Habari wana JF.
Kwanza nianze kwa kukupongeza Mh. Waziri kwa hatua ambayo umeanza kuichukua, yaani hatua ya kuongoza wizara kwa kutoka Ofisini na kutizama matatizo ya wananchi yanayowakabiri yaliyo chini ya Wizara yako, kwa kweli hiyo ni hatua nzuri kabisa.
Kwanza kabisa ulianzia pale TRL kwa kusafiri na Treni kutoka DSM hadi Dodoma na wewe kujionea mwenyewe hali ya usafiri wa reli ndani ya nchi yetu Tanzania, na jana nasikia tena umefanya ziara ya kishtukiza pale katika kituo cha mabasi cha Ubungo kwa mabasi yanayoenda Mikoani, ama kwa hakika mie nakupongeza sana.
Sasa ndugu yangu Mh. Waziri nakuomba uangalie na uchukuzi wa abiria ndani ya jiji la Dar es Salaam. Mh. Waziri hali ya usafiri katika jiji la Dsm unatisha ndugu yangu. Mie binafsi nashindwa kuelewa ama ni kuongezeka kwa abiria yaani wakazi wa jiji au kupungua kwa wawekezaji katika kuwekeza kwenye usafiri huu wa daladala. Ziara yangu binafsi ilianzia jana jioni ambapo nilitokea maeneo ya katikati ya jiji, safari yangu ikianzia mnamo majira ya saa 1 jioni, kulekea Tabata, mh Waziri huwezi kuamini mbali ya kuchelewa kufika mwisho wa safari yangu pia ilinilazimu kutumia mabasi/daladala 4 hadi kufika Tabata yaani Posta-Bugurunu gari 1, Buguruni-Tabata Reli gari la 2,Tabata Reli-Tabata bima gari la 3, Tabata bima-Tabata Segerea basi la 4.
Katika mlolongo huo magari yalikuwa ya shida na kugombania na hivo kumaliza safari yangu mnamo majira ya saa 5. Ziara yangu vivyo hivyo leo asubuhi hali ni hiyo hiyo, kufika kituoni saa 12 asubuhi na kufika mjini saa 2 asubuhi.
Mh. Waziri hali ni mbaya sana, ninakuomba pia na wewe katika dhana ile ile ya kuongoza wizara kwa kutoka na kutambua matatizo ya Wananchi, ujongee na kujaribu pia usafiri wa daladala ndani ya Jiji hili la Dar es Salaam. Mh. Waziri karibu ili kwa pamoja tuone ni kwa jinsi gani maisha haya ya wakazi wa Jiji hili la Dsm yanavozidishwa ugumu.
Fanya kitu Mheshimiwa Mwakyembe na wakazi hawa wa Dsm watakukumbuka kama, tunavyowakumbuka majemedari waliopita katika jiji hili Mh. Keenje, na Mh Mwaibula. Karibu Mh.
Kwanza nianze kwa kukupongeza Mh. Waziri kwa hatua ambayo umeanza kuichukua, yaani hatua ya kuongoza wizara kwa kutoka Ofisini na kutizama matatizo ya wananchi yanayowakabiri yaliyo chini ya Wizara yako, kwa kweli hiyo ni hatua nzuri kabisa.
Kwanza kabisa ulianzia pale TRL kwa kusafiri na Treni kutoka DSM hadi Dodoma na wewe kujionea mwenyewe hali ya usafiri wa reli ndani ya nchi yetu Tanzania, na jana nasikia tena umefanya ziara ya kishtukiza pale katika kituo cha mabasi cha Ubungo kwa mabasi yanayoenda Mikoani, ama kwa hakika mie nakupongeza sana.
Sasa ndugu yangu Mh. Waziri nakuomba uangalie na uchukuzi wa abiria ndani ya jiji la Dar es Salaam. Mh. Waziri hali ya usafiri katika jiji la Dsm unatisha ndugu yangu. Mie binafsi nashindwa kuelewa ama ni kuongezeka kwa abiria yaani wakazi wa jiji au kupungua kwa wawekezaji katika kuwekeza kwenye usafiri huu wa daladala. Ziara yangu binafsi ilianzia jana jioni ambapo nilitokea maeneo ya katikati ya jiji, safari yangu ikianzia mnamo majira ya saa 1 jioni, kulekea Tabata, mh Waziri huwezi kuamini mbali ya kuchelewa kufika mwisho wa safari yangu pia ilinilazimu kutumia mabasi/daladala 4 hadi kufika Tabata yaani Posta-Bugurunu gari 1, Buguruni-Tabata Reli gari la 2,Tabata Reli-Tabata bima gari la 3, Tabata bima-Tabata Segerea basi la 4.
Katika mlolongo huo magari yalikuwa ya shida na kugombania na hivo kumaliza safari yangu mnamo majira ya saa 5. Ziara yangu vivyo hivyo leo asubuhi hali ni hiyo hiyo, kufika kituoni saa 12 asubuhi na kufika mjini saa 2 asubuhi.
Mh. Waziri hali ni mbaya sana, ninakuomba pia na wewe katika dhana ile ile ya kuongoza wizara kwa kutoka na kutambua matatizo ya Wananchi, ujongee na kujaribu pia usafiri wa daladala ndani ya Jiji hili la Dar es Salaam. Mh. Waziri karibu ili kwa pamoja tuone ni kwa jinsi gani maisha haya ya wakazi wa Jiji hili la Dsm yanavozidishwa ugumu.
Fanya kitu Mheshimiwa Mwakyembe na wakazi hawa wa Dsm watakukumbuka kama, tunavyowakumbuka majemedari waliopita katika jiji hili Mh. Keenje, na Mh Mwaibula. Karibu Mh.