Mheshimiwa Rais, mimi ni Mstaafu Serikalini. Niliitumikia Serikali kwenye Idara ya Afya kwa muda wa miaka 39 mpaka nilipostaafu mwaka 2019. Katika kipindi chote hiko, nimesaidia kuwalea Vijana watatu wa kike ambao Wazazi wao waliniletea Mjini nisaidie kuwasomesha kutokana na wao kukosa fedha au kutokuwa na mwamko wa kuwasomesha. Nililibeba jukumu hilo kama Mzazi.
Mabinti wawili niliwasomesha mpaka walipomaliza Kidato cha Nne mwaka 2014. Wakaendelea na Kidato cha Tano na kumaliza Kidato cha Sita mwaka 2017. Wote wakachaguliwa kwenda JKT kwa mujibu wa Sheria. Matokeo yalipotoka mmoja alipata Division One na mwingine Division Two.
Baada ya kumaliza Mikataba yao huko JKT, wamekuwa wakijihusisha na shughuli ndogondogo kwani uwezo wa Mstaafu mimi kuwalipia Ada Chuo Kikuu sina kwa sasa maana walijaribu kuomba mikopo (Loan Board) lakini hawakupata. Mnamo mwezi August 2021, Jeshi la Polisi lilitangaza Ajita kwa vijana wenye Elimu ya Kidato cha 4, 6 na Chuo Kikuu.
Vijana wangu hawa waliomba nafasi hizo LAKINI wote WAMEKOSA kisa walifaulu sana (Division One na Two). Kijana wa Tatu yeye nilimsomesha mpaka Kidato cha Nne na alipata Division Four (Point 27), pia alipitia JKT lakini nae AMEKOSA nafasi hizo kisa alipata Point 27 na wanaotakiwa ni wenye kuanzia Point 29-32!!.
Mheshimiwa Rais wewe ni Mama, ni kweli kama Nchi tumefikia huko kwamba KUFAULU ni disqualification ya kupata kazi!!!
TAFADHALI Mheshimiwa Rais, tengua utaratibu huo wa Jeshi la Polisi. Ni vema wangewaita wote wenye 1-4 waje wapambane kwenye Usaili na sio kuwabagua waliofeli.
NAKUOMBA Mheshimiwa Rais liangalie suala hili kwa jicho la huruma
Mabinti wawili niliwasomesha mpaka walipomaliza Kidato cha Nne mwaka 2014. Wakaendelea na Kidato cha Tano na kumaliza Kidato cha Sita mwaka 2017. Wote wakachaguliwa kwenda JKT kwa mujibu wa Sheria. Matokeo yalipotoka mmoja alipata Division One na mwingine Division Two.
Baada ya kumaliza Mikataba yao huko JKT, wamekuwa wakijihusisha na shughuli ndogondogo kwani uwezo wa Mstaafu mimi kuwalipia Ada Chuo Kikuu sina kwa sasa maana walijaribu kuomba mikopo (Loan Board) lakini hawakupata. Mnamo mwezi August 2021, Jeshi la Polisi lilitangaza Ajita kwa vijana wenye Elimu ya Kidato cha 4, 6 na Chuo Kikuu.
Vijana wangu hawa waliomba nafasi hizo LAKINI wote WAMEKOSA kisa walifaulu sana (Division One na Two). Kijana wa Tatu yeye nilimsomesha mpaka Kidato cha Nne na alipata Division Four (Point 27), pia alipitia JKT lakini nae AMEKOSA nafasi hizo kisa alipata Point 27 na wanaotakiwa ni wenye kuanzia Point 29-32!!.
Mheshimiwa Rais wewe ni Mama, ni kweli kama Nchi tumefikia huko kwamba KUFAULU ni disqualification ya kupata kazi!!!
TAFADHALI Mheshimiwa Rais, tengua utaratibu huo wa Jeshi la Polisi. Ni vema wangewaita wote wenye 1-4 waje wapambane kwenye Usaili na sio kuwabagua waliofeli.
NAKUOMBA Mheshimiwa Rais liangalie suala hili kwa jicho la huruma