Fikiria unapengine miaka 50 au 60, inamaana miaka yako ya kuishi iliyobakia hapa duniani NI pengine 10, 20 au 30 hivi na hii ni kwa mujibu wa Biblia.
Unakuta kwa umri wako wa sasa ndio umebobea kwenye Kuiba mali za watu kwa nafasi yako;
Kumbuka huwezi kutubu, toba inayokubalika huku umejilimbikizia mali za dhuluma ndani.....na pengine unaendelea kudhulumu (kujilimbikizia)
Tusichukulie mzaha; SIKU ZA MWISHO NI NGUMU SANA ZAIDI YA UGUMU WOWOTE UMEWAHI KUUWAZIA HAPA DUNIANI....
Mali zako, Watoto wako, marafiki zako, mchungaji/sheikh wote hawataweza kukusaidia chochote!
Unakuta kwa umri wako wa sasa ndio umebobea kwenye Kuiba mali za watu kwa nafasi yako;
- Unadhulumu watu hasa wasio nawa kuwasemea, masikini, mayatima nk
- Unapindisha sheria ILI ujinufaishe mwenyewe,
- Unatesa watu kwa uchawi na ushirikina kwa sababu ya wivu na husuda
- Una ua watu kwa tamaa ili uzidi kujitajirisha
- Ukifanya biashara unapunja watu kwenye Mizani ili uzidi kuwa tajiri
- Unachukua mashamba, viwanja nk unajilimbikizia halafu baada ya miaka 20/30 haupo tena
- Unanyima watoto wa masikini nafasi za kazi unawapa wenye sifa za kuunga unga wenye hela
- unatumia hela ya wizi kujenga majumba ya kifahari kila pahala kama kilivyokuwa kizaz cha Dhamud kilicho angamizwa na Mungu mwenyewe...
Kumbuka huwezi kutubu, toba inayokubalika huku umejilimbikizia mali za dhuluma ndani.....na pengine unaendelea kudhulumu (kujilimbikizia)
Tusichukulie mzaha; SIKU ZA MWISHO NI NGUMU SANA ZAIDI YA UGUMU WOWOTE UMEWAHI KUUWAZIA HAPA DUNIANI....
Mali zako, Watoto wako, marafiki zako, mchungaji/sheikh wote hawataweza kukusaidia chochote!