Mh! Maji yamenifika shingoni

Mh! Maji yamenifika shingoni

Shida na raha

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2014
Posts
3,773
Reaction score
3,474
Habari zenu wana MMU rudi kwenye mada hapo juu.

Sikuona shida kumtumia sms ya kwamba simtaki tena maana hana mapenzi ya kweli kwangu.

POINT: Niiko na Msichana wangu yapata miaka miwili sasa niliishi nae kwenye mazingira magumu, nilimsaidia kwa kila hali ilimradi nimridhishe asiwe na matamanio na vitu vya watu.

Punde, akapata safari ya kwenda Dar kwa shangazi yake ambae ni mwalim, maisha yakaanza kumkubali akaanza kupata kamwili kidogo, awali ya yote alikua ananisumbua kila kukicha nimsaidie hiki na kile, ikafika kipindi nikamwambia nataka tuonane mimi na wewe, kwavile mda umekwenda na bado tuko wapenzi, akakubaliana na lile akaniambia nimtumie nauli ili aje, sikua na tabu nikamtumia. Baada ya kumtumia akaanza visingizio eti amekatazwa na shangazi asije ili alinde nyumba.

Nikakubali na hili ikapita mwezi, nikamuuliza "bado hajakuruhusu shangazi yako?" akanijibu bado nikapotezea na ikafika kipindi mambo yangu yakawa mabaya kidogo nikamwelezea anitumie 20, na 10 achukue yeye akashindwa akabaki ananijibu "nikikutumia hii nitakufa maskini" nikaona isiwe tabu na hilo pia nikaachana nalo ikafika kipindi nikamuonea huruma sana nikamtumia kiwango cha pesa(.....) nikamwambia fanya biashara zako, ukipata faida mtaji nirudishie, kweli alifanikiwa na zaidi ila alikataa kunirudishia mtaji hadi leo.

Na hilo pia nimeachana nalo, nikabaki najiuliza huyu ananipenda kweli ama yuko kimaslahi zaidi?Nilipata jibu baada ya kumwambia njoo sasa tukutane akanijibu kwamba hawezi kuacha biashara na kuja kwangu kwanza nimuache, cha kushangaza zaidi hanipigii sim mpaka nimtafute mimi, nikamwambia basi jaribu kuweka voda maana ndo naitumia sana ila nayo akakataa eti watu wake wote wako airtel, ana line mbili za airtel na voda moja kwanini asiweke airtel 1 na voda 1?

Juzi akanipigia simu nikajua leo nimepata bahati ya kupigiwa na yeye lakini wapi, kumbe alikua na yake angalia sasa eti kunipigia kote sim ananiuliza picha zangu mbona kwenye fb sizioni umezifuta, alikua na maana yake kuniuliza hivyo maana akaunti yake na namba za siri niko nazo na nilishawahi kufanya hivyo.Wakati nina kama wiki sijaingia fb na kibaya zaidi nimeshaanza mahusiano na mwanamke mwengine wa kizanzibar na nimeshamwelezea yote haya, jamani mwenye ushauri, pendekezo, msaada wa kimawazo anipe matusi si pahala pake hauna cha kujenga pita kama ushuzi.
 
mkuu maneno mengiiiii kumbe jibu la tatizo unalo...mpende huyo mzazibar kwa dhati na huyo mwngne achana naye.
 
We kama umeamua kuanzisha maisha mapya just move on. Huyo wa kwanza alishaonesha kukupotezea na wewe mpotezee
 
Wakati nina kama wiki sijaingia fb na kibaya zaidi nimeshaanza mahusiano na mwanamke mwengine wa kizanzibar na nimeshamwelezea yote haya, jamani mwenye ushauri, pendekezo, msaada wa kimawazo anipe matusi si pahala pake hauna cha kujenga pita kama ushuzi.

eti kibaya zaidi...mi nikajua jambo la heri.....
 
Uwe unaweka hata vituo na koma basi ukiwa unaandika, kah!! Koma na vituo vya kutafta.

Back to the topic!! Huyo mdada alivoenda Dar keshakutana na wajanja wa mjini. Kwahiyo ni kama vile unajipendekeza. Kwanini ujipendekeze kwa mwanamke? Chukua hatua
 
Teh Teh ya kupita kama ushuzi ni hatari....
 
Mkuu ikiwezekana mblok huyo binti acha mawasiliano naye ya aina yoyote.

Mtunze huyo mzenj bwana
 
Wawezaje kuanza sentensi na (sikuona shida ....) Je insha ulikuwa unaandikaje shuleni? au bado hujaanza hiyo awamu? Stori yenyewe haiko constructive in a way that we can understand it and give opinion. Can you start again please and try to be clear? JF nilitegemea iwe ya watu makini lakini kumbe kuna na wanafunzi wa kuandika sentensi?

Sijakutukana, sijakubeza ila nataka nikusaidie ila sikuelewi. Nisamehe kama nimekukwaza ila kama nimesema ukweli basi rudia kuandika.
 
Habari zenu wana MMU rudi kwenye mada hapo juu.

Sikuona shida kumtumia sms ya kwamba simtaki tena maana hana mapenzi ya kweli kwangu.

POINT: Niiko na Msichana wangu yapata miaka miwili sasa niliishi nae kwenye mazingira magumu, nilimsaidia kwa kila hali ilimradi nimridhishe asiwe na matamanio na vitu vya watu.

Punde, akapata safari ya kwenda Dar kwa shangazi yake ambae ni mwalim, maisha yakaanza kumkubali akaanza kupata kamwili kidogo, awali ya yote alikua ananisumbua kila kukicha nimsaidie hiki na kile, ikafika kipindi nikamwambia nataka tuonane mimi na wewe, kwavile mda umekwenda na bado tuko wapenzi, akakubaliana na lile akaniambia nimtumie nauli ili aje, sikua na tabu nikamtumia. Baada ya kumtumia akaanza visingizio eti amekatazwa na shangazi asije ili alinde nyumba.

Nikakubali na hili ikapita mwezi, nikamuuliza "bado hajakuruhusu shangazi yako?" akanijibu bado nikapotezea na ikafika kipindi mambo yangu yakawa mabaya kidogo nikamwelezea anitumie 20, na 10 achukue yeye akashindwa akabaki ananijibu "nikikutumia hii nitakufa maskini" nikaona isiwe tabu na hilo pia nikaachana nalo ikafika kipindi nikamuonea huruma sana nikamtumia kiwango cha pesa(.....) nikamwambia fanya biashara zako, ukipata faida mtaji nirudishie, kweli alifanikiwa na zaidi ila alikataa kunirudishia mtaji hadi leo.

Na hilo pia nimeachana nalo, nikabaki najiuliza huyu ananipenda kweli ama yuko kimaslahi zaidi?Nilipata jibu baada ya kumwambia njoo sasa tukutane akanijibu kwamba hawezi kuacha biashara na kuja kwangu kwanza nimuache, cha kushangaza zaidi hanipigii sim mpaka nimtafute mimi, nikamwambia basi jaribu kuweka voda maana ndo naitumia sana ila nayo akakataa eti watu wake wote wako airtel, ana line mbili za airtel na voda moja kwanini asiweke airtel 1 na voda 1?

Juzi akanipigia simu nikajua leo nimepata bahati ya kupigiwa na yeye lakini wapi, kumbe alikua na yake angalia sasa eti kunipigia kote sim ananiuliza picha zangu mbona kwenye fb sizioni umezifuta, alikua na maana yake kuniuliza hivyo maana akaunti yake na namba za siri niko nazo na nilishawahi kufanya hivyo.Wakati nina kama wiki sijaingia fb na kibaya zaidi nimeshaanza mahusiano na mwanamke mwengine wa kizanzibar na nimeshamwelezea yote haya, jamani mwenye ushauri, pendekezo, msaada wa kimawazo anipe matusi si pahala pake hauna cha kujenga pita kama ushuzi.

pole mkuu kwa kuhuhudumia mgodi mfu ambao hata siku moja usingetoa madini. Hivi wewe huoni dem hana muda na wewe na hata chembe ya penzi kwako hana na ndio maana amekufanya Shamba la bibi we we unajitia kipofu eti unaendelea kupiga baruti mwamba ukitegemea mawe yatatoka.. achana mchwa huo anza maisha yako boss.
 
wewe mbayaa unatuambia tupite kama nini vile?hahahaaa
 
ivi inakuaje mwanaume kabisa ambaye unategemewa siku moja uwe kiongozi wa familia alafu unashindwa kutatua tatizo dogo kama hili. sasa sikiliza bhana mzee wahenga hawakukosea walivyosema FIMBO YA MBALI HAIUI NYOKA. tumia akili kwani AKILI NI MALI au umesahau kwamba AKUPAE KISOGO SI MWENZIO.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom