Michango ya harusi vs graduation ceremonies!!

if you think it was right, then no regret can happen!
 

Mkuu, ni sawa na kumuona mtu anayewaelimisha wananchi waache tabia ya kuvunja maghala ya nafaka kwa ajili ya kutengeneza pombe wakati wa sherehe kwamba huyo ni anti-social!!!! What type of socialization ru talking about that doesn't care about priority?! If so, i better announce to the wholly world that am anti-social than spending the limited resources available for socialization!!!
 
Ni kweli, ingawaje nina elimu ya chuo kikuu lakini sijawahi kuvaa joho!! Hata hivyo, hadi leo sijajutia uamuzi wangu!!!!
Kwani kuvaa joho kulihitaji hizo milioni? Kwa nini usingeenda kujumuika na wenzako chuoni (ambayo haihitaji hela) and then ukaendelea na msimamo wako wa kususia sherehe? Ni sawa na bwana harusi asusie ndoa kanisani, akidhani atakuwa amesevu gharama, kumbe angeweza kuhudhuria kanisani na kufunga ndoa halafu asiingie ukumbini kwenye sherehe, sasa wewe ni sawa na kusema hukufunga ndoa na hukuhudhuria sherehe eti kisa unaweza kuishi tu na mkeo/mmeo bila wasi wasi !!
 

Mtindio,
Kama unadhani kufuata ujinga wa hao ndugu ni kutoambilikia basi tuombe Mungu taifa lisiwe na watu kama wewe. Wewe umetoa ajira kwa huyu mwenzetu. Mchangiaji huyu anatakiwa kuwa mfano. Mjinga ni mjinga tu habadiliki eti kwa vile ni ndugu, baba, mama au shangazi.

Ukibadilika kama mwenzetu utakuwa umesaidia kuondoa janga hili la ujinga.
Hivi unajua ni idadi gani ya wajinga wanaoshindwa kufanya mambo yao kwa visingizio vya wanajamii kama ndugu, baba, mama, mjomba na marafiki.

Maendeleo hayana cha urafiki, ubaba, umama.
Saidia kukomboa fikra za kijinga zilizojifunika kwenye koti la utii kwa ndugu.
 

Sasa Kususa Kwako kulikufanya ukose yote! Mtaji ulikosa, sherehe hukufanya (ukainyima raha nafsi yako) na pia uliwakosea wazazi kwa kutowasikiliza.

Hapa tujifunze kitu kimoja: Kwamba kama hatuwezi kufaidika kwa kugoma, bora tusigome (if you can't fight them , then join them)
 

Mawazo ya kimapinduzi kama haya yanahitajika sana, Malcolm X alisema kama watu weusi wa Marekani wangekuwa wanaweka juhudi za kujiendeleza kama wanavyoweka katika jitihada za ulimbwende wa nywele zao basi wangekuwa mbali sana.

Na sisi ni hivyo hivyo, keeping up with the Joneses kwa siku moja halafu kesho chali. Waswahili walisema "Mali bila daftari hupotea bila habari".It is time to keep it simple, tamaa za kufanya vitu vikubwa nje ya uwezo wetu zitatuingiza katika vishawishi vya ufisadi au kuwatwika ndugu jamaa na marafiki mizigo wasiyoiweza, na kwa tamaduni zetu mbovumbovu watu wanajisikia obligated kutoa hata senti tano nyekundu ya mwisho ilimradi wasionekane wachawi na ma party poopers.

Kufurahia shughuli si lazima iwe ya gharama sana, ubunifu unaotakiwa ukiwekwa shughuli isiyo na gharama itafana sana, tatizo tunataka kutumia pesa kama fimbo ya kumaliza kila tatizo.
 
Sasa Kususa Kwako kulikufanya ukose yote! Mtaji ulikosa, sherehe hukufanya (ukainyima raha nafsi yako) na pia uliwakosea wazazi kwa kutowasikiliza.

Wewe una akili sana mkuu..nikukwaa u-Prezidaa nitakupa u-Lowasa..lol
 
Je, wazazi walikubaliana na wazo zima la wewe kujiairi?
Je, walikubaliana na aina ya biashara unayotaka kufanya?
Je, hakukuwa na mivutano mingine ya kijamii nyumbani juu ya maisha yako baada ya chuo?

Kama majibu ya maswali hayo yote ni NDIO. Basi ulikuwa sahihi kukata kushiriki katika matumizi ya 1.5 mil in a couple of hours insted of investing it for a better future. Ila iwapo wazazi for any reason hawakuunga mkono swala zima la wewe kujiajiri au kujihusisha na biashara uliyopropose then hukupaswa kugomea sherehe, kwa sababu that way utakuwa unatumia nguvu kulazimisha wakubaliane na jambo ambalo hukufanikiwa kuwaconvince kuwa ni sahihi.

Pole kwa kukutana na challenges hizo.

Ningependa kujua, nini kilitokea baadae? Je, umeshapata kazi hivi sasa?
 
Pole sana, ila what i can say is this,ungewasikiliza wazazi wako kwa kile ambacho waliplan kufanya kwa ajili yako na kukaa kutafakari kwa kina kuhusu hilo swala,wazazi wako wanaelewa kabisa kuwa uko mtaani unasota,na walipoamua pia kufanya sherehe walikuwa wanaelewa kuwa bado hujapata ajira, Mtazamo wangu ungewasikiliza huwezi jua walikua wameandaa nini kwa ajili yako kwenye hiyo sherehe,yawezekana kabisa walipanga hata kukupa zaidi ya hizo zilizotumika katika hiyo sherehe,maana haiwezekani kufanya sherehe bila kuwa na zawadi,nionanvyo walikuwa na malengo mazuri kabisa na yawezekana baada ya sherehe ungepata mtaji wa kufanya hiyo biashara uliokuwa umeiplan.

kingine unajua kabla hujaamua kufanya kitu tunapaswa kufikiri prons and cons za lili jambo ambalo tunataka kufanya,misimamo mingine huwa inasababisha tunateseka bila sababu,wakati hatukupasa kuteseka kihivyo,kweli misimamo mngine ni mazuri ila kuna jambo na jambo la kuwa na misimamo ambayo hutabadilishwa.
Ni hayo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…