charz91
Member
- Aug 10, 2013
- 34
- 12
MIAKA 53 YA UHURU, NI UHURU KWA NCHI
GANI?
Leo 9 Dec 2014 Ni mwaka wa 53 tangu ile nchi
iliyofahamika zamani kama Jamhuri ya watu wa
Tanganyika ijipatie uhuru wake mnamo 9 Dec
1961.
Hakuna siri, na wala sidhani kama kuna mtu
yeyote anaweza kubisha hili la kwamba Jamhuri
ya watu wa Tanganyika iliuliwa mnamo April 26
1964, katika ile ajari mbaya ya "Muungano wa
kipekee kati yake na Jamhuri ya watu wa
Zanzibar." Wala sitaki kujishughurisha kutoa
ufafanuzi kwenye jambo hili, kwa maana hata
wale wanaopiga kelele juu ya Uhai wa Tanganyika
wana ukweli ndani ya mioyo yao kwamba Jamhuri
ya Tanganyika ilikufa kwa hila siku ile ya April 26,
1964.
Nirejee basi kwenye kichwa cha makala yangu,
kilichohoji MIAKA 53 YA UHURU, NI UHURU KWA
NCHI GANI? Naam, lazima tujiulize Je, ni Nchi
gani hiyo ambayo hii leo inaadhimishiwa miaka
hiyo 53? Kwa maana kama Tanganyika mbona
ilishakufa, au kama uhuru wa leo ni uhuru kwa
Tanzania Bara kama wasemavyo watawala wetu
ama ninavyomsikia huyu mtangazaji wa TBC Taifa
akitangaza, ni vyema hawa watawala wetu na
chombo chao hiki wakatoa semina kwa umma,
wakituelimisha nasi tukaijua hiyo Tanzania Bara.
Lakini Kama tunajua kuwa Tanganyika ilikwisha
zikwa tangu mwaka 1964, sasa iwaje leo
tuadhimishe siku yake ya kuzaliwa? Hivi toka lini
tukafanya birthday ya mtu ambaye
amekwishakufa?
Kwakweli ni ujuha mkubwa kusheherekea kitu
ambacho sisi wenyewe tunakubali kuwa
kilikwishakufa, kwani si ni sisi ambao tuliingia
Bunge la katiba tukiipinga na kuikataa hii nchi
ambayo leo tunaisheherekea siku ya kuzaliwa
kwake?, si ni sisi wenyewe ambao tuliwatukana
wale wengine waliokuwa na ndoto za kumfumfua
huyu tunayemsheherekea leo, sasa kwanini? leo
sisi wenyewe tutumie mabilioni kumkumbuka
yule tusiyemtaka?
Wakati wenzangu wakiwa kule shamba la bibi
wakiimba na kusheherekea siku yakuzaliwa ya
mfu, mimi niko nyumbani kwangu nikiandaa
chakula cha mchana na kwavile nimejiridhisha
yakuwa wako pale wakifanya mwendelezo wa wizi
wa mali ya Umma, wakitumia rasilimali za taifa
bila tija, wakifisadi na kutafuna matunda ya nchi
waliyoiua, kwakweli sina haja yakuwafatilia zaidi
wacha nijilie ugali wangu na samaki, baadae
nikafurahie mapumziko kwavile leo ni siku
yakuwa huru.
TUTAFAKARI SIKU HII NA TUJIULIZE YALIYOTOKEA
BUNGE LA KATIBA, NA ITOSHE KUSEMA ULE
ULIKUWA UJUHA?
GANI?
Leo 9 Dec 2014 Ni mwaka wa 53 tangu ile nchi
iliyofahamika zamani kama Jamhuri ya watu wa
Tanganyika ijipatie uhuru wake mnamo 9 Dec
1961.
Hakuna siri, na wala sidhani kama kuna mtu
yeyote anaweza kubisha hili la kwamba Jamhuri
ya watu wa Tanganyika iliuliwa mnamo April 26
1964, katika ile ajari mbaya ya "Muungano wa
kipekee kati yake na Jamhuri ya watu wa
Zanzibar." Wala sitaki kujishughurisha kutoa
ufafanuzi kwenye jambo hili, kwa maana hata
wale wanaopiga kelele juu ya Uhai wa Tanganyika
wana ukweli ndani ya mioyo yao kwamba Jamhuri
ya Tanganyika ilikufa kwa hila siku ile ya April 26,
1964.
Nirejee basi kwenye kichwa cha makala yangu,
kilichohoji MIAKA 53 YA UHURU, NI UHURU KWA
NCHI GANI? Naam, lazima tujiulize Je, ni Nchi
gani hiyo ambayo hii leo inaadhimishiwa miaka
hiyo 53? Kwa maana kama Tanganyika mbona
ilishakufa, au kama uhuru wa leo ni uhuru kwa
Tanzania Bara kama wasemavyo watawala wetu
ama ninavyomsikia huyu mtangazaji wa TBC Taifa
akitangaza, ni vyema hawa watawala wetu na
chombo chao hiki wakatoa semina kwa umma,
wakituelimisha nasi tukaijua hiyo Tanzania Bara.
Lakini Kama tunajua kuwa Tanganyika ilikwisha
zikwa tangu mwaka 1964, sasa iwaje leo
tuadhimishe siku yake ya kuzaliwa? Hivi toka lini
tukafanya birthday ya mtu ambaye
amekwishakufa?
Kwakweli ni ujuha mkubwa kusheherekea kitu
ambacho sisi wenyewe tunakubali kuwa
kilikwishakufa, kwani si ni sisi ambao tuliingia
Bunge la katiba tukiipinga na kuikataa hii nchi
ambayo leo tunaisheherekea siku ya kuzaliwa
kwake?, si ni sisi wenyewe ambao tuliwatukana
wale wengine waliokuwa na ndoto za kumfumfua
huyu tunayemsheherekea leo, sasa kwanini? leo
sisi wenyewe tutumie mabilioni kumkumbuka
yule tusiyemtaka?
Wakati wenzangu wakiwa kule shamba la bibi
wakiimba na kusheherekea siku yakuzaliwa ya
mfu, mimi niko nyumbani kwangu nikiandaa
chakula cha mchana na kwavile nimejiridhisha
yakuwa wako pale wakifanya mwendelezo wa wizi
wa mali ya Umma, wakitumia rasilimali za taifa
bila tija, wakifisadi na kutafuna matunda ya nchi
waliyoiua, kwakweli sina haja yakuwafatilia zaidi
wacha nijilie ugali wangu na samaki, baadae
nikafurahie mapumziko kwavile leo ni siku
yakuwa huru.
TUTAFAKARI SIKU HII NA TUJIULIZE YALIYOTOKEA
BUNGE LA KATIBA, NA ITOSHE KUSEMA ULE
ULIKUWA UJUHA?