Mheshimiwa Makonda Njoo Temeke usikie mabomu ya samaki yanavyorindima

Eddie Juma

Member
Mar 22, 2016
16
5
Mimi kama mdau wa masuala ya Uvuvi salama na ninayeishi karibu na bahari kwakweli bado naendelea kusikitishwa na uvuvi haramu unaoendelea katika wilaya ya Temeke ukianzia visiwa vya Sinda Mjimwema na kuendelea mpaka Buyuni, Kinachoniuma zaidi uvuvi wa mabomu siyo uvuvi wa siri bali ni aina ya njia mojawapo inayoweza kuonyesha ni kiasi gani baadhi ya viongozi wetu walivyobado usingizini.

Hivi inakuwaje miaka inapita mabomu ya kuvulia samaki bado yanaendelea kupigwa kila kukicha na hakuna viongozi wa mitaa na madiwani ambao wanaonyesha kukerwa na hali hiyo, kwani milio ya mabomu hayo yanasikika na hao ninaowaita viongozi walio usingizini aidha kwa makusudi wanalazwa na maslahi binafsi, kwani ukiachilia vikundi vya BMU ambavyo vinaendelea kupiga kelele za kuzuia uvuvi haramu hakuna viongozi wa serikali wa maeneo ya kuanzia Mjimwema, Gezaulole, Muongozo na kuendelea ambao wameonekana kuungana na kuamua kwa dhati ya kuzuia uvuvi huo.

Hali hii ndiyo imenifanya nikuombe Mkuu wa Mkoa kufuatilia na kuona ni jinsi gani utaweza kutusaidia kuzuia hali inayoendelea katika bahari ya wilaya ya Temeke ambayo ndiyo wilaya inayoongoza kwa uvuvi wa kutumia mabomu katika wilaya zote za Tanzania kutokana na taarifa ya WWF.
 
Umeongea jambo la maana na ukweli kabisa, eneo la Mjimwema, Sinda kwenda buyuni uvuvi wa mabomu umekithiri sana mchana kweupe hawana hata wasiwasi. Tunaomba kama wenye mamlaka wataona andiko hili wachukue hatua sahihi.
 
Madalali tena,au ni wavuvi ,,,,,, mabomu hayo wanayovulia ni yale ya kivita au yepi mkuu
Ni mabom flani hivi yapo kama baruti na yanaua kama ukikosea kuliripua huwa wanazama chini ya maji wana litegesha halafu wanapanda juu na ki uzi chake kisha wanaisogeza boti umbali kama mita 100 hivi ndio wanawasha ule uzi ukishika moto unatambaa mpaka ndani ya maji kwenda kuliripua lile bomu.Baada ya hapo ni utitiri wa mizoga ya samaki yaani kila kiumbe kilichopo eneo hilo kinavurugika.
 
Ni mabom flani hivi yapo kama baruti na yanaua kama ukikosea kuliripua huwa wanazama chini ya maji wana litegesha halafu wanapanda juu na ki uzi chake kisha wanaisogeza boti umbali kama mita 100 hivi ndio wanawasha ule uzi ukishika moto unatambaa mpaka ndani ya maji kwenda kuliripua lile bomu.Baada ya hapo ni utitiri wa mizoga ya samaki yaani kila kiumbe kilichopo eneo hilo kinavurugika.
Ndugu yangu Lavan, nashukuru kwa kunipa support kwenye tatizo hili manake nilishatuma taarifa zinazofanana na tatizo hili lakini response ya wadau uilikuwa ndogo sana, nashukuru kwa kufikia mpaka kutoa maelezo hayo, naomba wadau tupigie kelele kuhusu suala la uvuvi kwani ni aibu ya Taifa letu, achilia mbali uharibifu unaofanyika, fikiria meli zinazoshusha mafuta ndiyo mashahidi wakubwa wa mabomu hayo kwani kule wanaposhusha mafuta siyo mbali na hujuma hiyo inapofanywa je wale wageni wanatuchukuliaje sisi kama Taifa??!! , narudia kwa kuwaomba wadau wote wa Jamii forums tupigie kelele kuhusu uvuvi huu haramu ukomeshwe kwa kila anayemjua mtu mwenye uwezo wa kuongeza nguvu katika kuzuia naomba amjulishe, kwani tumechoka BMU peke yake hazitoshi kuzuia kwani hazina mfuko maalum na wala ufundi na uwezo wa kupambana na wapigaji mabomu waliopo baharini na boti zao.
 
Back
Top Bottom