti kwanza na ku graduate ndo uingie kwenye hicho chumba simchezo.
Kile cheti sio ishu,matokeo ya mtihani wako yatakuja kujulikana mwishoni unapokuwa unafunga Ukurasa wa maisha yako hapa Duniani.
 
Ndoa si kwa kila mtu. Usipoitamani usiingie..ukiingia vizuri sana...ikikushinda sepa.
 


At least umekuja na statistics
 
Kukaa mbali mbali na mtu siyo sawa na kuishi nae kila siku... Poleni sana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…