Kuna taarifa kuwa kuna mgomo umeanza wa daladala jiji la Mwanza. Mwenye ukweli amwage hapa ili tujue chanzo chake ni nini?
Wadau kama tutakumbuka vizuri,jana katika taarifa za habari kulikuwa na habari ya wamachinga kupewa maeneo mawili katikati ya jiji la mwanza na mkuu mpya wa mkoa bwa magesa mulongo,maeneo waliyopewa ni standi ya Tanganyika na ile ya magari ya kwenda airport kutokea Igoma.katika pitapita zangu asubuhi ya leo mjini nilikuta machinga wameamka usiku kuwahi maeneo katika sehemu hizo,hivyo kukawa top hakuna gari kuingia wala kusha pale Stand ya Tanganyika,na ile nyingine.Kufuatia kitendo hicho,watu wa daladala wamejipanga vyema hasa wale waliokuwa wanatumia maeneo hayo wamegogoma,na wamezifunga barabara zote za katikati ya mji kwa kuegesha magari barabarani na wao kushuka.
My take: Wakati wa Ndikilo,kulikuwa na mpango wa halmashauri ya jiji la Mwanza kusafisha mji kwa kuwatoa wamachinga katikati ya mji,zoezi lililotumia million mia 2,sasa iweje leo warudishwe tena kwa kupewa maeneo makubwa zaidi?nadhani Mulongo anafanya hivi kuwafuta machozi machinga wa Mwanza,ili kumpiga kumbo Wenje ambae amekuwa mstari wa mbele kuwatetea,ili kuirahisishia CCM kupiga kampeni vizuri katika uchaguzi mkuu ujao,na baada ya hapo,wawafukuze tena.
Magesa hii ni Mwanza,usipotulia na kutumia Busara utaomba uhamisho mwenyewe,ila ukiwa mstaarabu kama wana Mwanza walivyo,hautatamani kuhamishwa.